Usafiri wa kwenda zimbabwe (harare)

Usafiri wa kwenda zimbabwe (harare)

Chilangachiba

Member
Joined
Oct 2, 2012
Posts
26
Reaction score
2
Hi, ndugu zangu, habari za leo! Ninasafari ya kwenda Zimbabwe mwisho wa mwezi huu, naomba kujua kama upo usafiri wa mabasi wa kutoka Dar kwenda Harare. Na je nauli ni shilingi ngapi kwa sasa. Naomba anayefahamu anijulishe.

Asanteni sana
 
Mkuu sijui uunganishe from Mbeya? Sina hakika kama kuna straight away mpaka kwa Mugabe.
 
Mkuu sijui uunganishe from Mbeya? Sina hakika kama kuna straight away mpaka kwa Mugabe.

Ipo. Kuna mabasi yanajulikana kama TAQWA yanaenda Harare, Lusaka, Lubumbashi... na ni kila siku. Ila jiandae maana yamekaa kimizigo mizigo zaidi. Ofisi zipo ubungo jirani na Terminal.
 
Njia ya mkato unaweza kuchukua boti hadi zimbabwe, kwani iko upande wa bahari ya hindi !!:confused2:
 
Ipo. Kuna mabasi yanajulikana kama TAQWA yanaenda Harare, Lusaka, Lubumbashi... na ni kila siku. Ila jiandae maana yamekaa kimizigo mizigo zaidi. Ofisi zipo ubungo jirani na Terminal.
aah, kumbe ndo TAQWA. jamaa inabidi ajiandae kukaa mpaka siti ibonyee.
 
Ipo. Kuna mabasi yanajulikana kama TAQWA yanaenda Harare, Lusaka, Lubumbashi... na ni kila siku. Ila jiandae maana yamekaa kimizigo mizigo zaidi. Ofisi zipo ubungo jirani na Terminal.

Sawa kabisa,Taqwa nauli toka Dar mpaka Zimbabwe (harare) wanachukua 120000.Ila ndio hivyo ni zaidi ya lory,ingawa si wakati wote!
 
Hamna kampuni inayopeleka mabasi hizo long trip zaidi ya TAQWA,Tatizo lake jamaa huwa hawana haraka utakaa
kwenye bus mpaka tigo iote sugu!!seat zake hazichoshi ni sleeping coach
 
Sawa kabisa,Taqwa nauli toka Dar mpaka Zimbabwe (harare) wanachukua 120,000.Ila ndio hivyo ni zaidi ya lory,ingawa si wakati wote!
Kha, mbona ghali hivyo??
Yaani kutoka sehemu moja ya Muungano hadi ingine ni gharama namna hii? Mulugo inakuaje hii?
 
Kuna TAQWA na FALCON zinaenda Zimbabwe, Tatizo kubwa hayo magari ni ya miashara ya kubeba mizigo, Wazimbabwe wanakuja sana Tanzania kuchukua nguo na vitu vingine, kwa hiyo, TAQWA na FALCON ndio njia yao ya kubebea mizigo

unaenda Zimbabwe sehemu gani, hebu sema nikueleze njia nzuri
 
Unaweza pia kuchukua magari yanyokwenda Lusaka na pale Lusaka kuna magari yanayokwenda Harare kila siku.
 
Mwana fanya hivi, chukua basi hadi tunduma, then ukifika tunduma vuka mpaka panda mabasi ya Lusaka. Ukifika Lusaka (inter bus terminal) kuna mabasi mazuri sana, (sidhani kama kwa sasa bongo tunayo mabasi mazuri kama yale) kila siku yanaenda moja kwa moja harare. Achana kabisa na sijui mabasi ya taqwa and the likes yanayotoka dar kuelekea lusaka hadi harare, I'm telling you utafika harare baada ya mwezi mkuu. Nauli hope haiwezi kuzidi kilo ya bongo, lakini inabidi uwe fresh mfukoni au vip?.
 
Mwana fanya hivi, chukua basi hadi tunduma, then ukifika tunduma vuka mpaka panda mabasi ya Lusaka. Ukifika Lusaka (inter bus terminal) kuna mabasi mazuri sana, (sidhani kama kwa sasa bongo tunayo mabasi mazuri kama yale) kila siku yanaenda moja kwa moja harare. Achana kabisa na sijui mabasi ya taqwa and the likes yanayotoka dar kuelekea lusaka hadi harare, I'm telling you utafika harare baada ya mwezi mkuu. Nauli hope haiwezi kuzidi kilo ya bongo, lakini inabidi uwe fresh mfukoni au vip?.

Kilo ya bongo ni sawa na bei gani ya Zimbabwe?
 
Back
Top Bottom