Usafiri Dodoma to Arusha/Moshi

Usafiri Dodoma to Arusha/Moshi

kitalembwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2014
Posts
6,143
Reaction score
15,757
Wakuu,,,,

Mm sio mwenyeji wa Dom , japo naendaga mara kadhaa na kurudi! Sijawahi kukaa zadi ya siku nne, nikimaliza kilichonipeleka narudi ! Sana Sana napajua nyerere square, bunge , waswanu na bambalaga!!

Back to the topic, kuna rafiki yangu yupo huko, anahitaji kusafiri usiku wa tar 24 kwenda Arusha/moshi ! Je Ni usafiri gani anaweza kupata ? Ni mtoto wa kike, ni muoga pia kiusalama hataweza kupanda malori ama hizi private ! Je Dom hakunaga coaster ambazo ni special zinasafiri usiku ? Hata huu msimu wa sikukuu pia ?

Ingekuwa ni Dar Ni rahisi Sana, hata kama sio msimu wa sikukuu coaster zinazosafiri usiku zipo !

Je kwa Dom Kama zipo zinazoenda Arusha/Moshi zipo zinapark wapi ? Au wapi akabahatishe mabus makubwa ? (Muda ni kuanzia saa moja mpaka saa tatu usiku) Mtaniuliza kwa Nini asafiri usiku? Majukumu yamembana likizo yake inaanza tar 24 jioni na anataka akajumuike na ndugu zake !
 
Hiyo saa moja aende pale stand ya Machame ndo njia ya Arusha anaweza pata Machame yenyewe ama private. Akikaa mpaka saa mbili hawezi kosa gari pale.
 
Aende pale Machame atapata private hata inayoendeshwa na mdada au akate tiketi leo kwa ajili ya tarehe 24.
Au apande gari hadi Kondoa then apande Coaster from Kondoa to Arusha.
 
Hiyo saa moja aende pale stand ya Machame ndo njia ya Arusha anaweza pata Machame yenyewe ama private. Akikaa mpaka saa mbili hawezi kosa gari pale.
Shukran boss ntamuelekeza hivyo
 
Aende pale Machame atapata private hata inayoendeshwa na mdada au akate tiketi leo kwa ajili ya tarehe 24.
Au apande gari hadi Kondoa then apande Coaster from Kondoa to Arusha.
Hio ticket atakayokata ni ya bus,,, ? Linasafiri usiku ?
 
Barabara Hiyo Kwa Muda Huo Aende Machame Ila Kipindi Hiki Hatakosa Ila Lazima Awe Mvumilivu Kungoja Gari Ambayo Huna Uhakika Nalo
 
Barabara Hiyo Kwa Muda Huo Aende Machame Ila Kipindi Hiki Hatakosa Ila Lazima Awe Mvumilivu Kungoja Gari Ambayo Huna Uhakika Nalo
Shukran chief,,,wadau wengi walishauri aende hapo machame sijui ndo penye stand/kituo chao alafu asikilizie
 
Basi za mwisho n saa 9-10 tena za mbeya na hapo itakuja ikiwa imejaa hatari.

Aende pale Machame kwa msimu huu Kuna Costa Ila muda wa saa 1-3 usiku ategemee kupata Private na wengi wanaotoka muda huo huishia Arusha hvyo Kama kwao n Moshi ndan ndan itamlazimu aweke kambi Arusha au aunge akalale Moshi mjin.

Akikosa Gari ya moja kwa moja Arusha/Moshi basi anaweza panda Gari inayoishia Babati zipo zile Basi za Dar to Babati, uzuri wa Babati Costa n nyingi pia Kuna zile Basi za bukoba na kigoma zinapita Babati saa sita usiku Ila ategemee kusimama mpaka Arusha sababu huwa zinajaa sana zikitoka Singida na hzo Gari huwa haziachi mtu wao wanaangalia pesa tuu.

Akifika Arusha/Moshi usiku sana mwambie anitafute nimueleke sehemu salama kwake akapumzike
 
Shukran chief,,,wadau wengi walishauri aende hapo machame sijui ndo penye stand/kituo chao alafu asikilizie
Hapo Buses Za Machame NA ABC Wana Ofisi Zao Kukata Tickets Na Kupanda/Kushuka.
Buses Za Kutoka Songea Superfeo, Mbeya, Iringa Dar Es Salaam Kwenda/Kutoka

LAZIMA Yapite Hapo Kuna Nafasi Kubwa Kupata Usafiri
 
Basi za mwisho n saa 9-10 tena za mbeya na hapo itakuja ikiwa imejaa hatari.

Aende pale Machame kwa msimu huu Kuna Costa Ila muda wa saa 1-3 usiku ategemee kupata Private na wengi wanaotoka muda huo huishia Arusha hvyo Kama kwao n Moshi ndan ndan itamlazimu aweke kambi Arusha au aunge akalale Moshi mjin.

Akikosa Gari ya moja kwa moja Arusha/Moshi basi anaweza panda Gari inayoishia Babati zipo zile Basi za Dar to Babati, uzuri wa Babati Costa n nyingi pia Kuna zile Basi za bukoba na kigoma zinapita Babati saa sita usiku Ila ategemee kusimama mpaka Arusha sababu huwa zinajaa sana zikitoka Singida na hzo Gari huwa haziachi mtu wao wanaangalia pesa tuu.

Akifika Arusha/Moshi usiku sana mwambie anitafute nimueleke sehemu salama kwake akapumzike
Shukrani kwa maelekezo mujarabu chief !!! NB hizo costa kwa msimu huu wa sikukuu zinapatikana muda gani pengine kuanzia saa 12 hivi mpk saa 3 usiku ?
 
Hapo Buses Za Machame NA ABC Wana Ofisi Zao Kukata Tickets Na Kupanda/Kushuka.
Buses Za Kutoka Songea Superfeo, Mbeya, Iringa Dar Es Salaam Kwenda/Kutoka

LAZIMA Yapite Hapo Kuna Nafasi Kubwa Kupata Usafiri
POA mkuu
 
Shukrani kwa maelekezo mujarabu chief !!! NB hizo costa kwa msimu huu wa sikukuu zinapatikana muda gani pengine kuanzia saa 12 hivi mpk saa 3 usiku ?
Uzuri Costa zinapaki karibu na Machame pale round about pia Costa ikijaa ndio inang'oa hvyo huenda mpaka muda huo zitakuwepo Jambo jema asichague Gari ya kupanda muhimu aangalie Hilo Gari linausalama kwa maana ya watu waliomo humo na mizigo waliopakia hii naongelea kwenye private car ambazo zitakuwa n nyingi na uhakika kuliko Costa ambazo Kuna zenye kibali na ambazo hazina kibali.

Mwisho wa siku hapa atakuwa amepata mwanga mkubwa sana mwisho n yeye Leo aende pale Machame akasome ramani tena aende muda ileile anayota kusafiri ili ajipange aone kama itawezekana
 
Uzuri Costa zinapaki karibu na Machame pale round about pia Costa ikijaa ndio inang'oa hvyo huenda mpaka muda huo zitakuwepo Jambo jema asichague Gari ya kupanda muhimu aangalie Hilo Gari linausalama kwa maana ya watu waliomo humo na mizigo waliopakia hii naongelea kwenye private car ambazo zitakuwa n nyingi na uhakika kuliko Costa ambazo Kuna zenye kibali na ambazo hazina kibali.

Mwisho wa siku hapa atakuwa amepata mwanga mkubwa sana mwisho n yeye Leo aende pale Machame akasome ramani tena aende muda ileile anayota kusafiri ili ajipange aone kama itawezekana
Powa ngoja nimwambie Leo akasome some mazingira aone
 
Back
Top Bottom