Usafi wa vyoo taasisi za umma Dar

Usafi wa vyoo taasisi za umma Dar

suala la usafi wa vyoo ni kwa watanzania wote, hasa vyuo vikuu nakumbuka pale UDSM Hall 7 watu walikuwa wanajisaidia chooni kwa kusimama juu ya sinki huku ametandika gazeti MZALENDO ama DAILY NEWS (Ukubwa wake unatosha kupokea kinye.si hata kiwe kingi vipi.
Wasomi wetu hii imekaaje?
 
Labda hawaflashi sababu hakuna maji. Au makusudi?
Hebu nikupe mfano; ikiwa unasafiri Dar - Moshi, kuna hoteli pale Kati ya Korogwe na Mombo ipo upande wa kulia. Mabasi yana mwaga abiria kwa wingi sana pale kujisaidia lakini hukuti choo kichafu.

Vyoo vyake ni visafi sana hakuna hata harufu. Nadhani ni kwa sababu maji yanakuwepo wakati wote. Maji ya bomba ni muhimu sana vyooni hasa vyoo vya watu wengi.
Karibu Machinga Complex ujionee vyoo vya kisasa. Hivi stendi za mwendokasi vyoo vipo upande gani?
 
Kiukweli Watanzania kwa ujumla suala la choo ni kitu cha mwisho kabisa katika UJENZI, hata USAFI, hapa naorodhesha taasisi 6 za umma zenye angalau vyoo bora & safi katika jiji la Dar es Salaam.

1. Hospitali MWANANYAMALA
2. Hospitali AMANA
3. RITA Makao Makuu
4. IMMIGRATION HQ Kurasini
5. MACHINGA COMPLEX
6. Uwanja wa Ndege -JNIA
Ukitaka kuchoka nenda kwenye vyuo vya umma utafikiri vyoo vya garage
 
suala la usafi wa vyoo ni kwa watanzania wote, hasa vyuo vikuu nakumbuka pale UDSM Hall 7 watu walikuwa wanajisaidia chooni kwa kusimama juu ya sinki huku ametandika gazeti MZALENDO ama DAILY NEWS (Ukubwa wake unatosha kupokea kinye.si hata kiwe kingi vipi.
Aisee. Mbona unajiumbua Mzee wa jalalani
 
tufike sehemu tuwe na usafi wa vyoo kama tunavopigilia pamba harusini na umaridadi wa kucheza KWAITO.
Kuna siku nilienda hospital ya mkuranga kubeba mwili wa ndugu yangu aliefariki, nakashikwa na haja, nilipoenda chooni, hali niliyokutana nayo, ilinilazimu nikodi pikipiki inipeleke kwenye vyoo vya kulipia.

Lakini shida haikuishia chooni tu, kwenye chumba cha kuhifadhia maiti, nilikuta sisimizi wanaingia kwenye mwili wa marehemu.

Kwakua ulikua umelazwa chini tu, shida hapa siyo mwili kulazwa chini, sehemu kama ile kuna takiwa kuwa na dawa ya kudekia, ambayo huuwa wadudu, na hairuhusu wadudu wanaotambaa.
 
Hapo kwenye hospital ya Mwananyamala, mkuu unaongopea umma! Nakushangaa hujaiweka hospital ya Lugalo!
Lugalo wanaweza kuwa Vyoo visafi, ila sidhani kama mtoa mada, avijua vyoo vyote vya hospital za uma, hivyo inawezekana huko hajafika.
 
Back
Top Bottom