Ustaarabu kwa sisi dunia ya tatu ni changamoto kubwa sana, kumbuka aliyechafua ni abiria mwenzako aliyetangulia kutumia chombo hicho cha usafiri,Abiria wenyewe sio wastaarabu unakuta mtu anakula ndizi ganda anatupa ndani ya gari, anakula karanga, mahindi magunzi anaacha ndani ya gari. Mfano haya mabasi yanayoenda mikoa mbalimbali ndio balaa unakuta yanapoanza safari ni masafi na siku hizi wanaweka mpaka disturb lakini ikifika mchana angalia chini ya viti utakuta kila aina ya uchafu kuanzia chupa tupu za soda, biscuit,pipi, mifuko ya kuhifadhia chakula na n.k na wengine wanatupa tu dirishani, inabidi muanze kuwapa elimu watu mnaoishi nao hili ni janga