Usafi jiji la kimataifa la Arusha

Otorong'ong'o

JF-Expert Member
Aug 17, 2011
37,526
25,734
Wana Bodi,

Napenda kuchukua nafasi hii kuipongeza kwa dhati kabisa Halamashauri ya Jiji la Arusha kwa kuuboresha mji huu...

WACHUUZI NA WAMACHINGA
Hakika kwa mtu yeyote mgeni akifika leo Arusha atastaajabu kwa usafi wa Jiji hili la Kimataifa na kitalii Barani Afrika..
Sikuwahi kuamini kwamba ipo siku wale wafanya biashara wadowadogo sana sana kina mama waliokuwa wanapanga bidhaa zao chini mf. nyanya, parachichi, ndizi mbivu kuku wabichi n.k, kwamba kuna siku watakuja kutoka katikati ya Jiji.

Ila kwasasa hakuna hata mchuuzi mmoja unaweza ukamuona katikati ya mji....Hapa naomba kutoa pongezi za dhati kabisa.
Maduka ya bishara nayo yanaudhabidhaa zao ndani ya duka bila kutoa baadhi ya bidhaa zao nje ya maduka...

PARKING
Kwasasa bara bara za arusha zina pitika kwa raha mustarehe kabisa. Magari yamepaki kwa utaratibu maalu(I love this)....Kuna space ya kutosha, bara bara unaiona mwanzo mpaka mwisho kabisa....nazo boda boda zinapaki kwa ustaarabu wa ajabu kabisa....Pia napenda kutoa pongezi zangu za dhati katika hili...

USAFI WA BARABARA
Hakika bara za jiji la Arusha hususani maeneo ya katikati ya mji ni safi mno....isipokuwa maeneo machache ambayo yanauchafu, mchanga na tope lilikwama pembezoni mwa bara bara.....Natoa pongezi pia katika hili..

OMBI KWA MANISPAA
Naomba usafi huu uendelee hivi hivi isije ikawa ni nguvu ya soda.....Pia naomba Manispaa iwe makini sana maana nimeshaanza kuona baadhi ya kina mama na wamachinga wanarejeakatikati ya mji hasa wakati wa jioni kuanzia saa 4.00pm..(Saa kumi jioni)....Hasa maeneo ya France corner na kilombero...Naomba Manispaa ifuatilie swala hili...

Yote kwa yote mji wa Arusha kwa sasa ni msafi....Hakika kwa staili hii tunaweza ipiku Manispaa ya Moshi kwa usafi;
Karibu Arusha, Karibu mji wa kitalii, karibu Geneva of Afrika.
 
Lazima ufurahi wanyonge kuendelea kukandamizwa kwenye nchi yao na wenye madaraka!!

Sidhani kama ungekuwa na mzazi, ndugu au jamaa yako anayejihusisha na hii shughuli ungefurahia jambo hili!!
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Lazima hii spidi iendelee tuweza kuufanya mji wetu kuwa msafi. Hongera kwa jiji..
 
Mikokoteni haitakiwi kuonekana mjini mwisho Sakina,Ngulelo,Kijenge,Njiro relini.......hah ha ha ha ha ha ha.
 
mtoa mada ebu uje utembelee barabara ya kwenda Ilboru kupitia Mianzini au pale karibu kwa molel uangalie kama lami imewekwa make kipindi bado napiga umande tuliaidiwa na politician moja kua atafanya hivo.
 
mtoa mada ebu uje utembelee barabara ya kwenda Ilboru kupitia Mianzini au pale karibu kwa molel uangalie kama lami imewekwa make kipindi bado napiga umande tuliaidiwa na politician moja kua atafanya hivo.

Mada haijaongelea uwekwaji wa lami bali 'Usafi wa Jiji la Arusha'
 
Mikokoteni haitakiwi kuonekana mjini mwisho Sakina,Ngulelo,Kijenge,Njiro relini.......hah ha ha ha ha ha ha.

Central Busness District..(CBD)

Japokuwa hata hayo maeneo ambayo mikokoteni ni mwisho bado yapo karibu na mji..
 
Wanasema mkokoteni mwisho ngaramtoni,ngulelo.. mjini wanataka zile pikipiki za matairi matatu. Walikuja huku mtaani kwetu wakasema hvyo.
 
Lazima ufurahi wanyonge kuendelea kukandamizwa kwenye nchi yao na wenye madaraka!!

Sidhani kama ungekuwa na mzazi, ndugu au jamaa yako anayejihusisha na hii shughuli ungefurahia jambo hili!!

Hakika kama ningekuwa nina ndugu wala nisingeona shida, tena ningefurahi sana...

Huwezi mtu ukatoka huko utokako na karai la ndizi mbivu au matunda halafu unakuja katikati ya mji unauza....Mbaya zaidi wanafanya uchafuzi mkubwa katikati ya mji.....

Hili zoezi natamani liendelee daima..
 
Kweli viongozi husika wanastahili pongezi.Wajaribu kuangalia soko la kilombero wapaangalie kwa umakini.Kuna mfereji wa maji machafu wenye harufu mbaya kuelekea sambamba na barabara na shoping centre.Inakera sana hata wageni (watalii)wakifika maeneo hayo hupata tabu ya harufu kali.Pia wafanya biashara wadogo wadogo bado wapo maeneo hayo.Kazeni buti Jitihada zenu zimeonekana.
 
Kweli viongozi husika wanastahili pongezi.Wajaribu kuangalia soko la kilombero wapaangalie kwa umakini.Kuna mfereji wa maji machafu wenye harufu mbaya kuelekea sambamba na barabara na shoping centre.Inakera sana hata wageni (watalii)wakifika maeneo hayo hupata tabu ya harufu kali.Pia wafanya biashara wadogo wadogo bado wapo maeneo hayo.Kazeni buti Jitihada zenu zimeonekana.

Ni kweli kabisa...Pale Kilombero panatia kinya....Na wale wafanyabiashara wanarudi kwa kasi ya ajabu.....

Halmashauri inatakiwa kuliangalia hili kwa makini.......
 
the city clean n' the roads are clearly visible in short pako gud sn, kazi kwetu kumaintain.
 
Oyoh!,, ma city, ma town, ipo juu kwa kweli karbia tutawapita Moshi! Hongera mkurugenz wa jiji!
 
Back
Top Bottom