Urusi: Tumechoshwa na madai ya Marekani

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,950
_93327555_gettyimages-630537660.jpg


Ripoti ya mashirika ya kijasusi
ya Marekani ilisema kuwa Putin aliamrisha kufanyika kwa udukuzi,
Urusi inasema kuwa madai kuwa Urusi iliendesha kampeni ya udukuzi wa mitandao ili kushawishi uchaguzi wa urais nchini Marekani si kweli.

Msemaji wa serikali ya Urusi Dmitry Peskov aliwaambia waandishi wa habari kuwa Urusi imechoshwa na madai hayo.

Alisema kuwa ripoti iliyotolewa na mashirika ya ujasusi nchini Marekani kuhudu madai hayo haina msingi wowote.

Hayo ndiyo matamshi ya kwanza kutoka Urusi tangu rais mteule Donald Trump akabidhiwe ripoti hiyo.

Trump amekuwa akipinga madai ya udukuzi wa Urusi tangu ashinde uchaguzi wa urais mwezi Novemba.
 
Back
Top Bottom