Urusi kujenga mji mwezini ifikapo 2040

Urusi kujenga mji mwezini ifikapo 2040

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
11,129
Reaction score
24,429
Russia kujenga mji mwezini ifikapo 2040
Russia imetangaza kuwa imenuia kujenga mji mwezini ifikapo mwaka 2040, katika mradi ambao utafanyika kwa awamu tatu.
Kwa mujibu wa televisheni ya al Alam, ratiba ya huko nyuma ya Shirika la Anga za Juu la Russia iliyotangazwa mwaka 2014 ilisema kuwa, shirika hilo lina mpango wa kutuma mwanadamu mwezini ili kuandaa mazingira ya kuwekwa jiwe la msingi la kujenga mji katika usawa wa mwezi.
Mamia ya wataalamu wa anga za juu wa Russia wamewasilisha maombi yao ya kutaka kuteuliwa kuwa watu wa kwanza kwenda kufanikiza kazi hiyo.
Hata hivyo na baada ya kuitisha kikao maalumu, shirika hilo la anga za juu la Russia limetangaza kuwa, kazi ya kujenga mji huo wa kwanza mwezini itafanyika kwa awamu tatu na kukamilika mwaka 2040.
Katika awamu ya kwanza itatumwa 'module' maalumu kuzunguka mwezi. Awamu ya pili itakuwa ni ya operesheni maalumu ya kupeleka watu mwezini na pia kujenga kituo cha kudumu juu ya mwezi baina ya mwaka 2025 hadi 2040.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, awamu ya tatu ya ujenzi wa mji huo itamalizika mwaka 2040. Kwa mujibu wa Shirika la Anga za Juu la Russia, hati za mwisho za operesheni hiyo ya mwezini zitakamilika mwishoni mwa mwezi Februari 2019.
 
Russia kaacha mbali kwenye anga za juu, America anaelekea kuishi kwenye Mars half wana MISSION TO THE SUN. wanataka kusongelea jua kwa karibu sana. Maandalizi ya hii Mission yameanza
 
Walishindwa kupata dawa ya ujana WA milele wakati wa Dictator Stalin Ha Ha Ha!
 
Wamechelewa Sana Warusi,

Bora wangewekeza kwenye Mars,

Mwezi siku zijazo kuna uwezekano wa kuja kuigonga dunia na sehemu Fulani ya dunia kuangamia,

Mars ni sayari kubwa mfano wa dunia,

Ni bora kupeleka uhai kwenye Mars na sio kupoteza pesa nyingi kwenye hamna uhai mwezini
 
Aisee! Wenzetu wanatumia hela nyingi kuwekeza huko mwengine(US safari ya Mars,Urusi Mwezini) ni nini agenda yao,au wanataka kuilipua dunia na hiyo mibomu yao ya nyuklia na kukimbilia huko!
Nalog off
unaona mbele sana aisee, yani siku ikisikika vita ya dunia wenzetu tayari wamesha andaa mji wao mpya,Kazi kwetu kwa sisi Waafrika, Mwenyez Mungu atatulinda tu
 
Do u think hayo hawayajui?
Wamechelewa Sana Warusi,

Bora wangewekeza kwenye Mars,

Mwezi siku zijazo kuna uwezekano wa kuja kuigonga dunia na sehemu Fulani ya dunia kuangamia,

Mars ni sayari kubwa mfano wa dunia,

Ni bora kupeleka uhai kwenye Mars na sio kupoteza pesa nyingi kwenye hamna uhai mwezini
 
Russia kujenga mji mwezini ifikapo 2040
Russia imetangaza kuwa imenuia kujenga mji mwezini ifikapo mwaka 2040, katika mradi ambao utafanyika kwa awamu tatu.
Kwa mujibu wa televisheni ya al Alam, ratiba ya huko nyuma ya Shirika la Anga za Juu la Russia iliyotangazwa mwaka 2014 ilisema kuwa, shirika hilo lina mpango wa kutuma mwanadamu mwezini ili kuandaa mazingira ya kuwekwa jiwe la msingi la kujenga mji katika usawa wa mwezi.
Mamia ya wataalamu wa anga za juu wa Russia wamewasilisha maombi yao ya kutaka kuteuliwa kuwa watu wa kwanza kwenda kufanikiza kazi hiyo.
Hata hivyo na baada ya kuitisha kikao maalumu, shirika hilo la anga za juu la Russia limetangaza kuwa, kazi ya kujenga mji huo wa kwanza mwezini itafanyika kwa awamu tatu na kukamilika mwaka 2040.
Katika awamu ya kwanza itatumwa 'module' maalumu kuzunguka mwezi. Awamu ya pili itakuwa ni ya operesheni maalumu ya kupeleka watu mwezini na pia kujenga kituo cha kudumu juu ya mwezi baina ya mwaka 2025 hadi 2040.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, awamu ya tatu ya ujenzi wa mji huo itamalizika mwaka 2040. Kwa mujibu wa Shirika la Anga za Juu la Russia, hati za mwisho za operesheni hiyo ya mwezini zitakamilika mwishoni mwa mwezi Februari 2019.
Television ya All alam? Iko mji gani hiyo TV?
 
Back
Top Bottom