wiseboy.
JF-Expert Member
- Aug 11, 2014
- 2,931
- 4,550
Hili jambo ni zito na linahitaji hekima sana kulijua, wengi wetu tumejikuta tunamchukia Sana Rais Magufuli kwa sababu ya mwenendo wa hali ya kisiasa na kiuchumi ndani ya taifa letu.
Nimekaa chini na kutafakari kwa kina sana baada ya kuwa nimemjadili kwa kina Rais Magufuli (mjadala wangu binafsi) na nikaibuka na jibu moja tu kwamba, Magufuli ana nia nzuri mno na Tanzania lakini watu waliomzunguka ni tatizo kubwa mno, (japokuwa na yeye ana matatizo yake binafsi).
Nimepata jibu hilo baada ya kuwa nimesoma kwa kina na kujua kazi za Urais na utendaji wake wote kwa ujumla.
Rais Magufuli amezungukwa na wachumia tumbo tupu, hawa kazi yao kubwa ni kumlaghai na kumtapeli Rais.
Kwa hiyo wanaichukulia tabia yake ya ukali kama point ya kutomshauri au kumweleza ukweli wa mambo ulivyo.
Fikiria Waziri mzima wa Fedha anapojigamba mbele ya media kuwa uchumi umekua, wakati mzunguko wa pesa mitaani umekata kabisa na pesa haina thamani hata kidogo.
Fikiria baraza la mawaziri kumwacha Rais asaini kufukuza kazi watu zaidi ya elfu kumi, bila ya waziri yoyote yule kumshauri Rais juu ya athari za kiuchumi na maisha ya familia zitakazo adhirika kwa wazazi kukosa ajira .
Fikiria baraza la mawaziri kumwacha Rais bila kumshauri azuie mikutano ya kisiasa na shughuli zote za kisiasa wakati katiba inaruhusu.
Kumwacha Rais bila kumshauri anunue ndege kwa pesa Cash wakati hata serikali ya Marekani yenyewe huwa inanunua silaha za kivita Kama ndege jeshi kutoka kampuni ya kimarekani ya "LOCKHEED MARTIN " kwa instalment, ije kuwa taifa maskini Kama letu?
Mambo ni mengi tu, kuyaeleza yote tutahitaji kitabu.
Mtu anapokuwa kiongozi mkuu wa nchi, kundi la watu waovu humzunguka ili kupata maslahi yao,wengine huwa ni under cover spies wa mataifa ya nje yenye chuki au kuhujumu taifa husika.
Kama kweli waliomzunguka Rais ni wazalendo wa kweli, wanaogopa nini kumshauri na kumwambia ukweli tu hata Kama atawafukuza kazi?
Kuogopa kufukuzwa kazi kwa maslahi ya taifa huo ni uchumia tumbo.
Mawaziri wote zaidi ya 50 kweli wangejitosa hata 15 tu na kumweleza ukweli Rais pengine hali ya kiuchumi isingekuwa ngumu hivi.
Kama hofu ni kwamba atawafukuza, unadhani atawafukuza wote, hata Kama ni wote, itafika wakati atakosa wa kufanya naye kazi na kujikuta anaanza kupokea ushauri.
Ndo maana nikasema Urais ni taasisi kwa maana ya kwamba ,Rais kuna sehemu nyingi tu anahitaji msaada wa mawazo kutoka kwa wenzake.
Nakumbuka ripot ya makinikia iliyokuwa ikirushwa live na TV, Rais aliwaomba Makamu wake na waziri mkuu aende nao pembeni wajadili jambo.
Humu JF kumejaa matapeli ya CCM kazi yao kubwa ni kumsifia Rais hata Kama kuna matatizo sehemu, hayo ndo matapeli kabisa, shida yao ni kupata shibe tu basi.
Bungeni ndo hovyo kabisa, kazi yao ni kupiga meza na kuunga mkono hoja, kwa hali hiyo Rais atawezaje ku Perform wakati kila jambo yeye anasifiwa tu,hata Kama ana hulka ya kupenda sifa, waliomzunguka wakionyesha kutokubaliana naye ni lazima atabadilika.
Rais kazungukwa na genge la matapeli.
Nimekaa chini na kutafakari kwa kina sana baada ya kuwa nimemjadili kwa kina Rais Magufuli (mjadala wangu binafsi) na nikaibuka na jibu moja tu kwamba, Magufuli ana nia nzuri mno na Tanzania lakini watu waliomzunguka ni tatizo kubwa mno, (japokuwa na yeye ana matatizo yake binafsi).
Nimepata jibu hilo baada ya kuwa nimesoma kwa kina na kujua kazi za Urais na utendaji wake wote kwa ujumla.
Rais Magufuli amezungukwa na wachumia tumbo tupu, hawa kazi yao kubwa ni kumlaghai na kumtapeli Rais.
Kwa hiyo wanaichukulia tabia yake ya ukali kama point ya kutomshauri au kumweleza ukweli wa mambo ulivyo.
Fikiria Waziri mzima wa Fedha anapojigamba mbele ya media kuwa uchumi umekua, wakati mzunguko wa pesa mitaani umekata kabisa na pesa haina thamani hata kidogo.
Fikiria baraza la mawaziri kumwacha Rais asaini kufukuza kazi watu zaidi ya elfu kumi, bila ya waziri yoyote yule kumshauri Rais juu ya athari za kiuchumi na maisha ya familia zitakazo adhirika kwa wazazi kukosa ajira .
Fikiria baraza la mawaziri kumwacha Rais bila kumshauri azuie mikutano ya kisiasa na shughuli zote za kisiasa wakati katiba inaruhusu.
Kumwacha Rais bila kumshauri anunue ndege kwa pesa Cash wakati hata serikali ya Marekani yenyewe huwa inanunua silaha za kivita Kama ndege jeshi kutoka kampuni ya kimarekani ya "LOCKHEED MARTIN " kwa instalment, ije kuwa taifa maskini Kama letu?
Mambo ni mengi tu, kuyaeleza yote tutahitaji kitabu.
Mtu anapokuwa kiongozi mkuu wa nchi, kundi la watu waovu humzunguka ili kupata maslahi yao,wengine huwa ni under cover spies wa mataifa ya nje yenye chuki au kuhujumu taifa husika.
Kama kweli waliomzunguka Rais ni wazalendo wa kweli, wanaogopa nini kumshauri na kumwambia ukweli tu hata Kama atawafukuza kazi?
Kuogopa kufukuzwa kazi kwa maslahi ya taifa huo ni uchumia tumbo.
Mawaziri wote zaidi ya 50 kweli wangejitosa hata 15 tu na kumweleza ukweli Rais pengine hali ya kiuchumi isingekuwa ngumu hivi.
Kama hofu ni kwamba atawafukuza, unadhani atawafukuza wote, hata Kama ni wote, itafika wakati atakosa wa kufanya naye kazi na kujikuta anaanza kupokea ushauri.
Ndo maana nikasema Urais ni taasisi kwa maana ya kwamba ,Rais kuna sehemu nyingi tu anahitaji msaada wa mawazo kutoka kwa wenzake.
Nakumbuka ripot ya makinikia iliyokuwa ikirushwa live na TV, Rais aliwaomba Makamu wake na waziri mkuu aende nao pembeni wajadili jambo.
Humu JF kumejaa matapeli ya CCM kazi yao kubwa ni kumsifia Rais hata Kama kuna matatizo sehemu, hayo ndo matapeli kabisa, shida yao ni kupata shibe tu basi.
Bungeni ndo hovyo kabisa, kazi yao ni kupiga meza na kuunga mkono hoja, kwa hali hiyo Rais atawezaje ku Perform wakati kila jambo yeye anasifiwa tu,hata Kama ana hulka ya kupenda sifa, waliomzunguka wakionyesha kutokubaliana naye ni lazima atabadilika.
Rais kazungukwa na genge la matapeli.