Je Mimi Ni mraibu
Hili linaweza lisiwe jambo rahisi kufanya. Katika kipindi chetu chote cha utumiaji, tulijiambia, “naweza kuhimili.” Hata kama hili lilikuwa kweli mwanzoni, sio hivyo sasa.
Mihadharati ilitutawala sisi. Tuliishi kutumia na tulitumia ili tuishi. Kwa ufupi, mraibu ni mtu ambaye maisha yake yanatawaliwa na
dawa za kulevya.
Labda unakiri kuwa na tatizo la dawa za kulevya, lakini wewe mwenyewe hujichukulii kama mraibu. Sisi wote tuna mtazamo tofauti kuhusu mraibu ni nani. Hakuna aibu katika kuwa mraibu mara unapoanza kuchukua hatua sahihi. Kama unaweza kujitambua na tatizo letu, labda unaweza kujitambua na suluhisho letu.
Maswali yafuatayo
yaliandikwa na waraibu wanaopata nafuu. Kama una shaka kuwa wewe ni mraibu au hapana, chukua dakika kadhaa kusoma maswali
yafuatayo na kuyajibu kwa ukweli uwezavyo.
1. Je, wewe hutumia ukiwa peke yako?
Ndio
Hapana
2. Umeshawahi kubadilisha dawa moja ya kulevya kwa nyingine, ukidhania dawa moja wapo ndio iliokuwa tatizo?
Ndio
Hapana
3. Umeshawahi kumlaghai au kumdanganya daktari ili upewe dawa?
Ndio
Hapana
4. Umeshawahi kuiba dawa za kulevya, au kufanya uhalifu ili kupata fedha za kununua mihadharati?
Ndio
Hapana
5. Je, unatumia dawa za kulevya mara kwa mara unapoamka
Ndio
Hapana
6. Umeshawahi kutumia dawa ya kulevya moja ili kudhibiti athari za dawa nyingine?
Ndio
Hapana
7. Je, unaepuka watu au sehemu ambazo zinapinga matumizi yako ya dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
8. Umeshawahi kutumia dawa ya kulevya bila kujua ni nini, au kujua itakufanya nini?
Ndio
Hapana
9. Je, uwezo wako wa kufanya kazi au masomo yako umeshawahi kuathiriwa na utumiaji wako wa dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
10. Je, umeshawahi kukamatwa kutokana
na utumiaji wa dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
11. Je, umeshawahi kudanganya kuhusu dawa unayotumia au kiasi unachotumia?
Ndio
Hapana
12. Je, unaweka ununuzi wa dawa za kulevya mbele ya majukumu mengine ya kifedha?
Ndio Hapana
13. Je, umeshawahi kujaribu kuacha au kudhibiti utumiaji wako?
Ndio
Hapana
14. Je, umeshawahi kuwekwa jela, hospitali au kituo cha marekebisho kwa sababu ya utumiaji?
Ndio
Hapana
15. Je, utumiaji huingilia usingizi wako au ulaji wako?
Ndio
Hapana
16. Je, wazo la kuishiwa na dawa za kulevya hukuogopesha?
Ndio
Hapana
17. Je, unahisi kuwa haiwezekani wewe kuishi bila kutumia dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
18. Je, wewe hujiuliza juu ya utimamu wa akili yako mwenyewe?
Ndio
Hapana
19. Je, utumiaji wako wa dawa za kulevya unafanya maisha yako nyumbani yasiwe ya furaha?
Ndio
Hapana
20 Je, umeshawahi kufikiria kutokubalika au kushindwa kuwa na raha bila dawa za kulevya? Ndio
Hapana
21. Je, umeshawahi kuhisi kujitetea, mwenye hatia, au aibu juu ya utumiaji wako?
Ndio
Hapana
22. Je, unafikiria sana juu ya dawa za kulevya? Ndio
Hapana
23. Je, umeshakuwa na uwoga bila sababu au usioeleweka?
Ndio
Hapana
24. Je, utumiaji wako umeathiri uhusiano wako wa ngono au mapenzi?
Ndio
Hapana
25. Je, umeshawahi kutumia dawa za kulevya ambazo hukuzipendelea?
Ndio
Hapana
26. Je, umeshawahi kutumia dawa za kulevya kwa sababu ya maumivu ya kihisia au msongo wa mawazo?
Ndio
Hapana
27. Je, umeshawahi kutumia dawa yoyote ukazidisha?
Ndio
Hapana
28. Je, unaendelea kutumia dawa za kulevya licha ya matokeo mabaya?
Ndio
Hapana
29. Je, unafikiri unaweza kuwa na tatizo la utumiaji wa dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
“Je, mimi ni mraibu?”
Hili ni swali ambalo ni wewe pekee unayeweza kulijibu. Sisi wote tuligundua tulijibu maswali tofauti
na jibu la “Ndio”. Namba halisi ya majibu ya “Ndio” haikuwa na umuhimu kuliko vile tulivyojihisi ndani yetu na jinsi uraibu ulivyoathiri maisha yetu.
Baadhi ya maswali haya hata hayataji mihadharati. Hii ni kwa sababu uraibu ni maradhi sugu ambayo huathiri sehemu zote za maisha yetu – hata zile sehemu ambazo mwanzoni huonekana hazina uhusiano wa karibu na dawa za kulevya.
Dawa mbalimbali za kulevya tulizotumia sio muhimu kuzidi sababu za utumiaji na madhara yake kwetu.
Tulipoyasoma haya maswali mara ya kwanza, tulishikwa na hofu na kufikiri labda sisi ni waraibu. Baadhi yetu tulijaribu kupuuza fikra hizo kwa kusema:
“Hayo maswali hayana maana”;
Au
“Mimi niko tofauti. Najua natumia
mihadharati, lakini mimi sio mraibu. Nina matatizo halisi ya kihisia/ familia/ kikazi”;
Au
“Ni kwa vile tu kwa sasa nina wakati mgumu kujipanga”;
Au
“Nitaweza kuacha pindi nitakapopata mtu
anayefaa/ kazi sahihi, n.k.”
Kama wewe ni mraibu, kwanza lazima ukubali kuwa una tatizo la mihadharati kabla maendeleo yoyote hayajafanyika kuelekea kwa upataji nafuu. Haya maswali, yanapojibiwa kwa ukweli, yanaweza kukusaidia kuona jinsi utumiaji wa dawa za kulevya umesababisha wewe kushindwa kuyamudu maisha yako. Uraibu ni maradhi ambayo, bila kupata nafuu, mwisho ni jela, taasisi, na kifo. Wengi wetu tumekuja kwenye Narcotics Anonymous kwa sababu mihadharati imeacha kufanya kazi tuliyotegemea ifanye. Uraibu huchukua ufahari wetu, hadhi yetu, familia zetu, wapendwa wetu, na hata hamu ya kuishi. Kama hujafikia hatua hii kwenye uraibu wako, sio lazima ufikie kiwango hicho. Tumegundua kuwa kuzimu kulikuwa ndani yetu sisi wenyewe.
Kama unahitaji msaada,
Tupigie
+255742550551
Hili linaweza lisiwe jambo rahisi kufanya. Katika kipindi chetu chote cha utumiaji, tulijiambia, “naweza kuhimili.” Hata kama hili lilikuwa kweli mwanzoni, sio hivyo sasa.
Mihadharati ilitutawala sisi. Tuliishi kutumia na tulitumia ili tuishi. Kwa ufupi, mraibu ni mtu ambaye maisha yake yanatawaliwa na
dawa za kulevya.
Labda unakiri kuwa na tatizo la dawa za kulevya, lakini wewe mwenyewe hujichukulii kama mraibu. Sisi wote tuna mtazamo tofauti kuhusu mraibu ni nani. Hakuna aibu katika kuwa mraibu mara unapoanza kuchukua hatua sahihi. Kama unaweza kujitambua na tatizo letu, labda unaweza kujitambua na suluhisho letu.
Maswali yafuatayo
yaliandikwa na waraibu wanaopata nafuu. Kama una shaka kuwa wewe ni mraibu au hapana, chukua dakika kadhaa kusoma maswali
yafuatayo na kuyajibu kwa ukweli uwezavyo.
1. Je, wewe hutumia ukiwa peke yako?
Ndio
Hapana
2. Umeshawahi kubadilisha dawa moja ya kulevya kwa nyingine, ukidhania dawa moja wapo ndio iliokuwa tatizo?
Ndio
Hapana
3. Umeshawahi kumlaghai au kumdanganya daktari ili upewe dawa?
Ndio
Hapana
4. Umeshawahi kuiba dawa za kulevya, au kufanya uhalifu ili kupata fedha za kununua mihadharati?
Ndio
Hapana
5. Je, unatumia dawa za kulevya mara kwa mara unapoamka
Ndio
Hapana
6. Umeshawahi kutumia dawa ya kulevya moja ili kudhibiti athari za dawa nyingine?
Ndio
Hapana
7. Je, unaepuka watu au sehemu ambazo zinapinga matumizi yako ya dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
8. Umeshawahi kutumia dawa ya kulevya bila kujua ni nini, au kujua itakufanya nini?
Ndio
Hapana
9. Je, uwezo wako wa kufanya kazi au masomo yako umeshawahi kuathiriwa na utumiaji wako wa dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
10. Je, umeshawahi kukamatwa kutokana
na utumiaji wa dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
11. Je, umeshawahi kudanganya kuhusu dawa unayotumia au kiasi unachotumia?
Ndio
Hapana
12. Je, unaweka ununuzi wa dawa za kulevya mbele ya majukumu mengine ya kifedha?
Ndio Hapana
13. Je, umeshawahi kujaribu kuacha au kudhibiti utumiaji wako?
Ndio
Hapana
14. Je, umeshawahi kuwekwa jela, hospitali au kituo cha marekebisho kwa sababu ya utumiaji?
Ndio
Hapana
15. Je, utumiaji huingilia usingizi wako au ulaji wako?
Ndio
Hapana
16. Je, wazo la kuishiwa na dawa za kulevya hukuogopesha?
Ndio
Hapana
17. Je, unahisi kuwa haiwezekani wewe kuishi bila kutumia dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
18. Je, wewe hujiuliza juu ya utimamu wa akili yako mwenyewe?
Ndio
Hapana
19. Je, utumiaji wako wa dawa za kulevya unafanya maisha yako nyumbani yasiwe ya furaha?
Ndio
Hapana
20 Je, umeshawahi kufikiria kutokubalika au kushindwa kuwa na raha bila dawa za kulevya? Ndio
Hapana
21. Je, umeshawahi kuhisi kujitetea, mwenye hatia, au aibu juu ya utumiaji wako?
Ndio
Hapana
22. Je, unafikiria sana juu ya dawa za kulevya? Ndio
Hapana
23. Je, umeshakuwa na uwoga bila sababu au usioeleweka?
Ndio
Hapana
24. Je, utumiaji wako umeathiri uhusiano wako wa ngono au mapenzi?
Ndio
Hapana
25. Je, umeshawahi kutumia dawa za kulevya ambazo hukuzipendelea?
Ndio
Hapana
26. Je, umeshawahi kutumia dawa za kulevya kwa sababu ya maumivu ya kihisia au msongo wa mawazo?
Ndio
Hapana
27. Je, umeshawahi kutumia dawa yoyote ukazidisha?
Ndio
Hapana
28. Je, unaendelea kutumia dawa za kulevya licha ya matokeo mabaya?
Ndio
Hapana
29. Je, unafikiri unaweza kuwa na tatizo la utumiaji wa dawa za kulevya?
Ndio
Hapana
“Je, mimi ni mraibu?”
Hili ni swali ambalo ni wewe pekee unayeweza kulijibu. Sisi wote tuligundua tulijibu maswali tofauti
na jibu la “Ndio”. Namba halisi ya majibu ya “Ndio” haikuwa na umuhimu kuliko vile tulivyojihisi ndani yetu na jinsi uraibu ulivyoathiri maisha yetu.
Baadhi ya maswali haya hata hayataji mihadharati. Hii ni kwa sababu uraibu ni maradhi sugu ambayo huathiri sehemu zote za maisha yetu – hata zile sehemu ambazo mwanzoni huonekana hazina uhusiano wa karibu na dawa za kulevya.
Dawa mbalimbali za kulevya tulizotumia sio muhimu kuzidi sababu za utumiaji na madhara yake kwetu.
Tulipoyasoma haya maswali mara ya kwanza, tulishikwa na hofu na kufikiri labda sisi ni waraibu. Baadhi yetu tulijaribu kupuuza fikra hizo kwa kusema:
“Hayo maswali hayana maana”;
Au
“Mimi niko tofauti. Najua natumia
mihadharati, lakini mimi sio mraibu. Nina matatizo halisi ya kihisia/ familia/ kikazi”;
Au
“Ni kwa vile tu kwa sasa nina wakati mgumu kujipanga”;
Au
“Nitaweza kuacha pindi nitakapopata mtu
anayefaa/ kazi sahihi, n.k.”
Kama wewe ni mraibu, kwanza lazima ukubali kuwa una tatizo la mihadharati kabla maendeleo yoyote hayajafanyika kuelekea kwa upataji nafuu. Haya maswali, yanapojibiwa kwa ukweli, yanaweza kukusaidia kuona jinsi utumiaji wa dawa za kulevya umesababisha wewe kushindwa kuyamudu maisha yako. Uraibu ni maradhi ambayo, bila kupata nafuu, mwisho ni jela, taasisi, na kifo. Wengi wetu tumekuja kwenye Narcotics Anonymous kwa sababu mihadharati imeacha kufanya kazi tuliyotegemea ifanye. Uraibu huchukua ufahari wetu, hadhi yetu, familia zetu, wapendwa wetu, na hata hamu ya kuishi. Kama hujafikia hatua hii kwenye uraibu wako, sio lazima ufikie kiwango hicho. Tumegundua kuwa kuzimu kulikuwa ndani yetu sisi wenyewe.
Kama unahitaji msaada,
Tupigie
+255742550551