Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,421
- 40,409
Kuna dada mmoja nilisoma naye darasa moja miaka mingi iliyopita, tulikuwa hatuna mahusiano yoyote...zaidi ya hisia zake na zangu kuwa zinawasiliana tu. Wiki tatu hivi zilizopita, nilipokea simu kutoka kwake tukasalimiana na kujuliana hali, pamoja na kuniambia jitihada alizotumia kupata namba yangu. Yeye alishaolewa na anafamilia yake zaidi ya miaka 10. Ilitokea wamehama hama kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine kutokana na mazingira ya kazi. Ndani ya wiki tatu hizi tumewasiliana sana, naye anatumia nguvu nyingi sana kunipigia simu, kutuma sms n.k
Juzi, ndipo akaamua kuniambia changamoto alizonazo kwenye ndoa; mumewe amebadilika, akirudi nyumbani anamjibu kwa ukali, hakuna masikilizano, matumizi hatoi, mzee anawajali watoto tu, amekuwa hana thamani ndani ya nyumba zaidi ya kuonekana kama beki 3.
Nilijaribu kumpa ushauri wa hapa na pale, lakini naona uelekeo wake naye anatafuta pa kupunguzia msongo wa mawazo. Najaribu kufikiria huu ukaribu huu unaojisogeza, unaweza kusababisha kula tunda kimasihara, lakini hofu yangu nisije kuwa kikwazo kwenye familia yake au yangu. Na nikikata mawasiliano naye pale anaponipigia nahisi nitakuwa sijamtendea haki.
Wakuu mnanishauriji kwenye hili jambo?
Juzi, ndipo akaamua kuniambia changamoto alizonazo kwenye ndoa; mumewe amebadilika, akirudi nyumbani anamjibu kwa ukali, hakuna masikilizano, matumizi hatoi, mzee anawajali watoto tu, amekuwa hana thamani ndani ya nyumba zaidi ya kuonekana kama beki 3.
Nilijaribu kumpa ushauri wa hapa na pale, lakini naona uelekeo wake naye anatafuta pa kupunguzia msongo wa mawazo. Najaribu kufikiria huu ukaribu huu unaojisogeza, unaweza kusababisha kula tunda kimasihara, lakini hofu yangu nisije kuwa kikwazo kwenye familia yake au yangu. Na nikikata mawasiliano naye pale anaponipigia nahisi nitakuwa sijamtendea haki.
Wakuu mnanishauriji kwenye hili jambo?