voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,884
Mtadanganyana na kudanganyika wenyewe kwa wenyewe!
Jiulizeni Mkurugenzi TISS kupelekwa Ikulu, kwa mfumo ule ule wa Lukuvi na Kabudi! Hamjifunzi jambo hapo tu? Pale wanaenda kuwekwa kwenye ulinzi wa karibu zaidi.
Na bado mengi yanafuatia!
Eti maridhiano!
Kwamba mmeridhiana Samia akiondoka atawaachia na nyinyi zamu yenu au?
Ukweli ni kwamba hali ndani ya CCM sio nzuri tangu Makamba Senior alipotoa zile kauli zake kwenye NEC Dodoma.
Imeleta mtarafuku mkubwa na ulianzia pale pale Dodoma.
Pamoja na Mwenyekiti wa CCM kuwaita wajumbe na kujaribu kuwatuliza.
Kwenye kikao kingine cha dharura jioni ile ile. Wajumbe wengi walikereka sana na kauli za Makamba!
Kwamba..." ilifika mahali wazee tukasema Hapana"
Na..."wazuri huwa hawafi"
Na wanahoji ni nini kiko nyuma ya Pazia na jeuri zile za Makamba!
Nini kweli kilitokea?
Hivyo ukweli umebaki kwamba kuna mgawanyiko mkubwa ndani ya CCM kuliko ilivyo kwa CCM na Upinzani.
Asali Gang wametishika mno!
Hii kuruhusu vyama kufanya siasa, ni mbinu tu ya Samia kujaribu kubadili upepo ndani ya CCM ili wasahau tofauti zao na kuwageukia wapinzani baada ya kuruhusiwa siasa za majukwaani.
Fukuto ni kubwa, hata wajane walisusa huo ufunguzi wa Bwawa. Pamoja na kupewa mialiko.
Wale mnaojidanganya nguvu ya Magufuli imekwisha, kaeni mjitafakari.
Asali Gang wametishika na jinsi watu walivyomshabikia mtoto wa Magufuli alipokwenda kupokea tuzo kwa niaba ya baba yake.
Legacy ya Magufuli haiko kwa hao viongozi waliokuwa wafuasi wake tu. Ambao kwa sasa wanapukutishwa kutoka serikali ya Samia. Hao ni tone tu.
Bali Magufuli yuko kwenye mioyo ya watanzania wengi kwa asilimia kubwa sana. Kama hamuamini subirini 2025!
Halafu muwaone wale wanasiasa, watakaotumia majukwaa yao kumponda Marehemu Magufuli, watakachoambulia!
"Magufuli yupo na ataendelea kuwepo sana!"
Na huenda ndie mwanasiasa anayetajwa kwa wingi kila siku kuliko mwanasiasa yeyote nchini.
Nimemaliza wenye kutukana endeleeni kama kawaida, lakini huo ndio ukweli halisi. Sio mnavyofurahia maridhiano kama vile Samia kisha ridhiana na nyinyi akiondoka mtaingia nyinyi.
Alamsikhi
10101.
View attachment 2470604
Jiulizeni Mkurugenzi TISS kupelekwa Ikulu, kwa mfumo ule ule wa Lukuvi na Kabudi! Hamjifunzi jambo hapo tu? Pale wanaenda kuwekwa kwenye ulinzi wa karibu zaidi.
Na bado mengi yanafuatia!
Eti maridhiano!
Kwamba mmeridhiana Samia akiondoka atawaachia na nyinyi zamu yenu au?
Ukweli ni kwamba hali ndani ya CCM sio nzuri tangu Makamba Senior alipotoa zile kauli zake kwenye NEC Dodoma.
Imeleta mtarafuku mkubwa na ulianzia pale pale Dodoma.
Pamoja na Mwenyekiti wa CCM kuwaita wajumbe na kujaribu kuwatuliza.
Kwenye kikao kingine cha dharura jioni ile ile. Wajumbe wengi walikereka sana na kauli za Makamba!
Kwamba..." ilifika mahali wazee tukasema Hapana"
Na..."wazuri huwa hawafi"
Na wanahoji ni nini kiko nyuma ya Pazia na jeuri zile za Makamba!
Nini kweli kilitokea?
Hivyo ukweli umebaki kwamba kuna mgawanyiko mkubwa ndani ya CCM kuliko ilivyo kwa CCM na Upinzani.
Asali Gang wametishika mno!
Hii kuruhusu vyama kufanya siasa, ni mbinu tu ya Samia kujaribu kubadili upepo ndani ya CCM ili wasahau tofauti zao na kuwageukia wapinzani baada ya kuruhusiwa siasa za majukwaani.
Fukuto ni kubwa, hata wajane walisusa huo ufunguzi wa Bwawa. Pamoja na kupewa mialiko.
Wale mnaojidanganya nguvu ya Magufuli imekwisha, kaeni mjitafakari.
Asali Gang wametishika na jinsi watu walivyomshabikia mtoto wa Magufuli alipokwenda kupokea tuzo kwa niaba ya baba yake.
Legacy ya Magufuli haiko kwa hao viongozi waliokuwa wafuasi wake tu. Ambao kwa sasa wanapukutishwa kutoka serikali ya Samia. Hao ni tone tu.
Bali Magufuli yuko kwenye mioyo ya watanzania wengi kwa asilimia kubwa sana. Kama hamuamini subirini 2025!
Halafu muwaone wale wanasiasa, watakaotumia majukwaa yao kumponda Marehemu Magufuli, watakachoambulia!
"Magufuli yupo na ataendelea kuwepo sana!"
Na huenda ndie mwanasiasa anayetajwa kwa wingi kila siku kuliko mwanasiasa yeyote nchini.
Nimemaliza wenye kutukana endeleeni kama kawaida, lakini huo ndio ukweli halisi. Sio mnavyofurahia maridhiano kama vile Samia kisha ridhiana na nyinyi akiondoka mtaingia nyinyi.
Alamsikhi
10101.
View attachment 2470604