Uponyaji kupitia kukumbatia mti au kutembea msituni

Uponyaji kupitia kukumbatia mti au kutembea msituni

The redemeer

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2025
Posts
4,780
Reaction score
8,155
Miti ni waponyaji.
Unapokaa chini ya mti au kuukumbatia, unahisi nishati yake ya uponyaji. Ina nguvu ya asili inayotuliza akili na mwili.

Katika nchi kama Japani, kuna tiba inayoitwa Forest Therapy (Shinrin-yoku) — yaani tiba ya kuwa msituni — ambayo hutumika kusaidia watu waliokumbwa na msongo wa mawazo (anxiety) na mfadhaiko (depression).
Pia, harufu ya miti hutumika kama njia ya kuongeza kinga ya mwili kwa njia ya asili.

ukiwa karibu na miti, unaponywa kimwili na kiroho. Uumbaji huu wa asili unakutuliza, unakuinua, na kukurudisha kwenye hali ya usawa wa ndani. 🌳💚
 

Attachments

  • FB_IMG_1748671411993.jpg
    FB_IMG_1748671411993.jpg
    33.7 KB · Views: 27
Kama una matakataka yote kichwani katembeleeni sehemu za asili hasa ukiwa peku mfano porini, pembeni mwa bahari.
Unapona.
Jiulize kwann shule za mission za kikatoliki zinafanya vizuri huwezi sikia wanafunzi wanaanguka mapepo.
Siri ipo kwenye miti KAZI ya rangi ya kijani ni kufyonza matakataka yote kichwani sijui hasira, hangover,hofu, huzuni,nk na kuleta utulivu wa akili.
 
Hii dhana inaweza kuwa kweli, nikitembea msituni/porini na kukaa kivulini chini ya mti huwa najisikia vizuri sana
 
Hii dhana inaweza kuwa kweli, nikitembea msituni/porini na kukaa kivulini chini ya mti huwa najisikia vizuri sana
Unapata chaji mwili wa mwanadamu ni kama betri ya simu ikiwa low ndo hivyo unakuwa teja
 
Back
Top Bottom