Upole!!

Dr Lizzy

Platinum Member
Joined
May 25, 2009
Posts
31,010
Reaction score
60,472
Kwa faida ya kina kaka embu wadada tujuzane mnapenda wapenzi/wenzi wenu waweje linapokuja swala la upole.Hapa siongelei ule upole wa muda kwamba ikitokea ugomvi mara moja moja anaweza kujishusha ...naongelea ule upole ambao ndio tabia yake.Yani kila kitu ye anakua mdogo tu....hata kama kosa sio lake anakua mdogo...hata kama anaonewa anakua mdogo!!

Binafsi mi naogopa kua na mtu wa aina hii kwenye mahusiano kwasababu najijua ni mkorofi kidogo kwahiyo naona kama ntamuonea sana.Iwe kwa makusudi au la najua mwisho wa siku ntaishia kujisikia vibaya na ntakua nimeshamuonea tayari!!Napenda mtu ambae nikikosea atanipa live na sio kwakunibembeleza maana wakati mwingine mtu akikwambia kitu kwa utaratibu ni rahisi kupotezea ila ukiona kakasirika kweli usikilizaji na uelewaji unaongezeka!!

Michango tafadhali......
 


ok, afadhali umejitambua kwa hilo,
hata hivyo kwa jinsi ulivyo ni vema ukapata mpole!!!!!!!!!!!!!
 
UNAJUA NYIE MABINTI MNA MAtatizo sana, mwanamke ukimpenda kupita kiasi na ukiwa mpole sana kwake anakuita *****,zobalangu n.k.na anaweza kukuletea bwana mwingine hivihiviiiiiiiii. ukiwa mkali kila cku unampa kichapo anapokosea,mnasema mnanyanyaswa, ukiwa haueleweki wakati mwingine unakuwa mkali sana wakati mwingine mpole, utasikia oooh, hili bwana langu hata silielewi, sijui lLINANIPENDA KWELI? WALA HALIELEWEKI, MIM "I PREFER TO BE UNPREDICTABLE"
 

afazali leo umetuongelea wanaume wapole, yaani tunanyanyaswa kweli aisee.
 
ok, afadhali umejitambua kwa hilo,
hata hivyo kwa jinsi ulivyo ni vema ukapata mpole!!!!!!!!!!!!!

Kujitambua ni muhimu....that way unajua kabisa nini kinakufaa na nini hakikufai!!
Mhhh mpole atanifaa vipi wakati sitaki kumtoa machozi mtoto wa watu????
 
Unapenda wakali lizzy, tena wa kukupigapiga kwa marungu hata kwa vijikosa vidogo jamani? Au nimekosea bibie?
 
Mpole wa namna hiyo hapana, atakuwa hajiamini mwoga
maana hata kutoa ushauri itakuwa vigumu
mtakuwa mnashauriana vipi kama kila kitu ndio
upole uwe wa kawaida, mcheshi

 


Kila kitu kiwe na kiasi!!Mambo ya kukatana ngwara kwenye mahusiano sio vizuri kabisaaaaa!!Na huyo anaetumia upole wako kukuletea mwanaume ndani kama ungekua mkali asingekuletea ndani ila bado angekuzunguka tu!!!
 

Upole asilia hauji kwa kuamua kichwani bali anakuwa nao mtu tangu anakua.
Wewe hata sasa huwezi tena kuwa mpole.
Binafsi sijazoea kufokea mtu, kumkasirikia mtu au kumpiga, especially kama nimfanyie haya mke (nikija kuoa). Why???

Nilivyokuwa nakua (nilivyokuwa primary school 1987 - 1993) nimepitia yote hayo.
So najua uchungu wake na jinsi mtu unavyokosa amani.
Najiuliza siku zote, hivi hakuna njia nyingine ya kumfundisha mtu na kumuelimisha kwamba hiki na kile hakitakiwi zaidi ya kumkaripia, kumpiga, kumfokea n.k???
 
Mpole wa namna hiyo hapana, atakuwa hajiamini mwoga
maana hata kutoa ushauri itakuwa vigumu
mtakuwa mnashauriana vipi kama kila kitu ndio
upole uwe wa kawaida, mcheshi

Blaki Womani,

Nimeongeza size ya fonts kwenye post yako niweze kukusoma vizuri!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…