Upishi wa Pilau ya Nyama na Kachumbari

Jade_

Senior Member
Apr 19, 2015
122
214
Hali zenu wana mapishi, natumai mpo salama. Wiki iliyopita nilionyesha namna nilivyopika biskuti za tangawizi. Leo nawashirikisha namna ya kupika pilau ya nyama na kachumbari. Hiki chakula kilisindikizwa na white sauce niliyopika h a p a.

Ukitaka kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.


Turudi kwenye mapishi yetu.
Pilau
Nilianza kupika pilau kwa kukaanga vitunguu kwenye mafuta ya mzaituni (olive oil) mpaka vilivyoanza kunyauka. Baada ya hapo niliweka kitunguu saumu kilichotwangwa nikakangaa kidogo na baadaye nikaweka tangawizi na nikaendelea kukaanga.
Pic 1.jpg

Nikianza kukaanga vitunguu kwenye mafuta

Pic 2.jpg

Nikiweka kitunguu saumu

Pic 3.jpg

Nikiendelea kukaanga vitunguu baada ya kuweka tangawizi

Baada ya vitunguu kupata rangi, niliweka viungo vya pilau (pilau masala), nikakaanga kidogo na nikaongeza vitunguu vingine ili kuzimua harufu na ladha ya vitunguu visivyoungua. Nikakaanga kidogo halafu nikaweka vipande vya nyama vilivyopikwa na chumvi, nikakaanga tena.
Pic 4.jpg

Nikiweka viungo vya pilau

Pic 5.jpg

Nikiongeza vitunguu vingine

Pic 6.jpg

Nikiweka vipande vya nyama vilivyopikwa

Nilivyomaliza kuzikaanga nyama, niliweka maji ya moto nikafunika mchanganyiko mpaka ukachemka. Ulivyochemka niliweka majani ya bay (bay leaves) na nikaacha ichemke mpaka vitunguu vyote vikalainika. Niliweka maji ya moto ya kutosha nikaacha mchanganyiko uchemke tena.
Pic 8.jpg

Mchanganyiko baada ya kuweka maji ya moto

Pic 9.jpg

Nilivyoweka majani ya bay

Maji ya pilau yalivyochemka nilitoa majani ya bay na nikaweka mchele wa kawaida (sio basmati) ukachemka mpaka ukaiva.
Pic 10.jpg

Nikiweka mchele

Pic 11.jpg

Mchele ukichemka

Pic 12.jpg

Pilau imeiva

Kachumbari
Nilianza kutengeneza kachumbari kwa kuchanganya vinegar, olive oil chumvi na mnanaa (mint) uliyosagwa wenye sukari, nikaweka pembeni. Kwenye chombo kingine niliweka kitunguu na nyanya na baadaye nikamiminia mchanganyiko wetu tuliyotayarisha nikachanganyia.
Pic 13.jpg

Mchanganyiko wa vinegar, olive oil, chumvi na mnanaa wenye sukari

Pic 14.jpg

Mchanganyiko wa nyanya na vitunguu

Pic 15.jpg

Nikichanganya viungo vyote vya kachumbari

Pic 16.jpg

Pilau, kachumbari, na kwenye bakuli ni white sauce

Pic 17.jpg

Pilau, kachumbari na white sauce kwa ukaribu
 
Hali zenu wana mapishi, natumai mpo salama. Wiki iliyopita nilionyesha namna nilivyopika biskuti za tangawizi. Leo nawashirikisha namna ya kupika pilau ya nyama na kachumbari. Hiki chakula kilisindikizwa na white sauce lakini sionyeshi nilivyopika white sauce hapa, ila kwenye uzi mwingine.

Ukitaka kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.


Turudi kwenye mapishi yetu.
Pilau
Nilianza kupika pilau kwa kukaanga vitunguu kwenye mafuta ya mzaituni (olive oil) mpaka vilivyoanza kunyauka. Baada ya hapo niliweka kitunguu saumu kilichotwangwa nikakangaa kidogo na baadaye nikaweka tangawizi na nikaendelea kukaanga.
View attachment 2491122
Nikianza kukaanga vitunguu kwenye mafuta

View attachment 2491123
Nikiweka kitunguu saumu

View attachment 2491124
Nikiendelea kukaanga vitunguu baada ya kuweka tangawizi

Baada ya vitunguu kupata rangi, niliweka viungo vya pilau (pilau masala), nikakaanga kidogo na nikaongeza vitunguu vingine ili kuzimua harufu na ladha ya vitunguu visivyoungua. Nikakaanga kidogo halafu nikaweka vipande vya nyama vilivyopikwa na chumvi, nikakaanga tena.
View attachment 2491127
Nikiweka viungo vya pilau

View attachment 2491129
Nikiongeza vitunguu vingine

View attachment 2491130
Nikiweka vipande vya nyama vilivyopikwa

Nilivyomaliza kuzikaanga nyama, niliweka maji ya moto nikafunika mchanganyiko mpaka ukachemka. Ulivyochemka niliweka majani ya bay (bay leaves) na nikaacha ichemke mpaka vitunguu vyote vikalainika. Niliweka maji ya moto ya kutosha nikaacha mchanganyiko uchemke tena.
View attachment 2491131
Mchanganyiko baada ya kuweka maji ya moto

View attachment 2491132
Nilivyoweka majani ya bay

Maji ya pilau yalivyochemka nilitoa majani ya bay na nikaweka mchele wa kawaida (sio basmati) ukachemka mpaka ukaiva.
View attachment 2491133
Nikiweka mchele

View attachment 2491134
Mchele ukichemka

View attachment 2491137
Pilau imeiva

Kachumbari
Nilianza kutengeneza kachumbari kwa kuchanganya vinegar, olive oil chumvi na mnanaa (mint) uliyosagwa wenye sukari, nikaweka pembeni. Kwenye chombo kingine niliweka kitunguu na nyanya na baadaye nikamiminia mchanganyiko wetu tuliyotayarisha nikachanganyia.
View attachment 2491138
Mchanganyiko wa vinegar, olive oil, chumvi na mnanaa wenye sukari

View attachment 2491139
Mchanganyiko wa nyanya na vitunguu

View attachment 2491140
Nikichanganya viungo vyote vya kachumbari

View attachment 2491141
Pilau, kachumbari, na kwenye bakuli ni white sauce

View attachment 2491145
Pilau, kachumbari na white sauce kwa ukaribu
karbu nkufundishe pilau la nyanya nikikupikia huitaji hata kachumbali kwa utam
 
Hutaacha ukilianza na walaji wataona utofauti. Lina ladha yake ya kipekee, huo mchanganyiko wake kabla ya kuweka mchele, ni kama roast fulani. Mtu akiliona mwanzoni hatojua unapika pilau, akila sasa 😋😋😋😋
Jaribu siku dear sophy27 utanipa mrejesho.
Nyanya ni tomato paste au za kawaida ndio nzuri?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom