Upinzani Tanzania unanipa shida

FredKavishe

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,090
318
Niweke wazi mimi ni mwanachama hai wa Chadema.
Turudi kwenye mada tunaelekea uchaguzi wa wabunge wa East Africa week ijao lakini upinzani huu tulionao wote unaenda kwenye uchaguzi ukiwa haueleweki.

Sheria zilizolipotia zinasema Chadema 2 CUF 1 CCM 6(Wabunge wa kwenda bungeni East Africa),Ndugu Zitto aka raise hoja kwamba wabunge wa upinzani wote wanaweza gombea kutokana na chama kikiwa na uwakilishi Bungeni,Akamuandikia Spika barua ambayo bado haijapata majibu mpaka sasa.

Turudi historia nyuma kidogo mwaka 2015 kulikua na muungano wa Ukawa(NCCR,CUF,CHADEMA,NLD) Huku ACT ilisimama wenyewe.Lakini kwenye huu Ukawa kuna wagombea wengi waliacha kusimama kwenye udiwani ama ubunge kisa hii Ukawa lengo likiwa ni moja kumtoa CCM.

Sote hatuwezi kataa haswa kwa Kigoma,ACT iligawa kura nyingi na kufanya majimbo mengi yaliyokuwa chini ya NCCR kupotea,inawezekana kuhama kwa kina Zitto,Kitila na wenzake kulisababishwa na kupishana kimawazo wakati wakiwa Chadema,Lakini yaliyopita si ndwele tugange yajayo.Ndio maana tulimuona Ndugu Lema(Mb Arusha) kwenye mkutano wa ACT akisema upinzani unahitaji sauti moja.

Tukirudi kwenye mada tukubali asilimia 18 ya wabunge wa CHADEMA ilichangiwa na UKAWA maana kuna sehemu CUF na CHADEMA walirudisha wote fomu tulikosa majimbo kama Ukonga,Segerea.Kwahiyo kama kulikua na mchango wa UKAWA kwanini CHADEMA hawakukaa na wenzao kushauriana tupeleke kina nani ama wakati wa kushirikiana umeisha tunasubiri 2019 tuanze muungano wa kinafki tena.

Ndugu zangu wapinzani siasa ni hesabu,uongo kwenye hesabu huangukia pua haraka sana,tunahitaji umoja kwenye Upinzani.Ifahamike lengo letu sio vyeo lengo letu ni kuleta Elimu bure,Afya ya tija,Maendeleo,Ajira hili ndio lengo na Act,Chadema,Cuf hawawezi fanikiwa wao kama wao bila ushirikiano kuunda upinzani wenye nguvu.

Daima tuamini upinzani ukiwa mmoja wenye nguvu tutawashinda wapinzani wetu,karaha ya Wabunge wa Africa Mashiriki kwa kweli ina kera inafahamika Cuf ina matatizo yake hayo tuache lakini Chadema kufanya mchakato bila kuwashirikisha washiriki wenzake kwenye Ukawa ni ukakasi mkubwa.Bila kuwasahau Act wanahitajika kujenga upinzani imara rejea matokeo ya Uchaguzi mkuu Kigoma,Rejea matokeo ya Udiwani mwaka jana.

Mtafanya sisi vijana tuanze uliza maswali mnataka badilisha hii nchi kweli ama mnataka madaraka,umoja wa upinzani kwa maendeleo ya kweli.Tuanze na Ubunge wa East Africa
 
Upinzani Tanzania ni chadema tu hao wengine uliowataja hawaaminiki. Hivi leo chadema ijiunge na Lipumba kuna usalama hapo? Watanzania tunaikubali Chadema hao wengine tunawaona kama mamluki tu waliotumwa na CCM kutuvuruga.
 
Upinzani Tanzania bado sana,
kila mmoja anataka Kuvutia kwake
Chadema ime jimilikisha upinzani wa Tanzania
kila kitu inakiweka kiubinafsi zaidi,
Cdm hawataki kuona kuna upinzani Tanzania zaidi yao,
Hii Ukawa ni kiini macho tu
cdm hawana malengo hayo.
 
Upinzani Tanzania ni chadema tu hao wengine uliowataja hawaaminiki. Hivi leo chadema ijiunge na Lipumba kuna usalama hapo? Watanzania tunaikubali Chadema hao wengine tunawaona kama mamluki tu waliotumwa na CCM kutuvuruga.

Ni ujinga kudhani hivyo
upinzani ni cdm!!kwa lengo gani hasa kwa watanzania
ikiwa cdm yenyewe imeshindwa kujiongoza kwa misingi ya demokrasia na kumkomboa Mtanzania!!
Chama hakina utaratibu wakupata viongozi zaidi ya kuteuana Chumbani!!

chama kinakuwa si chawanachama
bali chama cha wahuni fulani pekee!!
Chama maamuzi yake yapo mfukoni mwa Mbowe na wahuni wachache!!
Tanzania upinzani bado sana
 
wanapinzana wenyewe,, unategemea nini.. nguvu ya mnyonge ni umoja
 
Upinzani Tanzania ni chadema tu hao wengine uliowataja hawaaminiki. Hivi leo chadema ijiunge na Lipumba kuna usalama hapo? Watanzania tunaikubali Chadema hao wengine tunawaona kama mamluki tu waliotumwa na CCM kutuvuruga.

CUF nimeshasema wana shida zao waweke pembeni.

Ukisema upinzani mmoja unakosea mbona hukusema 2015 upinzani mmoja tu ambao ni Chadema,tufunguke zaidi
 
CUF nimeshasema wana shida zao waweke pembeni.

Ukisema upinzani mmoja unakosea mbona hukusema 2015 upinzani mmoja tu ambao ni Chadema,tufunguke zaidi
Mkuu mwanzo tulidhani CUF ni wenzetu kumbe wametumwa na CCM.
 
Ni ujinga kudhani hivyo
upinzani ni cdm!!kwa lengo gani hasa kwa watanzania
ikiwa cdm yenyewe imeshindwa kujiongoza kwa misingi ya demokrasia na kumkomboa Mtanzania!!
Chama hakina utaratibu wakupata viongozi zaidi ya kuteuana Chumbani!!

chama kinakuwa si chawanachama
bali chama cha wahuni fulani pekee!!
Chama maamuzi yake yapo mfukoni mwa Mbowe na wahuni wachache!!
Tanzania upinzani bado sana
Hizi fitna mnazopiga ili chadema igawanyike kama Maalim seif na Lipumba hazitafanikiwa. Chadema imeimarika sana na itabaki kuwa chama chenye msimamo na hakitayumbishwa na fitna za CCM.
 
Upinzani Tanzania bado sana,
kila mmoja anataka Kuvutia kwake
Chadema ime jimilikisha upinzani wa Tanzania
kila kitu inakiweka kiubinafsi zaidi,
Cdm hawataki kuona kuna upinzani Tanzania zaidi yao,
Hii Ukawa ni kiini macho tu
cdm hawana malengo hayo.
Chadema ni chama makini huwezi kukaa meza moja na Lipumba ukasema mna malengo yanayofanana.wakati mwenzenu analipwa na CCM ili kuwavuruga. Kama ni ukawa wa style ya lipumba bora ufe.hatuwezi kukaa na joka ndani.
 
Upinzani Tanzania ni chadema tu hao wengine uliowataja hawaaminiki. Hivi leo chadema ijiunge na Lipumba kuna usalama hapo? Watanzania tunaikubali Chadema hao wengine tunawaona kama mamluki tu waliotumwa na CCM kutuvuruga.
wewe unatuongelea watanzania tumekupa uwakilishi?
 
Upinzani Tanzania bado sana,
kila mmoja anataka Kuvutia kwake
Chadema ime jimilikisha upinzani wa Tanzania
kila kitu inakiweka kiubinafsi zaidi,
Cdm hawataki kuona kuna upinzani Tanzania zaidi yao,
Hii Ukawa ni kiini macho tu
cdm hawana malengo hayo.
Lipumba ni wenu.
 
Ndugu yangu watanzania wataendelea kuteseka kwani hakuna wabunge kutoka upinzani wala chama tawala wapo kwa maslahi ya watanzania sana sana miezi miwili porojo zitapigwa pale bungeni na kila mbunge ataondoka na kitita cha posho ya walipa kodi masikini.
Tujifunze kutoka Kenya leo wameunda umoja wa vyama vya siasa NASA kuelekea uchaguzi mkuu na wamesaini hati ya makubaliano ikiwa wakishinda uchaguzi mkuu watakavyogawana madaraka.
 
Back
Top Bottom