Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,866
- 4,252
Ndio maono yangu. Kuna dalili kadha wa kadha zinazoashiria upinzani kupewa wizara moja ambayo ni ya Fedha. Wanasema mchawi mpe mwanao amlee. Katika kuutazama upinzani nikaona hakuna dalili ya UKAWA kwenye safu ya uwaziri. Ndipo nikamuona kiongozi mkuu wa ACT akipewa jukumu hilo. ACT waliandaa maandamano ya kumpongeza Rais Magufuli katika utendaji wake. Cheki hapa Kwa upande wa UKAWA wao wanadai kuwa Magufuli anatekeleza ilani ya UKAWA ila haitekelezi ipasavyo.
Baadhi ya viashiria.
1. Zitto kupongezwa na Rais kubaki Bungeni wakati wa hotuba yake.
2. Zitto kukutanishwa na Magufuli kupitia Kikwete.
3. Zitto kuwa mtaalam wa uchumi na mambo ya fedha
4. Zitto kuwa karibu zaidi na chama tawala kuliko wapinzani wengine. Rejea hata kubadilishana majimbo na Serukamba
5. Zitto kuongoza kamati ya POAC/PAC kwa ufanisi na muda mrefu.
6. Rais kutotenda haki kwa wabunge wa majimbo kwa kutowateua kuwa mawaziri
7. Rais kupenda kushitukiza kwa matukio ya uteuzi. Mfano kwa Waziri mkuu Majaliwa.
8. Rais kutimiza kauli yake kuwa yeye ni Rais wa wote bila kujali itikadi, vyama, dini, n.k.
9. Rais kutaka kuzima 'kelele' za upinzani bungeni na serikalini
10. Na mengine mengi
Hivyo yawezekana tukashuhudia hiki ninachokifikiria. Tatizo CCM watamwelewa Rais? Ni jambo la kukaa na kusubiria.
Baadhi ya viashiria.
1. Zitto kupongezwa na Rais kubaki Bungeni wakati wa hotuba yake.
2. Zitto kukutanishwa na Magufuli kupitia Kikwete.
3. Zitto kuwa mtaalam wa uchumi na mambo ya fedha
4. Zitto kuwa karibu zaidi na chama tawala kuliko wapinzani wengine. Rejea hata kubadilishana majimbo na Serukamba
5. Zitto kuongoza kamati ya POAC/PAC kwa ufanisi na muda mrefu.
6. Rais kutotenda haki kwa wabunge wa majimbo kwa kutowateua kuwa mawaziri
7. Rais kupenda kushitukiza kwa matukio ya uteuzi. Mfano kwa Waziri mkuu Majaliwa.
8. Rais kutimiza kauli yake kuwa yeye ni Rais wa wote bila kujali itikadi, vyama, dini, n.k.
9. Rais kutaka kuzima 'kelele' za upinzani bungeni na serikalini
10. Na mengine mengi
Hivyo yawezekana tukashuhudia hiki ninachokifikiria. Tatizo CCM watamwelewa Rais? Ni jambo la kukaa na kusubiria.