Upinzani: Katibu Mkuu CCM anashawishi wabunge wake wakatae mabadiliko yaliyofanywa na Kamati kwenye Muswada

Queen V

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
776
1,330
Vyama 10 vya Upinzani leo vimefanya mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa.

Vyama hivyo vimefanya hivyo leo Januari 27 ikiwa ni miaka 18 tangu machafuko yaliyotokea Zanzibar mwaka 2001 kufuatia madai ya udhalimu wa kisiasa yaliyopelekea mauaji ya watu 46 na majeruhi zaidi ya 600 huku Tanzania kwa mara ya kwanza ikizalisha wakimbizi ambapo watu takribani 2000 walikimbilia Mombasa.

Katika taarifa yao, wameipongeza Kamati ya Bunge kwa kuweza kubadili baadhi ya vifungu ambavyo walivizungumzia hapo awali katika Muswada.

Moja ya mambo waliyopongeza ni kuondolewa kwa hati yenye mashaka kama kigezo cha chama kusitishiwa ruzuku.

Licha ya mabadiliko hayo, wamesema kuwa bado muswada huo unahitaji marekebisho zaidi ikiwemo kupunguzwa kwa Ujinai wa Vyama vya Siasa. Wanaelezea kuwa karibu kila kifungu kina adhabu na ingawa kamati imejitahidi kupunguza lakini bado mkazo unahitajika.

"Haya Mambo kama ugaidi yana Sheria zake, tuyaache yashughulikiwe na sheria zake ili kufanya siasa nchini Tanzania isigeuke kuwa jinai" amesema Salum Mwalim(CHADEMA).

Jambo lingine walilozungumzia ni suala la kukataza vijana kufanya siasa vyuoni. Wamesema hakuna chuo cha siasa hivyo vijana waachwe wajijenge tangu vyuoni na kama kuna haja ya kudhibiti uwekwe utaratibu watakaolazimika kuufuata.

Pia wamemshutumu Katibu Mkuu wa CCM kuwa yuko Dodoma kuwashawishi Wabunge wa chama chake kuyakataa mabadiliko yaliyofanywa na Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ili kusimamia ahadi/dhamira aliyoweka ya muswada kupita kama ulivyo.

Salum Mwalimu amehoji kuwa, kama CCM hawakutaka mabadiliko katika muswada, kwanini Katibu Mkuu na Katibu Mwenezi walienda kutoa maoni mbele ya Kamati.

Amewaasa Wabunge wa CCM kufuata nyayo za wenzao walio kwenye Kamati ya Katiba na Sheria katika kuweka maslahi ya nchi mbele pindi Muswada utakaposomwa mara ya pili na kujadiliwa.
 
unajua Zitto na wenzie sijui wanakunywa vinywaji gani sikuhizi! kwani kutoa maoni ni kosa.!!
 
Wao wana Mamlaka na kwa Sheria /Muundo wa Chama na Serikali ni kama Ubunge kwao wame Zawadiwa ,wataamiliwa cha kusema na cha kufanya kwa Maslahi ya Chama chini ya Mwamvuli wa Bunge kupitisha (Uhalali) chochote.

Ila wakumbuke ,zilikuwepo Falme zenye Nguvu na hazipo tena so wafanye mambo kwa Maslahi ya Nchi na sio Vyama ambavyo vinapita tu kama Binadamu wanavyo pita hapa Duniani.
 
Vyama 10 vya Upinzani leo vimefanya mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa.

Vyama hivyo vimefanya hivyo leo Januari 27 ikiwa ni miaka 18 tangu machafuko yaliyotokea Zanzibar mwaka 2001 kufuatia madai ya udhalimu wa kisiasa yaliyopelekea mauaji ya watu 46 na majeruhi zaidi ya 600 huku Tanzania kwa mara ya kwanza ikizalisha wakimbizi ambapo watu takribani 2000 walikimbilia Mombasa.

Katika taarifa yao, wameipongeza Kamati ya Bunge kwa kuweza kubadili baadhi ya vifungu ambavyo walivizungumzia hapo awali katika Muswada.

Moja ya mambo waliyopongeza ni kuondolewa kwa hati yenye mashaka kama kigezo cha chama kusitishiwa ruzuku.

Licha ya mabadiliko hayo, wamesema kuwa bado muswada huo unahitaji marekebisho zaidi ikiwemo kupunguzwa kwa Ujinai wa Vyama vya Siasa. Wanaelezea kuwa karibu kila kifungu kina adhabu na ingawa kamati imejitahidi kupunguza lakini bado mkazo unahitajika.

"Haya Mambo kama ugaidi yana Sheria zake, tuyaache yashughulikiwe na sheria zake ili kufanya siasa nchini Tanzania isigeuke kuwa jinai" amesema Salum Mwalim(CHADEMA).

Jambo lingine walilozungumzia ni suala la kukataza vijana kufanya siasa vyuoni. Wamesema hakuna chuo cha siasa hivyo vijana waachwe wajijenge tangu vyuoni na kama kuna haja ya kudhibiti uwekwe utaratibu watakaolazimika kuufuata.

Pia wamemshutumu Katibu Mkuu wa CCM kuwa yuko Dodoma kuwashawishi Wabunge wa chama chake kuyakataa mabadiliko yaliyofanywa na Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ili kusimamia ahadi/dhamira aliyoweka ya muswada kupita kama ulivyo.

Salum Mwalimu amehoji kuwa, kama CCM hawakutaka mabadiliko katika muswada, kwanini Katibu Mkuu na Katibu Mwenezi walienda kutoa maoni mbele ya Kamati.

Amewaasa Wabunge wa CCM kufuata nyayo za wenzao walio kwenye Kamati ya Katiba na Sheria katika kuweka maslahi ya nchi mbele pindi Muswada utakaposomwa mara ya pili na kujadiliwa.
Kama Msajili wa Vyama ni Kada , ndio maana Ccm inaupongeza Muswada huo kwani lengo ni baya kwa Vyama vya Upinzani ndio maana Katibu mwenezi anausifia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kama akina bashuru wako huko basi jua kua muswada utapita kama ulivyo, hawa jamaa wako tayari hata kuwahonga wabunge wetu wapitishe na pia kuiona kamati ya bunge si chochote! wapigania demokrasia hili ni pigo kubwa sana, na inasikitisha na inahuzunisha sana!
 
Vyama 10 vya Upinzani leo vimefanya mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa.

Vyama hivyo vimefanya hivyo leo Januari 27 ikiwa ni miaka 18 tangu machafuko yaliyotokea Zanzibar mwaka 2001 kufuatia madai ya udhalimu wa kisiasa yaliyopelekea mauaji ya watu 46 na majeruhi zaidi ya 600 huku Tanzania kwa mara ya kwanza ikizalisha wakimbizi ambapo watu takribani 2000 walikimbilia Mombasa.

Katika taarifa yao, wameipongeza Kamati ya Bunge kwa kuweza kubadili baadhi ya vifungu ambavyo walivizungumzia hapo awali katika Muswada.

Moja ya mambo waliyopongeza ni kuondolewa kwa hati yenye mashaka kama kigezo cha chama kusitishiwa ruzuku.

Licha ya mabadiliko hayo, wamesema kuwa bado muswada huo unahitaji marekebisho zaidi ikiwemo kupunguzwa kwa Ujinai wa Vyama vya Siasa. Wanaelezea kuwa karibu kila kifungu kina adhabu na ingawa kamati imejitahidi kupunguza lakini bado mkazo unahitajika.

"Haya Mambo kama ugaidi yana Sheria zake, tuyaache yashughulikiwe na sheria zake ili kufanya siasa nchini Tanzania isigeuke kuwa jinai" amesema Salum Mwalim(CHADEMA).

Jambo lingine walilozungumzia ni suala la kukataza vijana kufanya siasa vyuoni. Wamesema hakuna chuo cha siasa hivyo vijana waachwe wajijenge tangu vyuoni na kama kuna haja ya kudhibiti uwekwe utaratibu watakaolazimika kuufuata.

Pia wamemshutumu Katibu Mkuu wa CCM kuwa yuko Dodoma kuwashawishi Wabunge wa chama chake kuyakataa mabadiliko yaliyofanywa na Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ili kusimamia ahadi/dhamira aliyoweka ya muswada kupita kama ulivyo.

Salum Mwalimu amehoji kuwa, kama CCM hawakutaka mabadiliko katika muswada, kwanini Katibu Mkuu na Katibu Mwenezi walienda kutoa maoni mbele ya Kamati.

Amewaasa Wabunge wa CCM kufuata nyayo za wenzao walio kwenye Kamati ya Katiba na Sheria katika kuweka maslahi ya nchi mbele pindi Muswada utakaposomwa mara ya pili na kujadiliwa.
Unafiki tu. Kwani chanzo cha musuada ni nani kama sio chama chake?
 
kama akina bashuru wako huko basi jua kua muswada utapita kama ulivyo, hawa jamaa wako tayari hata kuwahonga wabunge wetu wapitishe na pia kuiona kamati ya bunge si chochote! wapigania demokrasia hili ni pigo kubwa sana, na inasikitisha na inahuzunisha sana!
Bashiru anaishi huko, ndiko ofisi zake rasmi zilipo. Makao makuu ya chama anachokiongoza yako Dodoma.
 
Vyama 10 vya Upinzani leo vimefanya mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa.

Vyama hivyo vimefanya hivyo leo Januari 27 ikiwa ni miaka 18 tangu machafuko yaliyotokea Zanzibar mwaka 2001 kufuatia madai ya udhalimu wa kisiasa yaliyopelekea mauaji ya watu 46 na majeruhi zaidi ya 600 huku Tanzania kwa mara ya kwanza ikizalisha wakimbizi ambapo watu takribani 2000 walikimbilia Mombasa.

Katika taarifa yao, wameipongeza Kamati ya Bunge kwa kuweza kubadili baadhi ya vifungu ambavyo walivizungumzia hapo awali katika Muswada.

Moja ya mambo waliyopongeza ni kuondolewa kwa hati yenye mashaka kama kigezo cha chama kusitishiwa ruzuku.

Licha ya mabadiliko hayo, wamesema kuwa bado muswada huo unahitaji marekebisho zaidi ikiwemo kupunguzwa kwa Ujinai wa Vyama vya Siasa. Wanaelezea kuwa karibu kila kifungu kina adhabu na ingawa kamati imejitahidi kupunguza lakini bado mkazo unahitajika.

"Haya Mambo kama ugaidi yana Sheria zake, tuyaache yashughulikiwe na sheria zake ili kufanya siasa nchini Tanzania isigeuke kuwa jinai" amesema Salum Mwalim(CHADEMA).

Jambo lingine walilozungumzia ni suala la kukataza vijana kufanya siasa vyuoni. Wamesema hakuna chuo cha siasa hivyo vijana waachwe wajijenge tangu vyuoni na kama kuna haja ya kudhibiti uwekwe utaratibu watakaolazimika kuufuata.

Pia wamemshutumu Katibu Mkuu wa CCM kuwa yuko Dodoma kuwashawishi Wabunge wa chama chake kuyakataa mabadiliko yaliyofanywa na Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ili kusimamia ahadi/dhamira aliyoweka ya muswada kupita kama ulivyo.

Salum Mwalimu amehoji kuwa, kama CCM hawakutaka mabadiliko katika muswada, kwanini Katibu Mkuu na Katibu Mwenezi walienda kutoa maoni mbele ya Kamati.

Amewaasa Wabunge wa CCM kufuata nyayo za wenzao walio kwenye Kamati ya Katiba na Sheria katika kuweka maslahi ya nchi mbele pindi Muswada utakaposomwa mara ya pili na kujadiliwa.
Hivi wapinzani hawajui siasa au wadhani watu wanacheza. Anachofanya huyo KM si ndiyo kazi yake. Wabunge wa CCM kusupport agenda za CCM si ndiyo kazi yao. Kama vile kazi ya wananchi kupiga chama fulani ilikishike madaraka na kupitisha agenda zao kwa niaba ya wananchi kama wakifeli wanapigwa chini baada ya miaka mitano. Waache malalamiko ya kijinga kisa wanashindwa kuzuia huo muswada.
 
Ndugu zangu,

Baada ya mdogo wangu Zitto Kabwa kuwaajidi wafuasi wake wakae mkao wa tayari na bashasha kufuatilia harakati zake kwa mwaka 2019, nilijiandaa kumfuatilia ili nijue hatma yake.

Kama kawaida aliunza mwaka 2019 katika viunga vya mahakamani akiishitaki bunge na serikali huku akilazimisha tafsiri yake juu ya mambo kadhaa ndio sahihi kikatiba. Hatahivyo, ameanguka mahakamani kwa angalau mara mbili japo amefanikiwa kuwahataa wafuasi wake mitandaoni kuwa anahujumiwa.

Kwa upande wa Bungeni aliamua kuiandama serikali na hususani Rais Magufuli kuwa anazuia ripoti za CAG zisijadiliwe hadi akafikia hatua ya kuzusha ati Ndugu Rais anampango wa kumteua CAG mpya.

Kurunzi langu limepitia ripoti za CAG na kukuta hakuna kitu cha maana hivyo kuna propaganda imeandaliwa na Zitto kuwashawishi wabunge wa upinzani kutoka nje.

Nawasilisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zitto amewashika pabaya CCM mpaka bwana jobu uvumilivu ukamshinda akatoa ya moyoni kuhusu Zitto anavyomchachafya.

Endesheni nchi vizuri ili wapinzani waishiwe hoja.
Vinginevyo mtahitahidi kuzima wapinzani na hamtaweza kamwe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Wachache Wenye hekima wanaosema tofauti ndio salama na pona yetu. Kuliko wanafiki wengi wanaokaa kimya na wanaopiga makofi kila uchao. Anaekukosoa ndie rafiki wa kweli, Tuheshimu sana kioo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi naomba nisiwe na UPANDE, nianze na wewe; nini msimamo wako juu ya zile pesa ambazo hazijulikani jinsi zilivyo tumika, I mean zile Tsh 1.5 T ambazo mkaguzi mkuu wa serikali ali question na hadi leo hakuna majibu halisi. Wewe unazungumziaje juu ya hilo? Lingine ni hili, CAG pia alionesha wasiwasi wake juu ya mapato ambayo TRA wana declare kwamba wamekusanya kumbe sio ya kwao, wewe pia mawazo yako yakoje juu ya hayo mambo mawili, tuachane na bunge na mahakama.
 
Halafu wakitafutwa wahujumu uchumi wanapelekwa kina kitilya mahakamani mwaka wa nne sasa.Huyu Bashiru anachofanya ni afadhali ya mhujumu uchumi.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nahisi hi Ni Episode nyingine ngoja niongezee Luku, umeme usikate nikakosa uhondo mwingine🤣🤣🤣🤣. Maana Tanzania kwa Sasa VIONGOZI wetu kila kukicha Inaandaliwa Episode
 
Tunatunga sheria nyiingi zisizo na tija kwa taifa. Hizi sheria zilizopo tu bado wanasheria hawajazielewa. Tunawaongezea mzigo kila uchao kujifunza sheria mpya zisizo na tija.
Hao wanaozitunga leo wakiwa wamestaafu watapata taabu sana wasiokuwa na akili wakija kushika madaraka na kuzitumia vibaya.
Ni sawa na kuunda mabomu ya nyuklia alafu kiongzi ajaye akawa kichaa kama Kim akaamua kuyatumia kuua watu wake.
Taifa bila uhuru wa kisiasa litadumaa.
Angalia mfano wa Nyerere. Pamoja na kukaa madarakani miaka 23 nchi ilidumaa kwa kuwa hakukua na siasa. Kipindi cha Mwinyi vile vile.
Maendeleo ambayo nchi ilipata kipindi cha upinzani mkali cha JK ni zaidi ya mara dufu ya awamu tatu zilizopita.
Maendeleo ambayo nchi imepata kwa kipindi kifupi cha miaka mitatu ya Magu yatakuwa mara dufu ya maendeleo yatakayopatikana kwa miaka saba iliyobaki ENDAPO tutaua siasa za ushindani.
Siasa zikifa kila mtu atajisahau na wote tutalala usingizi.
Kifupi, siungi mkono kabisa sheria hii kwa kuwa inakwenda kudumaza harakati za maendeleo ya taifa.
Sheria hii ni sawa na mwenye mali kuzima taa kupunguza matumizi ya umeme huku akimnufaisha mlinzi kwa kumpa wasaa wa kulala lindoni.
 
ule muswada ni wa vyama vya siasa hivyo hakuna tatizo kwa katibu mkuu na katibu mwenezi kwenda kutoa maoni kwenye kamati pia hakuna kosa kwa katibu mkuu kushawishi wanachama wake kukataa baadhi ya vifungu ambavyo vimebadirishwa hawa kina Salum Mwaimu wamekosa pointi ndio maana baba wa taifa aliviambia vyama vya upinzani visianze kukimbilia urais bali viweke nguvu kwenye ubunge lakini walimwona mjinga badala ya kulalamika hakikishenji mnakuwa na wabunge wengi hivi ndivyo siasa ya vyama vingi ilivyo msitegemee wabunge wa CCM watakwenda kuwakilisha matakwa yenu
 
Back
Top Bottom