Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 339
- 677
Leo asubuhi nilipoamka nilikutana na Tweet moja ya Mh. Jakaya Kikwete Rais Mstaafu wa Tanzania. Twitter iliandikwa hivi, ‘’ What a wonderful bird's eye view of our beautiful Mount Kilimanjaro, I was able to capture today February 12th, 2020. I was on a TGFA flight from Nairobi to Dar es Salaam. I have never been this lucky before and I have seen this much snow’’. Chini aliweka over view ya Mlima Kilimanjaro.
Kwenye twitter hii ilichangiwa na watu wengi, lakini Mh Godbless Lema yeye alichangia kwa kuandika maneno haya “That was nice!! I think you also need to take a picture of the real situation of the country at the moment.The political situation of this country need your camera too.We need your voice Sir to work like your iPhone’’. Baada ya kusoma mchango wa Mh Lema pamoja na kuwa nimejibu comment yake, lakini nikapata kichwa cha kuandaa makala fupi ya ‘’UPINZANI TANZANIA HISTORIA INAWAHUKUMU’’.
Ndugu zangu inawezekana wazo la Mh Lema ni jema. Lakini historia inaonyesha upinzani wa Tanzania hauujawahi kumkubari Rais aliyemadarakani. Niwakumbushe tu, Mzee Mwinyi alitukanwa sana na NCCR- Mageuzi ikiongozwa na Mzee MREMA. Mnaokumbuka swala la CHAVUDA mtakubaliana na mimi juu ya Mrema alivyolisaliti Baraza la mawaziri. Lakini leo sizungumzii doctrine of ministerial responsibility.
Baada ya uchaguzi Mrema na wenzake walianza kumtukana mzee Mkapa. Walisema ameficha pesa, ameuza viwanda na mambo kedekede. Enzi hizo kulikuwa na CUF ya Ngangari na NCCR-Mageuzi kabla haijafanyiwa substation na CHADEMA. CUF walijaribu kwenda nje baada yam zee Mwinyi kuwagomea juu ya hoja yao ya yeye kuwakutanisha na Mh Mkapa. Wakati CUF wakizunguka nje ya nchi, mwaka 2001 Mzee Mkapa alitoa kauli nzito, alisema ‘’WABWEKE NJE AU WABWEKE NDANI, SERIKALI ILIYO MADARAKANI NI ILEILE’’. Alitoa kauli hiyo baada ya baadhi ya nchi kutaka kuingilia mambo ya ndani ya nchi.
Wapinzani hawa hawa baada ya JK kuwa Rais walimtukana JK matusi yote. JK hakuwajibu bali aliendelea na kazi. Walimpa majina yote, mara dhaifu, Vascow Da Gama nk lakini Kikwete aliendelea kuchapa kazi na wakati mwingine aliwaita kunywa nao chai Ikulu. Wakati JK kiongozi walisema Mh. Mkapa ndiye bora.
Leo JPM anafanya kazi usiku na Mchana, hao hao waliomtukana JK wanasema JK was excellent. Wanataka JK aongee naJPM. Yaani aliyeitwa Dhaifu aongee na JPM. Historia inawafunga. Inaezekana hoja zao ni nzuri, ila kwa kuwa imejengeka Tabia kuwa kila kiongozi anatukanwa awapo madarakani basi wanajikuta wanakosa msaada.
USHAURI: Upinzani uwe na tabia ya kukukubali baadhi ya mambo, lakini yale wanayokosa ufafanuzi wawe wanaomba kibari cha kuonana na PM au Rais. Rais hawezi kukataa kuzungumza na Mh Mbowe akitumia channel nzuri. Waziri mkuu hawezi kataa kumsikiliza Mbowe. Tukiwa na utamaduni huo nchi itaenda na hatutatunishiana misuli.
Na; Elius Ndabila
0768239284
Kwenye twitter hii ilichangiwa na watu wengi, lakini Mh Godbless Lema yeye alichangia kwa kuandika maneno haya “That was nice!! I think you also need to take a picture of the real situation of the country at the moment.The political situation of this country need your camera too.We need your voice Sir to work like your iPhone’’. Baada ya kusoma mchango wa Mh Lema pamoja na kuwa nimejibu comment yake, lakini nikapata kichwa cha kuandaa makala fupi ya ‘’UPINZANI TANZANIA HISTORIA INAWAHUKUMU’’.
Ndugu zangu inawezekana wazo la Mh Lema ni jema. Lakini historia inaonyesha upinzani wa Tanzania hauujawahi kumkubari Rais aliyemadarakani. Niwakumbushe tu, Mzee Mwinyi alitukanwa sana na NCCR- Mageuzi ikiongozwa na Mzee MREMA. Mnaokumbuka swala la CHAVUDA mtakubaliana na mimi juu ya Mrema alivyolisaliti Baraza la mawaziri. Lakini leo sizungumzii doctrine of ministerial responsibility.
Baada ya uchaguzi Mrema na wenzake walianza kumtukana mzee Mkapa. Walisema ameficha pesa, ameuza viwanda na mambo kedekede. Enzi hizo kulikuwa na CUF ya Ngangari na NCCR-Mageuzi kabla haijafanyiwa substation na CHADEMA. CUF walijaribu kwenda nje baada yam zee Mwinyi kuwagomea juu ya hoja yao ya yeye kuwakutanisha na Mh Mkapa. Wakati CUF wakizunguka nje ya nchi, mwaka 2001 Mzee Mkapa alitoa kauli nzito, alisema ‘’WABWEKE NJE AU WABWEKE NDANI, SERIKALI ILIYO MADARAKANI NI ILEILE’’. Alitoa kauli hiyo baada ya baadhi ya nchi kutaka kuingilia mambo ya ndani ya nchi.
Wapinzani hawa hawa baada ya JK kuwa Rais walimtukana JK matusi yote. JK hakuwajibu bali aliendelea na kazi. Walimpa majina yote, mara dhaifu, Vascow Da Gama nk lakini Kikwete aliendelea kuchapa kazi na wakati mwingine aliwaita kunywa nao chai Ikulu. Wakati JK kiongozi walisema Mh. Mkapa ndiye bora.
Leo JPM anafanya kazi usiku na Mchana, hao hao waliomtukana JK wanasema JK was excellent. Wanataka JK aongee naJPM. Yaani aliyeitwa Dhaifu aongee na JPM. Historia inawafunga. Inaezekana hoja zao ni nzuri, ila kwa kuwa imejengeka Tabia kuwa kila kiongozi anatukanwa awapo madarakani basi wanajikuta wanakosa msaada.
USHAURI: Upinzani uwe na tabia ya kukukubali baadhi ya mambo, lakini yale wanayokosa ufafanuzi wawe wanaomba kibari cha kuonana na PM au Rais. Rais hawezi kukataa kuzungumza na Mh Mbowe akitumia channel nzuri. Waziri mkuu hawezi kataa kumsikiliza Mbowe. Tukiwa na utamaduni huo nchi itaenda na hatutatunishiana misuli.
Na; Elius Ndabila
0768239284