nitaendaje mahakamani na ushahidi sina?
Ndio Maana mnaambiwa pigeni kimya...
nitaendaje mahakamani na ushahidi sina?
Mimi naamini kwamba tuliimbishwa kweli na vyombo vya habari wimbo unaosema "EL ni fisadi" na sisi tukauimba bila kujua maana yake.Sio siri kwamba unachokiamini ni matokeo ya unachokisikia hasa kama kitu hicho unakisikia mara kwa mara.Sasa naamini kwamba Lowasa sio fisadi kama tulivyoaminishwa.Nadiriki kusema kwamba hata kama Lowasa ni fisadi,ufisadi wake ni bora kuliko wa wengi walioko CCM.
Kwa nini mmeshindwa kumtetea kwa ID zenu zilizozoeleka badala yake mnatumia zile za akiba?
Acheni unafiki, mbona hamkumhoji Slaa alipoitaja ile orodha maanake alisema ushahidi anao?
Mbona Mbowe aliposema anashangaa fisadi Lowassa yupo mtaani ilhali vibaka wanachomwa moto mlikuwa mnakenua tu?.
Nyie jamaa hata hamueleweki mnachokisimamia ni kipi hasa?
Msitufanye wote wajinga humu mazee.
Lazima mlipe gharama za uropokaji wenu.