Upi hasa ufisadi wa Lowassa?

Upi hasa ufisadi wa Lowassa?

Naminipo

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
846
Reaction score
1,074
Nimekuwa nikijiuliza na kuuliza raia wenzangu wengine bila kupata majibu yaliyonyooka.
Ufisadi wa Lowassa ni upi hasa? Wengine ukiwauliza wanajibu we hujui kila mtu anajua, wengine wanasema hujui Richmond? Wengine wanasema ni tajiri sana yule kaupataje utajiri?

Binafsi naona raia mwenzetu hatendewi haki, ndiyo maana mwenyewe kashasema mwenye ushahidi aende mahakamani vinginevyo nyamaza.

Nami naendelea kujiuliza mtu ambaye ameshadidiwa ufisadi na pande zote chama tawala na upinzani kwa nyakati tofautitofauti kiasi ya kwamba hata mtoto aliyezaliwa miaka 8 imepita sasa labla yupo darasa la pili naye anaaminishwa kuwa Lowassa ni fisadi lakini yupo huru hatuoni hapo kuna tatizo. Mtu ambaye hadi bungeni amekuwa na cheo nyeti tu, hivi nchi hii wenye sifa mbaya ndiyo tunawapa vyeo au kinyume chake.

Naelekea kuamini Lowassa anaonewa kwasababu maalum. Na kwakuwa sasa ni mgombea kupitia upinzani basi ndiyo itakuwa shida kubwa. Wanaomnanga wajitokeze kutuelekeza nini hasa ufisadi wake?

Watu wengi wameimbishwa wimbo na kukubali kuuimba bila kujua maana ya maneno ya wimbo. Sasa tutafakari vizuri siasa za namna hii.
 
Na kwa hali ya tanzania katika miaka 8 iliyopita lowasa hakuwa na cheo cha maamuzi. Hivyo hakufanya ufisadi wowote. Tunalishwa tuhuma ya Richmond isiyothibitidhwa.
 
Kwa nini mmeshindwa kumtetea kwa ID zenu zilizozoeleka badala yake mnatumia zile za akiba?

Acheni unafiki, mbona hamkumhoji Slaa alipoitaja ile orodha maanake alisema ushahidi anao?

Mbona Mbowe aliposema anashangaa fisadi Lowassa yupo mtaani ilhali vibaka wanachomwa moto mlikuwa mnakenua tu?.

Nyie jamaa hata hamueleweki mnachokisimamia ni kipi hasa?

Msitufanye wote wajinga humu mazee.

Lazima mlipe gharama za uropokaji wenu.
 
Lowassa ni Msafi Kama Ni Richmond Yeye Anatamka Bila Kumungunya Maneno " Boss Wake Alitoa order Mchakato Uendelee" , So

Richmond So far "Ni Boss Wake", Tume ya Mwakyembe ya Uchunguzi Inasema Iliona Isiingie Ndani Zaidi Kwa Maana Serikali ya CCM

Ilikuwa Inaenda Kuanguka.Tunambiwa Takukuru Walifanya Uchunguzi Lakini Waligundua Hapakuwepo na Wrong Doing na Ndio

Maana File na Mjadala Vilifungwa Rasmi.

NB: Kwa Nini Wanataka Kutuaminisha Kuwa Edward Ni Richmond, Hawataki Kwenda Kuoji Aliyekuwa Boss Wake Edward Ili Ajibu

Tuhuma. Mpaka Ikulu Itoe Tamko Kuhusu Tuhuma Hizi, Vinginevyo Richmond Siyo Issue ya Lowassa.

Hizi Nzito, Kwa Maana Kwa Zaidi ya Miaka Saba Watanzania Wamemwonea Sana Lowassa. Hii Inatupelekea Kuamini Ya Kwamba

Mwasisis Wa Richmond Ndie Escrow:


RICHMOND=ESCROW, Chini ya CCM.
 
chadema walimtaja lowassa katika ile list of shame kutokana na kashfa ya richmond pekee c zaidi ya hapo swali la kujiuliza ni nani aliweza ku verify ile report ya mwakyembe kama ilikuwa na ukweli kiasi gani au mybe kulikuwa na chuki binafsi au kulikuwa na influence kutoka ngazi za juu ? cjawahi kuona hukumu isiyokuwa na natural justice lowassa anasema ajawai kuitwa na kamati ya mwakyembe kwa ajili ya interrogation japo ni haki ya msingi kuhojiwa kesi ya richmont aina tofauti na ya escrow mbona leo pinda ajaitwa fisadi ? au kwa vile lowassa alifanya maamuzi magumu ya kujiudhulu kwa kulinda heshima ya serikali na chama? pinda hakufanya hvyo? serikali kupitia ikulu imeweza kuwasafisha wezi wote wa scandal ya escrow bt wameshindwa kumsafisha lowassa japo hakuna file lake la wizi wa richmond kuanzia mahakama ya kijiji mpaka mahakama kuu
 
Mimi naamini kwamba tuliimbishwa kweli na vyombo vya habari wimbo unaosema "EL ni fisadi" na sisi tukauimba bila kujua maana yake.Sio siri kwamba unachokiamini ni matokeo ya unachokisikia hasa kama kitu hicho unakisikia mara kwa mara.Sasa naamini kwamba Lowasa sio fisadi kama tulivyoaminishwa.Nadiriki kusema kwamba hata kama Lowasa ni fisadi,ufisadi wake ni bora kuliko wa wengi walioko CCM.
Nimekuwa nikijiuliza na kuuliza raia wenzangu wengine bila kupata majibu yaliyonyooka.
Ufisadi wa Lowassa ni upi hasa? Wengine ukiwauliza wanajibu we hujui kila mtu anajua, wengine wanasema hujui Richmond? Wengine wanasema ni tajiri sana yule kaupataje utajiri?

Binafsi naona raia mwenzetu hatendewi haki, ndiyo maana mwenyewe kashasema mwenye ushahidi aende mahakamani vinginevyo nyamaza.

Nami naendelea kujiuliza mtu ambaye ameshadidiwa ufisadi na pande zote chama tawala na upinzani kwa nyakati tofautitofauti kiasi ya kwamba hata mtoto aliyezaliwa miaka 8 imepita sasa labla yupo darasa la pili naye anaaminishwa kuwa Lowassa ni fisadi lakini yupo huru hatuoni hapo kuna tatizo. Mtu ambaye hadi bungeni amekuwa na cheo nyeti tu, hivi nchi hii wenye sifa mbaya ndiyo tunawapa vyeo au kinyume chake.

Naelekea kuamini Lowassa anaonewa kwasababu maalum. Na kwakuwa sasa ni mgombea kupitia upinzani basi ndiyo itakuwa shida kubwa. Wanaomnanga wajitokeze kutuelekeza nini hasa ufisadi wake?

Watu wengi wameimbishwa wimbo na kukubali kuuimba bila kujua maana ya maneno ya wimbo. Sasa tutafakari vizuri siasa za namna hii.
 
Mkuu hakuna mtu mwenye jeuri ya kula pesa ya SIRIKALI mwenyewe......Mh.Edo Msafi.....
 
Hakuna Cha Fisadi Wala Nini, Ule Ni ugomvi na Majungu Ndani ya Chama Ndio Umewafikisha Hapo.
 
Hayo yalikuwa majungu yaliyopikwa baada ya kuona mkuu anafunikwa kiutendaji na pm wake
 
Sasa Dr Slaa alikuwa na polisi ya kumkamata Lowassa? Tumia akili

Uliwahi kuona akiitwa hata tume ya maadili kuhojiwa?

Kwani Slaa akisema ndio itimisho na uthibisho kwamba mtu ni fisadi?

Mbona Slaa alisema Kikwete ni fisadi kwenye list of shame mbona hujamwita Kikwete fisadi?

Acha kulazimisha agenda za kitoto
 
Baada ya Septemba mosi 2015 NANI ATAENDELEA KUMWITA LOWASA FISADI BILA USHAHIDI?
Sheria ya kutosema uongo mitandaoni itasemaje?
 
Back
Top Bottom