Upendo nilionao kwa simu za Nokia

Upendo nilionao kwa simu za Nokia

God knows

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2011
Posts
276
Reaction score
173
Mwanaume utanashati bwana, na baadhi ya gadgets ambazo mwanaume yeyote anayethamini mwonekano wake wa nje anatakiwa kuwa nazo ni saa na simu.

Binafsi nathamini na napenda nionekane unique and premium. Nitakula hata nyasi ili nihakikishe Napata kitu roho inapenda. Sijui ni addiction au nini, ila kuna muda nikiwa sina simu (labda imeibiwa kwa mfano), najisikia homa. Kurudi kwenye kitochi kwa sababu sina hela haijawahi kuwa option kwangu na nitahangaika mpaka niipate simu nyingine ya gharama ile ile au ya juu Zaidi ya ile.

Back to topic

Niliacha kutumia simu za Android 2014. Nilikuwa nakasirishwa sana na hii kitu “Unfortunately, XXXXXX has stopped.” Crushing ya apps ilikuwa inatokea mara nyingi sana hadi nikaapa kuhama na kutokurudi tena android.
1.jpg


Swali likaja, nihamie wapi?

Blackberry? Hapana. Sijawahi kuipenda simu hii Maisha yangu yote.

iPhone naipenda ila kiwango changu cha kipato kwa miaka ile kilikuwa kidogo sana. Nilitakiwa niwekeze hela kwa miezi sio chini ya minne ili niweze kununua iPhone mpya. Uvumilivu ungenishinda.

Windows Phone? Perfect. Bei ilikuwa inaruhusu. Angalau nilikuwa na uwezo wa kuspend TZS 600,000 na nikapata simu nzuri ambayo haicrash apps, performance nzuri na mwonekano premium, huku moyoni nikijisemea kwamba, kipato kikiongezeka nitahamia iPhone na nitabaki huko milele. Simu kama hii:
910c4f51-3602-4717-9bcb-2d03ceb4adb3.jpg


Microsoft walikuwa wananivuruga kwa sababu walikuwa wanatoa simu mpya kila mwaka which looks better than the previous. Ili kwenda nao sawa, I had to buy every new model whenever it is released and sell the previous one.

Nilivunjika moyo baada ya kusikia Microsoft kaacha kutoa simu mpya za Lumia. Simu ya mwisho kuitoa ilikuwa Microsoft Lumia 650 iliyotoka Feb, 2016 na mimi ndio niliyonunua na kuitumia kwa mara ya mwisho. Nilipata maumivu kama vile nimeachwa. 🙁🙁🙁🙁🙁

So I was like, is it the end of Lumia? Is Nokia no longer?

Muda huu nimepata ahueni baada ya kuona Nokia wamerudi tena sokoni (vitochi + smartphone).

Kitochi image.jpg


Wamerudi na smartphones zikiwa na android. Siipendi android ila I had to buy one for the love I had for Microsoft Lumia.

Washatoa matoleo mengi ya smartphones kama Nokia 3, 5, 6 na muda huu wanaitangaza Nokia 8. Sizioni madukani hapa Tanzania, sijui kwa nini?

Niliagiza hii niliyonayo hapa mkononi (Nokia 6) kutoka nje ya Tanzania na ilinifikia kama mwezi mmoja uliopita kwa gharama ya TZS 650,000. Kama wiki moja mbele, nikaja kuiona Jumia ikiwa inauzwa 1.2M. Ilikuja ikiwa na earphones zile zile za nokia, usb cable na charger yake kama unavyoona hapo chini.

Capture.PNG


Quick specs zake ni hizi:

Snapdragon 430 (Octa Core, Cortex A-53)

3 GB RAM

5.5” 1080p IPS LCD Screen

Adreno 505 GPU

32 GB Internal Storage

Dual Sim / Hybrid MicroSD Card Slot

16 MP Rear / 8 MP Front Camera Auto Focus

3000 mAh Battery

Fingerprint Scanner / NFC / Dolby Atmos



Nokia_6-color_variant-Matte_Black.jpg



IMG_0060.JPG


It looks premium when you hold it.

Ikichajiwa, inakaa na charge all day long. Yaani unaweza kuichaji usiku, ukaja nayo kazini, ukatumia siku nzima na ukarudi nayo nyumbani ikiwa haijazima.

What I hate: haina fast charging. Inatumia like 2 hrs to get fully charged.

Karibuni kwa majadiliano.
 
Niliagiza hii niliyonayo hapa mkononi (Nokia 6) kutoka nje ya Tanzania na ilinifikia kama mwezi mmoja uliopita kwa gharama ya TZS 650 said:
Naomba kujua jinsi ya kuagiza mkuu,
Mimi nazikubali sana Nokia
 
NOKIA ZILIPENDWA, IMESHAKUFA.. NI NGUMU SANA KUWAHAMISHA WATU WA SAMSUNG, IPHONE N.K
 
Kumbe microsoft walistop kutoa lumia maana nilikuwa nawafatilia na kupenda simu zao ila kipato hakikuruhusu.

Ila lazima nije kudaka hivi vitu.
 
God knows umeandika kuhusu kuagiza kwa 650,000/=, nimekuwa nikijaribu kuwatafuta watu wanaoweza kunifikishia hii kitu hapa bongo bila mafanikio.

Nataka kujua kama unaweza kusaidia jinsi ya kufanikisha hili swala mkuu.
 
God knows umeandika kuhusu kuagiza kwa 650,000/=, nimekuwa nikijaribu kuwatafuta watu wanaoweza kunifikishia hii kitu hapa bongo bila mafanikio.

Nataka kujua kama unaweza kusaidia jinsi ya kufanikisha hili swala mkuu.

Mkuu naogopa kushiriki kwenye huu mchakato wa kuagiza. Sina uzoefu sana. Kuna vitu nilishawahi agiza kipindi cha nyuma na vikapotea.

Kuna mtu humu huwa anaagiza na unamlipa commission kidogo. Unaweza kumtumia huyo kuagiza. Ila pia zipatikana Jumia.
upload_2017-10-10_13-20-41.png
 
Mkuu naogopa kushiriki kwenye huu mchakato wa kuagiza. Sina uzoefu sana. Kuna vitu nilishawahi agiza kipindi cha nyuma na vikapotea.

Kuna mtu humu huwa anaagiza na unamlipa commission kidogo. Unaweza kumtumia huyo kuagiza. Ila pia zipatikana Jumia.
View attachment 606200

Unajua kwa 650,000 na hiyo 987,000 unaokoa around 340,000, si haba kwa maisha yalivyobana now, hata nikitoa 700,000 bado ni fair.

Sema ubaya mmoja, hizi product za kuagiza kama ebay na amazon zinakuwaga mchina sometimes.

Usijali mkuu, ngoja nitafute solution nyingine.
 
Unajua kwa 650,000 na hiyo 987,000 unaokoa around 340,000, si haba kwa maisha yalivyobana now, hata nikitoa 700,000 bado ni fair.

Sema ubaya mmoja, hizi product za kuagiza kama ebay na amazon zinakuwaga mchina sometimes.

Usijali mkuu, ngoja nitafute solution nyingine.
jaribu kutumia service ya Mwl.RCT nimeitumia mimi kama unapanga vizuri bidhaa zako ni rahisi.

hizi Nokia mpya bei rahisi unazipata UAE kama ni abudhabi, dubai, etc

ukiconvert kwa tsh ni kama 489,000 kwa Nokia 6
 
jaribu kutumia service ya Mwl.RCT nimeitumia mimi kama unapanga vizuri bidhaa zako ni rahisi.

hizi Nokia mpya bei rahisi unazipata UAE kama ni abudhabi, dubai, etc

ukiconvert kwa tsh ni kama 489,000 kwa Nokia 6

Okay, hapo kwenye kupanga vizuri ndo sijakuelewa.
 
Okay, hapo kwenye kupanga vizuri ndo sijakuelewa.
kununua bidhaa nyingi toka muuzaji mmoja ili ku share shipping na gharama za nyengine za kuletewa.

mfano gharama ya kuileta Tanzania ni 50,000 ukiamua unaweza ukatoa mwenyewe, au mnaweza mkanunua watu wawili simu then mkashare gharama ya shipping hapa gharama inapungua.
 
kununua bidhaa nyingi toka muuzaji mmoja ili ku share shipping na gharama za nyengine za kuletewa.

mfano gharama ya kuileta Tanzania ni 50,000 ukiamua unaweza ukatoa mwenyewe, au mnaweza mkanunua watu wawili simu then mkashare gharama ya shipping hapa gharama inapungua.

Nimekuelewa mkuu, ngoja niwasiliane na jamaa nione.

Naona bei iko favorable hata kwa kununua mmoja.
 
Back
Top Bottom