Mzee wa Gumzo
Senior Member
- Apr 21, 2008
- 197
- 5
Wakati taarifa za awali hapo asubuhi zilitanabaisha kuwa mtihani wa geography uliokuwa ufanyike leo asubuhi ulitangazwa kufutwa baada ya kuvujishwa kwa makusudi, taarifa za uhakika zimejulisha kuwa mtihani wa geography ulifanyika kama ilivyopangwa isipokuwa ulisambazwa mtihani mwingine hivyo kuwaduwaza wanafunzi ambao walikuwa na uhakika wa kuvuna wasichokipanda(A).
Taarifa zinadhibitisha kuwa kwasasa mitihani inasambazwa usiku usiku kuanzia saa tisa na kwa kuwa mitihani yote imevujishwa, mitihani mingine imesambazwa kusudi ratiba iendelee kama kawaida.Hata hivyo wizara bado inakataa kuwa mitihani mingine imevujishwa.Mtihani wa history,physics,chemisty imesambaa kila kona za miji na vitongoji.
Taarifa za kuaminika zinaeleza kuwa kuvuja huku kwa mitihani kulisukwa na wahusika ambao walitaka kuiaibisha serikali kutokana na kukataa au kushindwa kutatua malalamiko ya waalimu.Wakati tunajiuliza kwanini mitihani ivuje kwa kiwango hiki,tarifa ni kwamba huu ni mpango maalumu na ulikuwa na kamati ya kuhakikisha kila mtihani unavujishwa na kusambazwa.
Kilichopo sasa ni kujaribu kupambana na wanafunzi wenye mitihani hiyo mitaani na kusambaza mitihani mipya usiku usiku kwenye vituo na shule lakini ukweli ni kuwa wahusika wakubwa wa hujuma hii wapo kwenye ofisi hizohizo za mabosi wa WIZARA NA NECTA
Taarifa zinadhibitisha kuwa kwasasa mitihani inasambazwa usiku usiku kuanzia saa tisa na kwa kuwa mitihani yote imevujishwa, mitihani mingine imesambazwa kusudi ratiba iendelee kama kawaida.Hata hivyo wizara bado inakataa kuwa mitihani mingine imevujishwa.Mtihani wa history,physics,chemisty imesambaa kila kona za miji na vitongoji.
Taarifa za kuaminika zinaeleza kuwa kuvuja huku kwa mitihani kulisukwa na wahusika ambao walitaka kuiaibisha serikali kutokana na kukataa au kushindwa kutatua malalamiko ya waalimu.Wakati tunajiuliza kwanini mitihani ivuje kwa kiwango hiki,tarifa ni kwamba huu ni mpango maalumu na ulikuwa na kamati ya kuhakikisha kila mtihani unavujishwa na kusambazwa.
Kilichopo sasa ni kujaribu kupambana na wanafunzi wenye mitihani hiyo mitaani na kusambaza mitihani mipya usiku usiku kwenye vituo na shule lakini ukweli ni kuwa wahusika wakubwa wa hujuma hii wapo kwenye ofisi hizohizo za mabosi wa WIZARA NA NECTA