Kifaurongo
JF-Expert Member
- Jan 18, 2010
- 4,287
- 2,437
Katika kutembea miji mbali mbali nchini nimeshuhudia kupanuka kwa kwa kasi kwa miji yetu.
Halmashauri zetu zimekuwa zikiwanyang'anya wakulima maeneo yaliyokuwa mashamba, kuyapima na kuyageza kuwa makazi. Kwa kigezo cha kila mkilima mwenye shamba, kugaiwa kiwanja.
Sera na sheria hii ya kugeuza mashamba ya wakulima kuwa makazi kwa mkulima kupewa kiwanja ktk eneo husika nimegundua inamakosa makubwa sana, sababu inaua kilimo na inasababisha kubsdilisha mfumo wa maisha ya waliokuwa wakitegemewa kilimo kama kazi ktk maisha yao kushindwa kujua cha kufanya.
Mawazo yangu ninadhani serikali inapoamuwa kupanua miji kwa kupima viwanja maeneo ya wakulima, ingekuwa vema wafidiwe maeneo mengine kwa ajili ya kuendeleza kilimo chao kuliko kuwaacha wakihangaika na jinsi ya kumudu maisha yao bila kilimo. Kuliko shida wanayopata ya jinsi ya kupata pesa za kununua chakula.
Halmashauri zetu zimekuwa zikiwanyang'anya wakulima maeneo yaliyokuwa mashamba, kuyapima na kuyageza kuwa makazi. Kwa kigezo cha kila mkilima mwenye shamba, kugaiwa kiwanja.
Sera na sheria hii ya kugeuza mashamba ya wakulima kuwa makazi kwa mkulima kupewa kiwanja ktk eneo husika nimegundua inamakosa makubwa sana, sababu inaua kilimo na inasababisha kubsdilisha mfumo wa maisha ya waliokuwa wakitegemewa kilimo kama kazi ktk maisha yao kushindwa kujua cha kufanya.
Mawazo yangu ninadhani serikali inapoamuwa kupanua miji kwa kupima viwanja maeneo ya wakulima, ingekuwa vema wafidiwe maeneo mengine kwa ajili ya kuendeleza kilimo chao kuliko kuwaacha wakihangaika na jinsi ya kumudu maisha yao bila kilimo. Kuliko shida wanayopata ya jinsi ya kupata pesa za kununua chakula.