Uonevu wa hali ya juu wa refa dhidi ya timu ya singida fountain gate

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
386
765
Jana nimeufuatilia mtanange kati ya timu ya Simba dhidi ya Singida Fountain Gate kombe la Mapinduzi 2024. Uonevu wa refa dhidi ya timu ya Singida unatakiwa kukemewa kwa kiasi kikubwa. Sababu zangu kuhusu uonevu huo ni kama ifuatavyo:-

(1) Baada ya muda wa dakika 90 kuisha refa aliongeza dakika 8 lakini hizi dakika za nyongeza mpira ulichezwa kwa muda wa dakika 11 bila Refa kupuliza kipenga cha kumaliza mpira.

(2) Kona ulioruhusiwa na Refa mpira ulikamatwa na kipa nje ya mstari na hakuna mchezaji wa Singida aliyeupiga mpira huo nje na kipa akaukamata nje ya mstari ni dhahiri mpira huo haukustahili kuwa kona. Huo mpira ulitakiwa upigwe kuelekeza kwa timu pinzani ya Simba.

(3) Huu ni ushauri kwa Timu ya Singida. Wakati wa kupiga penati mnaombwa kuchagua wachezaji maakini. Ile penati aliyopiga Kagere ilikuwa ni penati ya hovyo ambayo haijapa kutokea katika historia ya mpira. Jifunzeni kupiga penati.
 
Mambo yanabadilika ukijangusha kupoteza muda zitafidiwa dk zako ili upate haki yako ya muda je hizo dk zilizozidi kwanini singida wasiongeze goli ni faida kwa timu zote mbili au wao walisimama!
 
IMG-20240111-WA0964.jpg
 
Ushauri kwamba Singida FG wawe wanachagua wapigaji wazuri wa penati.
Pia uishauri timu yako nao wawe wanachagua wapigaji wa zuri wa penati.
Maana hata na wao kiliwakuta kama hiki kule Tanga.
 
Jana nimeufuatilia mtanange kati ya timu ya Simba dhidi ya Singida Fountain Gate kombe la Mapinduzi 2024. Uonevu wa refa dhidi ya timu ya Singida unatakiwa kukemewa kwa kiasi kikubwa. Sababu zangu kuhusu uonevu huo ni kama ifuatavyo:-
(1) Baada ya muda wa dakika 90 kuisha refa aliongeza dakika 8 lakini hizi dakika za nyongeza mpira ulichezwa kwa muda wa dakika 11 bila Refa kupuliza kipenga cha kumaliza mpira.
(2) Kona ulioruhusiwa na Refa mpira ulikamatwa na kipa nje ya mstari na hakuna mchezaji wa Singida aliyeupiga mpira huo nje na kipa akaukamata nje ya mstari ni dhahiri mpira huo haukustahili kuwa kona. Huo mpira ulitakiwa upigwe kuelekeza kwa timu pinzani ya Simba.
(3) Huu ni ushauri kwa Timu ya Singida. Wakati wa kupiga penati mnaombwa kuchagua wachezaji maakini. Ile penati aliyopiga Kagere ilikuwa ni penati ya hovyo ambayo haijapa kutokea katika historia ya mpira. Jifunzeni kupiga penati.
Kombe la mapinduzi ni michuano ya CCM, wao uchakachuaji wa matokeo ni shehemu ya utamaduni wao
 
Back
Top Bottom