Uonevu huu wa Jeshi la Polisi umevuka mipaka

bachelor sugu

JF-Expert Member
Jan 30, 2018
2,689
3,641
Habari za mchana Wakuu,

Ama kwa kweli nchi yetu tumefilisika kila kitu yaani kuanzia viongozi,skills za uongozi,pesa,hadi roho za huruma nazo tumefilisika zaidi kwa hawa viongoz/watawala wetu.

Kuna operation inayoendeshwa na jeshi la polisi hapa wilayani Kilosa ya kukamata pikipiki na pale unapobainika kuwa na kosa lolote basi kwanza unatulizwa mahabusu kisha taratibu za kupelekwa mahakamani zinafuata.

Kibaya zaidi hata ukiwa na kosa moja FAINI YAKE ni shilingi za Kitanzania 300,000/=(Laki Tatu tu) na ukiwa na makosa yote bei ni hiyo hiyo.Uonevu huo unaenda mbali zaidi kuwa ukiweza kulipa faini hiyo unahukumiwa MWEZI MMOJA JELA na ukishindwa unahukumiwa MIEZI SABA(7) JELA.

Hali imekuwa mbaya zaidi kwani mahabusu ya Polisi imejaa,Mahabusu ya Gereza imejaa mpaka wengine sasa hv wanahamishiwa Mahabusu zilizopo ktk vituo vingine vya Polisi vya wilaya hii.

Hv kweli nchi imekosa vyanzo vingine vya mapato mpaka kufikia sasa kuamua kuwa wanyang'anyi wa jasho la wananchi wake??,Lengo hasa ni nini kuwarudisha vijana wetu katika kazi zile haramu za kukaba na wizi?

Kwani watanzania tumemkosea nini huyu mtawala wetu ambaye tunaamini AMRI hizi zote ni kutoka kwake???

Dah hali ni mbaya kwa kweli jamani na tunakoelekea tusije hata siku moja kupoteza muda kumtafuta mchawi wetu maana uvumilivu nao una mwisho.

Ee M/Mungu tutupie jicho lako la huruma watanzania tunaangamia.
 
mahakama za chini kwa tanzania ni kama kangaroo courts, hukumu/faini kwa makosa ya barabarani zipo kwa mujibu wa sheria na sio mkuu wa polisi kujiamulia tu kuwa sasa faini ni laki tatu. lakini mambo kama haya yawe yanawapa akili watanzania mmelemaa sana na uoga na uzembeuzembe!
 
Habari za mchana Wakuu,

Ama kwa kweli nchi yetu tumefilisika kila kitu yaani kuanzia viongozi,skills za uongozi,pesa,hadi roho za huruma nazo tumefilisika zaidi kwa hawa viongoz/watawala wetu.

Kuna operation inayoendeshwa na jeshi la polisi hapa wilayani Kilosa ya kukamata pikipiki na pale unapobainika kuwa na kosa lolote basi kwanza unatulizwa mahabusu kisha taratibu za kupelekwa mahakamani zinafuata.

Kibaya zaidi hata ukiwa na kosa moja FAINI YAKE ni shilingi za Kitanzania 300,000/=(Laki Tatu tu) na ukiwa na makosa yote bei ni hiyo hiyo.Uonevu huo unaenda mbali zaidi kuwa ukiweza kulipa faini hiyo unahukumiwa MWEZI MMOJA JELA na ukishindwa unahukumiwa MIEZI SABA(7) JELA.

Hali imekuwa mbaya zaidi kwani mahabusu ya Polisi imejaa,Mahabusu ya Gereza imejaa mpaka wengine sasa hv wanahamishiwa Mahabusu zilizopo ktk vituo vingine vya Polisi vya wilaya hii.

Hv kweli nchi imekosa vyanzo vingine vya mapato mpaka kufikia sasa kuamua kuwa wanyang'anyi wa jasho la wananchi wake??,Lengo hasa ni nini kuwarudisha vijana wetu katika kazi zile haramu za kukaba na wizi?

Kwani watanzania tumemkosea nini huyu mtawala wetu ambaye tunaamini AMRI hizi zote ni kutoka kwake???

Dah hali ni mbaya kwa kweli jamani na tunakoelekea tusije hata siku moja kupoteza muda kumtafuta mchawi wetu maana uvumilivu nao una mwisho.

Ee M/Mungu tutupie jicho lako la huruma watanzania tunaangamia.
Mpigieni simu lugola... Alishasisitiza jeshi LA polisi liache kuonea na kunyanyasa wananchi Bali lifanye Kazi Kwa Haki na sheria
 
Mkuu kweli tuwekee namba yake tujaribu kumtafuta aisee maana this is too much.Kama vp itupie PM mi naumia kuna wadogo wa mtaani hapa wako ndani ndo naangalia namna ya kuweza kuwaokoa
Mpigieni simu lugola... Alishasisitiza jeshi LA polisi liache kuonea na kunyanyasa wananchi Bali lifanye Kazi Kwa Haki na sheria
 
Mkuu inasemekana Wakulugenzi wa halmashauli kila wilaya kuna senti wanatakiwa kurejesha kwa Mtawala hivyo kwa wilaya ambazo hazina vyanzo vya mapato hutumia njia mbadala kunusuru kibarua.

Inabidi wananchi tuwe makini na uonevu kama huu,
Yaani basi kubwa la abilia lenye siti zaidi ya 65 faini yake iwe ndogo kwa bodaboda ambayo ina siti moja faini iwe laki tatu.

Kweli namba inasomeka!
 
Kinacho SIKITISHA zaidi, ni kuna watu wanaitetea serikali kama roho ziwatoke, hawaoni huu uonevu wote unaofanyika. Leo wafuasi wa CUF huko lindi, kujumlisha VIONGOZI wao (Mbunge Selemani Bungara "Bwege" wamewekwa rumande bila sababu, baada ya jana kufunguliwa kwa kampeni za uchaguzi).

Zitto
 
Mkuu maana ya uonevu bila shaka unaijua vizuri coz Uonevu ni hali ya kutendewa jambo kinyume na na haki iliyowekwa kisheria.

Faini ya shilingi 300,000/= kwa kosa moja la barabarani ipo sehemu gani?

Iweje mtu akilipa fine awekwe jela mwezi mmoja.

Labda km ww sio mtanzania ndo hautauona huo uonevu
Huo Uonevu uko wapi? Embu fafanua kama ukipenda, unaelewa maana ya neno uonevu?
 
Sasa hapa Mkuu si ndo huu tunaita unyang'anyi wa watawala?

Hv lengo lao ni kutufanya tujute kwa nn tuliwapa hiyo nafasi au??
Mkuu inasemekana Wakulugenzi wa halmashauli kila wilaya kuna senti wanatakiwa kurejesha kwa Mtawala hivyo kwa wilaya ambazo hazina vyanzo vya mapato hutumia njia mbadala kunusuru kibarua.

Inabidi wananchi tuwe makini na uonevu kama huu,
Yaani basi kubwa la abilia lenye siti zaidi ya 65 faini yake iwe ndogo kwa bodaboda ambayo ina siti moja faini iwe laki tatu.

Kweli namba inasomeka!
 
Mkuu maana ya uonevu bila shaka unaijua vizuri coz Uonevu ni hali ya kutendewa jambo kinyume na na haki iliyowekwa kisheria.

Faini ya shilingi 300,000/= kwa kosa moja la barabarani ipo sehemu gani?

Iweje mtu akilipa fine awekwe jela mwezi mmoja.

Labda km ww sio mtanzania ndo hautauona huo uonevu


Sasa kama kosa halipo kisheria mbona mmesema anapekwa Mahakamani? Mahakama kazi yake ni ipi?
 
Mkuu 2015 nilikuwa msimamizi mkuu sehemu flani ambayo ilikuwa ikiaminika kuwa ni ngome ya upinzani ila baada ya kumaliza kupiga kura tulipoanza kuhesabu nilichoka mpaka nikapata hasira baba ubaya aliongoza mpaka nikaacha kuhesabu na kumuachia msaidizi wangu.

Yaani sometym nasemaga wacha atunyooshe tu ila roho ya ubinadaamu hunijia ktk majanga km haya huwa nawaonea huruma wanaotaabika licha ya kwamba inawezekana ndio waliotufikisha hapa
Ni sawa kwani hizo ndio Sera za ccm kuwajali wanyonge.mliiipenda wenyewe ndiindii chaguo lenu. Wenyewe ndindiii isomeni namba na bado
 
Back
Top Bottom