Kuna wazandiki huwa nawashangaa wanavyoponda pombe. Pombe haina madhara kama wanafiki wanavyotuaminisha. Pombe ni nzuri ukinywa kistaarabu, ina faida lukuki, ukibisha muulize Albert Chalamila.
Tafiti zinasema kuwa beer zinasaidia kujilinda na magonjwa ya moyo. Kama mnavyojua magonjwa ya moyo yanaondoa watu kimya kimya hivyo mimi nawashauri tunywe beer kujilinda na magonjwa ya moyo.
Hata Biblia inasisitiza tunywe pombe tufurahie, na mkituona tunakunywa pombe msitukwaze.
Too much of anything is bad, but too much good whiskey is barely enough
Tafiti zinasema kuwa beer zinasaidia kujilinda na magonjwa ya moyo. Kama mnavyojua magonjwa ya moyo yanaondoa watu kimya kimya hivyo mimi nawashauri tunywe beer kujilinda na magonjwa ya moyo.
Hata Biblia inasisitiza tunywe pombe tufurahie, na mkituona tunakunywa pombe msitukwaze.
Too much of anything is bad, but too much good whiskey is barely enough
- Tunachokijua
- Bia ni kinywaji kilichoanza kutumika duniani tangu miaka ya zamani sana.
Ingawa watu huona bia sio kinywaji chenye faida kwenye lishe, huwa na virutubisho vingi vinavyofaa kwa afya ya binadamu.
Baadhi ya virutubishoi vinavyopatikana kwenye bia ni calcium, madini chuma, magnesium, manganese, silicon, selenium, potassium na zinc. Aidha, huwa na mkusanyiko wa aina mbalimbali za vitamini ikiwemo vitamini A, E, D, K, B2, B3, B5, B6 pamoja na folate.
Bia ina faida zozote kwenye afya ya moyo?
Baadhi ya tafiti zinaonesha kuwa unywaji mdogo wa bia unaweza kupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo.
Utafiti wa mwaka 2020 unahitimisha kuwa watu wanaotumia bia kwa viwango vya wastani huwa na aina nzuri ya mafuta kwenye mishipa ya damu (HDL) pamoja na mishipa ya damu huwa na afya bora.
Utafiti wenye kichwa cha habari "Effects of moderate beer consumption on health and disease: A consensus document" wa G.de Gaetano et al (2016) unaweka bayana kuwa unywaji wa kiwango kidogo cha bia hupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo na mfumo wa damu.
Hata hivyo, utafiti huu unasisitiza kuwa kiwango cha kawaida kinachofaa kwa afya ya moyo ni bia yenye kiwango cha pombe kisichozidi 5%, ambapo mwanamke anapaswa kunywa wastani wa chupa 1 yenye mililita 330 huku mwanaume akiruhusiwa kunywa mililita 660, mara mbili zaidi ya kiasi anachopaswa kutumia mwanamke.
Pamoja na uwepo wa faida hizi, madaktari wengi huogopa kushauri wagonjwa kutumia bia kwa kuhofia unywaji mkubwa unaoweza kuwa hatari wa afya, hivyo kusababisha matatizo makubwa kwa mnywaji.
Haya yanathibitishwa na utafiti wa Norman M. Kaplan et al (2000) wenye kichwa cha habari "Nutritional and Health Benefits of Beer". Utafiti huu unasisitiza haja ya madaktari kutoa maana sahihi ya "unywaji mdogo/wa kiasi" wa bia kama wastani wa chupa 1 kwa wanawake na chupa 2 kwa wanawake kwa siku.
Madhara ya pombe
kwa upande mwingine, unywaji mkubwa wa pombe husababisha madhara makubwa kwa afya. Taasisi ya afya ya Johns Hopkins, baadhi ya matatizo ni kuongeza shinikizo la damu (presha), magonjwa ya moyo na kiharusi.
Aidha, husababisha ongezeko kubwa la uzito wa mwili linaloweza kuwa chanzo cha magonjwa sugu mfano kisukari.
Kwa mujibu wa Kituo cha Udhibiti na Kinga ya Magonjwa (CDC), madhara ya muda mrefu ya unywaji mkubwa wa pombe ni kusababisha ugonjwa wa ini, matatizo kwenye mfumo wa chakula na saratani.