Unyama siyo unyama

Unyama siyo unyama

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
12,210
Reaction score
23,255
Simba kula binadam MSITUNI ni unyama, Lakini Simba huyo kuuliwa na binadam MSITUNI Siyo-Unyama.

Bomu kurushwa Vitani ni Ushujaa, lakini Bomu kurusha mochwari ni Ufala.

Kutoa msaada siyo unyama, lakini kutumia msaada huo uliopewa kumuumiza mtoaji ni Unyama

Jeshi la polisi ni kazi yenye nidhamu siyo genge la waharifu waliovaa sare.

Misingi ya jeshi la polisi ni kukamata kwa mujibu wa sheria siyo kuuwa, kujeruhi na kutupa watu hovyo!

Kitendo kilichofanywa na jeshi la polisi kwa makada wa chadema kuwashambulia, kuwajeruhi na kuwatupa si cha kiungwana hata kidogo.
Ni kitendo cha kishetani kisicho hata na chembe ya utu ndani yake!

Hakuna aliyejuu ya sheria, Kumshambulia Raia ambae hana hatia, kumjeruhi na kibaya zaidi kwenda kumtupa kama takataka ni dhihaka ya juu sana kwa Mungu aliyemuumba;

Ni ishara ya kumuonesha hata Mungu kwamba aliumba takataka ambayo uhai wake hauna thamani.
Polisi Polisi polisi Mlioshiriki huo unyama Hakika nawaambia huo siyo Upolisi bali Uharifu kuliko hata waharifu wengine.

Wote mlioshiriki kusuka, kupanga, kujeruhi, kuumiza na kutupa hao viumbe wa Mungu Laana haitakauka Maishani mwenu kwa kufuru mliyoifanya!

Mmelifedhehesha sana jeshi la polisi bila sababu yoyote ya msingi!

Nafaham mlitaka kutuma ujumbe wa vitisho lakini inafaida gani kwenu kwa kujitwalia laana hiyo kuu?
 
Huyu mama mwenye mamlaka ya RSM katika kambi moja ya polisi jijini alilo lifanya jana halita muacha siku zote za maisha yake na laana itamuandama katika uzao wake.
 

Attachments

  • FB_IMG_1745555198811.jpg
    FB_IMG_1745555198811.jpg
    33.6 KB · Views: 18
  • FB_IMG_1745555206090.jpg
    FB_IMG_1745555206090.jpg
    41.3 KB · Views: 19
Huyu mama mwenye mamlaka ya RSM katika kambi moja ya polisi jijini alilo lifanya jana halita muacha siku zote za maisha yake na laana itamuandama katika uzao wake.
RSM ni Resident Sergeant Major ili hawa vijana wa siku hizi ambao haya mambo ya kijeshi/kipolisi hawajui, basi wajue
 
Huyu mama mwenye mamlaka ya RSM katika kambi moja ya polisi jijini alilo lifanya jana halita muacha siku zote za maisha yake na laana itamuandama katika uzao wake.
Ni jambo la hovyo sana kutweza na kutoa uhai wa mtu pasipo hatia, ni zaidi ya unyama
 
Mungu alifanya kazi siku sita, siku ya saba akapumzika, shetani akamvizia siku ya saba akaumba polisi
 
Back
Top Bottom