Unazifahamu phonetic alphabet?

Unazifahamu phonetic alphabet?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
10,889
Reaction score
18,836
Wakati mwingine kumtajia mtu jina na akakusikia vizuri ni kazi sana. Mara nyingi anaweza kukosea kuandika jina lako sababu hakusikia vizuri. Hivyo watu walikuja na phonetic alphabet ambazo msikiaji anaelewa wazi wazi herufi inayotamkwa. Kuna haja ya kuja na phonetic alphabet za kiswahili au abechede yetu inafanya kazi vizuri kabisa?
1719833347067.png
 
Makonda na wakatisha tiketi huwa wanakosea sana majina ya abiria, hata ukirudia mara tatu kumtajia majina yako akikupa tiketi utakuta ameandika majina si yako. Mfano loth hema utakuta ameandika noti ema
 
Tango victor mike,mikekilouniformunifom,thank u very much mkuu,umenikumbusha G4S nikiwa normal guard 2011 huko zenji ndo ilikuwa lugha yetu hiyo ya lindoni
 
Kwenye Aviation sana sana hizi ndizo hutumika kati ya marubani na waongoza ndege( Air Traffic Controllers)

Mfano Rubani wa ndege ya Air Tanzania yenye usajili wa 5H-TCE akitaka kuruka ataanza kujitambulisha kwa control Tower kwamba yeye ni "Five Hotel, Tango Charlie Echo"

Kisha yule jamaa wa control Tower atafahamu kwamba hii ni ndege ya Air Tanzania yenye usajili 5H-TCE. Then maongezi mengine yatafuata.

Kwa uchache tu.
 
Back
Top Bottom