Unayetafuta Mke/Mume

Unayetafuta Mke/Mume

angelita

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2013
Posts
3,017
Reaction score
2,446
Kila kijana au msichana anataka mwenza anayemcha Mungu, mwaminifu, mkweli, mkarimu, anayejali na mwenye upendo wa kweli. Na hayo ni mambo muhimu ya kuyatafuta kwa mwenzi wa Maisha.

Sasa cha kujiuliza kwanza ni je wewe unazo sifa zote? Je mtu akitafuta Mwenye sifa hizo unaweza kuwa mmoja wapo? Kumbuka Mungu anakupa wa kufanana naye.

Kabla hujaanza kuzunguka huku na huko, kutafuta mchumba mcha Mungu, anza leo kumcha Mungu. Haiwezekani binti au kijana unakesha bar, club na mambo Kama hayo halafu Mungu akupe mwenza mcha Mungu, Mungu hawezi kumpa mtoto wake anayemcha mtu Kama wewe, ambae haendi Kanisani, huna maombi binafsi, haufuati neno la Mungu na hauna uhusiano binafsi na Mungu.

Unataka mwenza mpole, mkarimu mwenye upendo wa kweli. Hakikisha hizo sifa unazo kwanza wewe. Jambo la kwanza la kuwa na mahusiano Imara ni kuinvest kwako kujenga kiroho chako character na muonekano. Hivyo kabla hujaangalia kushoto na kulia jiangalie kwanza wewe.
 
Vizur angelita kutukumbusha walimwengu.

Wengne huko church tunaonekana mara 3 kwa mwaka sababu ni shughuli zetu zinatutenga na j.pili uwenyejini.

Sabab nyingne ya kutompata wa kufanana naye ni haraka zetu. Tunapishana na muda sababu ya kasi ya maisha na utafutaji. Bado mkuu angelita uko sahihi....ILA tutaendelea ku-meet pasipo kufanana. TUKIKUTANA NDIPO TUTAFANYA MARIDHIANO YA KUFANANA KWETU.
 
Hahahaaaa Mbona mna mjaza Mungu maneno mdomoni jamani? Kuna wanaume kibao wanakesha bar na ni watu wa Michepuko lakini wameoa wanawake watulivu na walokole,and vice versa pia. Hili unasemaje? Mungu hakuwepo mpaka kawapa hawa wanawake na wanaume wenza wa Hivyo wakati wao wametulia?

Maamuzi ya Muumba Hamna anaye yajua na kujua formula anayo tumia. Mimi Nadhani Mtu kama una amua kubadilika basi badilika kwasababu ya nafsi yako na Si Kwasababu ya kupata mwenza mwema,maana mwisho wa siku wote tutafukiwa na tutakuwa na cha kujibu mbele yake.

Unacho kisema Hapa kina maana Kuwa ukishapata Huyo mwenza basi unaweza kurudi kwenye tabia zako Za awali,Au ikitokea mmetengana basi urudi tabia yako!

Do it for your soul and not for anyone else then the rest will follow.
 
Hahahaaaa Mbona mna mjaza Mungu maneno mdomoni jamani? Kuna wanaume kibao wanakesha bar na ni watu wa Michepuko lakini wameoa wanawake watulivu na walokole,and vice versa pia. Hili unasemaje? Mungu hakuwepo mpaka kawapa hawa wanawake na wanaume wenza wa Hivyo wakati wao wametulia?

Maamuzi ya Muumba Hamna anaye yajua na kujua formula anayo tumia. Mimi Nadhani Mtu kama una amua kubadilika basi badilika kwasababu ya nafsi yako na Si Kwasababu ya kupata mwenza mwema,maana mwisho wa siku wote tutafukiwa na tutakuwa na cha kujibu mbele yake.

Unacho kisema Hapa kina maana Kuwa ukishapata Huyo mwenza basi unaweza kurudi kwenye tabia zako Za awali,Au ikitokea mmetengana basi urudi tabia yako!

Do it for your soul and not for anyone else then the rest will follow.

Umenukuu vibaya Mkuu hiyo sio maana yake.

Huwezi kupata kazi nzuri yenye mshahara mzuri kama huna sifa za kukufanya upate hiyo kazi lbd ubahatike.

Nivizuri ukianza kujijenga kwanza wewe, ndio ugeukie upande wa pili. Hivyo unavyoviitaji kwa mwenzio na yeye pia anaviitaji.
 
Umenukuu vibaya Mkuu hiyo sio maana yake.

Huwezi kupata kazi nzuri yenye mshahara mzuri kama huna sifa za kukufanya upate hiyo kazi lbd ubahatike.

Nivizuri ukianza kujijenga kwanza wewe, ndio ugeukie upande wa pili. Hivyo unavyoviitaji kwa mwenzio na yeye pia anaviitaji.

Upo sahihi lkn nia na dhumuni la kujijenga binafsi iwe kwa ajili ya manufaa yako na Si kwa ajili tu ya kupata hiyo kazi,hiyo itakusaidia kuwa mpana kwenye mambo Mengi zaidi ya hayo yanayo husu hiyo kazi. kwasababu kuna Kesho na kesho kutwa kazi inaweza kuota mabawa kwahiyo utakuwa umejengeka kuweza kufanya biashara Au kupata kazi nyingine.

Kwahiyo kama tutakuwa na nia ya kujijenga kwa manufaa yetu tutakuwa tuna wigo mpana zaidi kuliko ambavyo utakuwa una target kazi fulani Au kupata mwenza mwema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom