Unaweza kuwa na nyota na usiwe na bahati na ukawa na bahati usiwe na nyota

Comred Mbwana Allyamtu

JF-Expert Member
Jun 28, 2016
348
847
UNAWEZA KUWA NA NYOTA NA USIWE NA BAHATI NA UKAWA NA BAHATI USIWE NA NYOTA.

Na. Comred Mbwana Allyamtu (CMCA)
Friday -19/02/2021
Marangu, Kilimanjaro, Tanzania

Actually iko hivyo, nyota na bahati ni vitu viwili tofauti kwenye safari ya maisha ya mwanadamu, kupata pesa ni bahati ila kuwa tajiri ni nyota, najua sijaeleweka hapa.

Any way...

Namanisha kuwa unaweza kuwa na pesa na usiwe tajiri, utajiri ni utamaduni wa kuwa na nidhamu ya pesa, muhasibu anaweza kutunza Billion's of money huku yeye akiwa masikini na akasimamia nidhamu ya fedha na kampuni isiteteleke huku yeye akilipwa laki saba kwa mwezi na akiishia kulalamika ugumu wa maisha mpaka siku anastaafu.

Hii inamaana kuwa kuitunza pesa mpaka kuwa tajiri inaitaji karma ya Mungu, no matter unaingiza pesa kiasi gani, simanishi kuwa mtu hawezi kuwa tajiri, ndio maana Bill Gates aliwahi kusema "Kuzaliwa masikini sio kosa ila kosa ni kufa masikini".

Unaweza kutengenezwa kuwa tajiri na unaweza kutengenezwa kuwa masikini, kama ambavyo matajiri wanageuzwa kuwa mashetani na masikini kuwa malaika, ila kumbuka huwezi kuwa tajiri kama huna nyota, hivi ndivo ilivyo kwenye kila kitu katika maisha ya mwanadamu.

Najua bado unastaajabu hili nalo eleza, huwezi kuwa yoyote kama huna nyota, lakini unaweza kufanya chochote ukiwa na bahati, iko hivyo.

Ebu tazama, kwa miaka 36, Maalim Seif alikuwa kwenye siasa huko Zanzibar, miaka yote hiyo alifanya siasa kutafuta uraisi, lakini Mungu hakumpa nyota ya uraisi bali Mungu alimpa bahati ya kuwa mwanasiasa bora nyakati zote Zanzibar, hata alipo shinda kwenye uchaguzi hakupewa ushindi hii ni kwasababu alikuwa na bahati ila alikosa nyota tu ya uraisi, hata alipo lazimisha aliishia umakamu rais tu, hii ndio maana halisi ya nyota na bahati.

Hii ya nyota na bahati katika maisha ya mwanadamu inamaana kubwa, ndio maana hata katika uchaguzi wa Rais Zanzibar mwaka 1985, yaani kwenye mchakato wa kupata jina la mgombea urais wa CCM, mchuano ulikuwa mkali mno baina ya Seif na Rais wa Nne wa visiwa hivyo, Idris Abdul Wakil, Kwamba Wazazibari wengi walitaka Seif ndiye awe Rais wa Zanzibar baada ya Rais Ali Hassan Mwinyi kupitishwa na Halmashauri Kuu CCM kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini Mungu akamnyima Seif nyota ya uraisi na kumpa bahati kisha Idris Abdul Wakil akapewa nyota ndio maana hakuangaika hata kuupata uraisi, Sasa nadhani unanielewa naposema bahati na nyota.

Hata kitendo cha Abdul Wakili kupigiwa kura nyingi za hapana, bado alishida kwasababu alikuwa na nyota ya uraisi na Seif alikuwa na bahati ya uraisi.

Hicho ni kipimo tosha kuwa Seif alipendwa sana na raia wake ila alikosa nyota tu ya kuwa raisi wa nchi, ndio maana hata uchaguzi wa urais wa Zanzibar mwaka 1995, alitikisa nchi, Alitoka wa pili nyuma ya Rais wa Tano wa Zanzibar, Dk Salmin Amour Juma, katika mchuano uliokuwa mkali, yeye alidai alishinda lakini bado hakuwa raisi, kwasababu alikuwa na bahati sio nyota.

Unajua unaweza kujiuliza inakuwaje Alli Kiba anaimba vizuri kuliko Mondi, aliingia kwenye gemu mda mrefu kuliko Mondi, lakini Diamond anamzidi mafanikio Kiba? Jibu ni rahisi, ni kwamba Kiba ana bahati ya muziki ila Mondi ana 'nyota' ya muziki.

Ndivyo ilivyo kwa Lowassa na Magufuli, Magufuli alikuwa na nyota ya urais, hakuwahi kuusaka uraisi kwenye historia yake, uraisi ulimuijia tu kama kuokota dodo kwenye mkaratusi, ndio maana alipojaribu tu uraisi alisukumiziwa moja kwa moja, hii ndio maana halisi ya 'nyota', tofauti na Lowassa aliye utafuta uraisi toka 1995, alitumia nguvu zake zote, pesa zake zote ili aupate uraisi lakini bado hakuupata ni kwasababu alikuwa na bahati ya urais na sio nyota.

Ndivyo ilivyo kuwa kwa Raila Odinga, Morgan Tsvangalai wa Zimbabwe, Kiza Besige au Etienne Tsekedi, Etienne Tsekedi Wamulumba aliusaka uraisi wa Kongo toka 1993 mpaka kifo kinamkuta aliambulia Uwaziri mkuu tu, yote haya yanadhihilisha unavyoweza kuwa na bahati na kukosa Nyota.

Felix Tsekedi hakuwahi kuota ndoto za uraisi, ila nyota ndio imemfanya kuwa raisi baada ya Kabila kumuhofia Moise Katumbi hivyo akauza urais kwa Felix Tsekedi na kumchinjia baharini Martin Fayulu, hivyo Felix Tsekedi Nyota ndio imemfanya kuwa raisi nafasi ambayo hakuwahi kuiangaikia.

Sasa Basi...

Nyota ni karma na ndoto ambayo Mungu amekupangia, yani mapito kwa kile ambacho Mungu amekupangia.

Ndio maana Gerald Ford alichaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Marekani kwa tiketi ya Republican mwaka 1949, Baada ya kuhudumia kipindi kimoja barazani, alitamani kuwa Spika, Bahati mbaya baraza lilikuwa na wawakilishi wengi wa Democrats, Hivyo, Democrats wakawa wanatoa Spika kila baada ya miaka miwili, nataka nikuoneshe tofauti ya "Bahati" na "Nyota".

Ford akaanza kuwekeza nguvu kwenye kufanya kampeni za Republican ili chama hicho kipate wawakilishi wengi, apate kutimiza azma yake ya kuwa spika.

Kila uchaguzi Republican walipigwa na Democrats, Ford akaishia kuwa kiongozi wa upinzani (house of minority), akaanza kujikatia tamaa, ilifika mahala chama chake kumpa fursa ya kugombea ugavana au useneta, aligoma, akisema ndoto yake ni Uspika.

Baada ya uchaguzi mwaka 1972, Democrats walishinda tena wawakilishi wengi, Ford akamwambia mkewe, Betty: "Nitajaribu tena mwaka 1974, tukishinda, nitakuwa Spika miaka miwili na mwaka 1976 nitastaafu, Tukishindwa, nitabaki mwakilishi mpaka mwaka 1976 halafu nitastaafu, " Ford akaendelea kuwa kiongozi wa upinzani.

Oktoba 10, 1973, Makamu wa Rais, Spiro Agnew, alijiuzulu kwa kashfa ya rushwa, Rais aliyekuwa madarakani, Richard Nixon, alikuwa Republican, Bunge (Congress) lilitawaliwa na Democrats, Nixon ikabidi afanye mazungumzo na viongozi wa Congress kuhusu uteuzi wa Makamu wa Rais, Congress wakamwambia hakuna mwingine zaidi ya Ford, nataka uone utofauti baina ya Bahati na Nyota.

Nixon akamtangaza Ford kuwa Makamu wa Rais na kupitishwa na Congress, Ford akamwambia Betty, "Nilitamani Uspika, lakini nimepata cheo kikubwa zaidi ya usipika Nadhani Umakamu wa Rais ni cheo kikubwa kunitosha kustaafu siasa 1976".

Ila kwakuwa Nyota ni karma na ndoto ambayo Mungu amekupangia, Mwaka 1974, Congress walimkuta Nixon na hatia ya kufanya faulo kwenye uchaguzi wa mwaka 1972 uliomrejesha madarakani kwa muhula wa pili, Faulo za Nixon hujulikana kama Kashfa ya Watergate, hivyo Nixon akang'oka madarakani, na makamu wake wa Rais, Ford akawa Rais, hii ndio maana halisi ya msamiati Nyota.

Nyota ni "Hidden Power" yani nguvu iliyofichwa ndani yako, Ni nguvu ambayo unakuwa nayo wewe lakini inatokana na kudra na mipango ya Mungu, ndio maana Ford aliutaka Uspika, akapambana miaka mingi na hakuupata, Ghafla akawa Makamu wa Rais kisha Rais bila kugombea, hii ndio Nyota, Huku Maalim Seif aliutaka uraisi akapambana miaka mingi na hakuupata, Ghafla akawa Makamu wa kwanza wa Rais, hii ndio bahati.

Bahati ni jitihada zilizo beba kudura ya Mungu, ndio maana unaweza kupambania ndoto yako na usifanikiwe kwa sababu kudura za Mungu kwako ni bahati tu na sio Nyota, Sasa nadhani nimeeleweka

Nyota ndio iliyomfanya Joe Biden kurejea Ikulu ya White House, alikotumikia miaka minane akiwa makamu wa rais, baada ya kuitafuta nafasi hii kwa karibu miaka 36 wakati akilitumikia Baraza la Seneti la Marekani, huku bahati aliyokuwa nayo Hillary Clinton ndio imemfanya ikulu ya White House ibaki historia kwake kuihudumu kama Rais wa nchi.

Unaweza kuwa na ndoto, lakini isitimie kwakuwa Nyota yako haiwezi kukufanya ufanikiwe, halikadharika unaweza kufanikiwa kwakuwa una bahati ila usifikie ndoto kwakuwa Nyota yako haiwezi kukufanya ufanikiwe kwenye ndoto yako.

Kwa kupata makala Zaidi wasiliana na Mimi WhatsApp 0679555526 uungwe group la Maktaba Kuu.

Ukinakili kazi zangu kumbuka kufanya acknowledgment.
Wako Mjoli wa Historia na diplomasia ya ulimwengu.

Ndimi: Comred Mbwana Allyamtu
Copyrights of this article reserved
written by Comred Mbwana Allyamtu
•Napatika Kwa mawasliano
Comred Mbwana Allyamtu

Kwa Tanzania
+255679555526.
+255765026057.

Kwa Rwanda
+250733153930
+250788214234

Kwa DRC
+243 977 860 824
Email- mbwanaallyamtu990@gmail.com

Copyright 2021, All Rights Reserved.

Maktaba Kuu.


FB_IMG_6125493025171306886.jpg
 
Je, nyota ya mtu mmoja inaweza kuibiwa, kuchafuliwa au kufifishwa na mtu mwingine ?
 
1)Unaweza kuwa tajiri alafu usiwe na nyota?2)Je'unaweza kuwa na nyota lakini ukawa masikini?
3)Naweza tafuta nikajua nyota yangu iliyofichwa ni ipi?
Rakims
 
1)Unaweza kuwa tajiri alafu usiwe na nyota?2)Je'unaweza kuwa na nyota lakini ukawa masikini?
3)Naweza tafuta nikajua nyota yangu iliyofichwa ni ipi?
Rakims
Habari mkuu,

MAJIBU:
1: Katika mfumo mzima wa unajimu nyota ni kipengele kimoja katika unajimu ndani humo kuna kitu kinaitwa milango au nyumba na mmoja kati ya hiyo ukiwa vizuri basi utanufaika huko na mmoja ukiwa vibaya basi utapata hasara huko na mwingine ukifa huko basi utafia huko ni ngumu kuelewa lakini rahisi kufahamu ikiwa utapitia makala yangu hii bonyeza link hii chini


2: Rejea jibu la kwanza

3: Ndio unaweza lakini nyota yako ni moja labda kama swali lako ni mlango upi umefungwa au umefichwa

Rakims
 
Habari mkuu,

MAJIBU:
1: Katika mfumo mzima wa unajimu nyota ni kipengele kimoja katika unajimu ndani humo kuna kitu kinaitwa milango au nyumba na mmoja kati ya hiyo ukiwa vizuri basi utanufaika huko na mmoja ukiwa vibaya basi utapata hasara huko na mwingine ukifa huko basi utafia huko ni ngumu kuelewa lakini rahisi kufahamu ikiwa utapitia makala yangu hii bonyeza link hii chini


2: Rejea jibu la kwanza

3: Ndio unaweza lakini nyota yako ni moja labda kama swali lako ni mlango upi umefungwa au umefichwa

Rakims
Mkuu kwenye blog yako nimepitia mpaka mwisho,ila ntapitia tena vizuri nikiwa home nimetulia,nambayako ya Airtel nimeisave ntakutafuta tu.
 
UNAWEZA KUWA NA NYOTA NA USIWE NA BAHATI NA UKAWA NA BAHATI USIWE NA NYOTA.

Na. Comred Mbwana Allyamtu (CMCA)
Friday -19/02/2021
Marangu, Kilimanjaro, Tanzania

Actually iko hivyo, nyota na bahati ni vitu viwili tofauti kwenye safari ya maisha ya mwanadamu, kupata pesa ni bahati ila kuwa tajiri ni nyota, najua sijaeleweka hapa.

Any way...

Namanisha kuwa unaweza kuwa na pesa na usiwe tajiri, utajiri ni utamaduni wa kuwa na nidhamu ya pesa, muhasibu anaweza kutunza Billion's of money huku yeye akiwa masikini na akasimamia nidhamu ya fedha na kampuni isiteteleke huku yeye akilipwa laki saba kwa mwezi na akiishia kulalamika ugumu wa maisha mpaka siku anastaafu.

Hii inamaana kuwa kuitunza pesa mpaka kuwa tajiri inaitaji karma ya Mungu, no matter unaingiza pesa kiasi gani, simanishi kuwa mtu hawezi kuwa tajiri, ndio maana Bill Gates aliwahi kusema "Kuzaliwa masikini sio kosa ila kosa ni kufa masikini".

Unaweza kutengenezwa kuwa tajiri na unaweza kutengenezwa kuwa masikini, kama ambavyo matajiri wanageuzwa kuwa mashetani na masikini kuwa malaika, ila kumbuka huwezi kuwa tajiri kama huna nyota, hivi ndivo ilivyo kwenye kila kitu katika maisha ya mwanadamu.

Najua bado unastaajabu hili nalo eleza, huwezi kuwa yoyote kama huna nyota, lakini unaweza kufanya chochote ukiwa na bahati, iko hivyo.

Ebu tazama, kwa miaka 36, Maalim Seif alikuwa kwenye siasa huko Zanzibar, miaka yote hiyo alifanya siasa kutafuta uraisi, lakini Mungu hakumpa nyota ya uraisi bali Mungu alimpa bahati ya kuwa mwanasiasa bora nyakati zote Zanzibar, hata alipo shinda kwenye uchaguzi hakupewa ushindi hii ni kwasababu alikuwa na bahati ila alikosa nyota tu ya uraisi, hata alipo lazimisha aliishia umakamu rais tu, hii ndio maana halisi ya nyota na bahati.

Hii ya nyota na bahati katika maisha ya mwanadamu inamaana kubwa, ndio maana hata katika uchaguzi wa Rais Zanzibar mwaka 1985, yaani kwenye mchakato wa kupata jina la mgombea urais wa CCM, mchuano ulikuwa mkali mno baina ya Seif na Rais wa Nne wa visiwa hivyo, Idris Abdul Wakil, Kwamba Wazazibari wengi walitaka Seif ndiye awe Rais wa Zanzibar baada ya Rais Ali Hassan Mwinyi kupitishwa na Halmashauri Kuu CCM kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini Mungu akamnyima Seif nyota ya uraisi na kumpa bahati kisha Idris Abdul Wakil akapewa nyota ndio maana hakuangaika hata kuupata uraisi, Sasa nadhani unanielewa naposema bahati na nyota.

Hata kitendo cha Abdul Wakili kupigiwa kura nyingi za hapana, bado alishida kwasababu alikuwa na nyota ya uraisi na Seif alikuwa na bahati ya uraisi.

Hicho ni kipimo tosha kuwa Seif alipendwa sana na raia wake ila alikosa nyota tu ya kuwa raisi wa nchi, ndio maana hata uchaguzi wa urais wa Zanzibar mwaka 1995, alitikisa nchi, Alitoka wa pili nyuma ya Rais wa Tano wa Zanzibar, Dk Salmin Amour Juma, katika mchuano uliokuwa mkali, yeye alidai alishinda lakini bado hakuwa raisi, kwasababu alikuwa na bahati sio nyota.

Unajua unaweza kujiuliza inakuwaje Alli Kiba anaimba vizuri kuliko Mondi, aliingia kwenye gemu mda mrefu kuliko Mondi, lakini Diamond anamzidi mafanikio Kiba? Jibu ni rahisi, ni kwamba Kiba ana bahati ya muziki ila Mondi ana 'nyota' ya muziki.

Ndivyo ilivyo kwa Lowassa na Magufuli, Magufuli alikuwa na nyota ya urais, hakuwahi kuusaka uraisi kwenye historia yake, uraisi ulimuijia tu kama kuokota dodo kwenye mkaratusi, ndio maana alipojaribu tu uraisi alisukumiziwa moja kwa moja, hii ndio maana halisi ya 'nyota', tofauti na Lowassa aliye utafuta uraisi toka 1995, alitumia nguvu zake zote, pesa zake zote ili aupate uraisi lakini bado hakuupata ni kwasababu alikuwa na bahati ya urais na sio nyota.

Ndivyo ilivyo kuwa kwa Raila Odinga, Morgan Tsvangalai wa Zimbabwe, Kiza Besige au Etienne Tsekedi, Etienne Tsekedi Wamulumba aliusaka uraisi wa Kongo toka 1993 mpaka kifo kinamkuta aliambulia Uwaziri mkuu tu, yote haya yanadhihilisha unavyoweza kuwa na bahati na kukosa Nyota.

Felix Tsekedi hakuwahi kuota ndoto za uraisi, ila nyota ndio imemfanya kuwa raisi baada ya Kabila kumuhofia Moise Katumbi hivyo akauza urais kwa Felix Tsekedi na kumchinjia baharini Martin Fayulu, hivyo Felix Tsekedi Nyota ndio imemfanya kuwa raisi nafasi ambayo hakuwahi kuiangaikia.

Sasa Basi...

Nyota ni karma na ndoto ambayo Mungu amekupangia, yani mapito kwa kile ambacho Mungu amekupangia.

Ndio maana Gerald Ford alichaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Marekani kwa tiketi ya Republican mwaka 1949, Baada ya kuhudumia kipindi kimoja barazani, alitamani kuwa Spika, Bahati mbaya baraza lilikuwa na wawakilishi wengi wa Democrats, Hivyo, Democrats wakawa wanatoa Spika kila baada ya miaka miwili, nataka nikuoneshe tofauti ya "Bahati" na "Nyota".

Ford akaanza kuwekeza nguvu kwenye kufanya kampeni za Republican ili chama hicho kipate wawakilishi wengi, apate kutimiza azma yake ya kuwa spika.

Kila uchaguzi Republican walipigwa na Democrats, Ford akaishia kuwa kiongozi wa upinzani (house of minority), akaanza kujikatia tamaa, ilifika mahala chama chake kumpa fursa ya kugombea ugavana au useneta, aligoma, akisema ndoto yake ni Uspika.

Baada ya uchaguzi mwaka 1972, Democrats walishinda tena wawakilishi wengi, Ford akamwambia mkewe, Betty: "Nitajaribu tena mwaka 1974, tukishinda, nitakuwa Spika miaka miwili na mwaka 1976 nitastaafu, Tukishindwa, nitabaki mwakilishi mpaka mwaka 1976 halafu nitastaafu, " Ford akaendelea kuwa kiongozi wa upinzani.

Oktoba 10, 1973, Makamu wa Rais, Spiro Agnew, alijiuzulu kwa kashfa ya rushwa, Rais aliyekuwa madarakani, Richard Nixon, alikuwa Republican, Bunge (Congress) lilitawaliwa na Democrats, Nixon ikabidi afanye mazungumzo na viongozi wa Congress kuhusu uteuzi wa Makamu wa Rais, Congress wakamwambia hakuna mwingine zaidi ya Ford, nataka uone utofauti baina ya Bahati na Nyota.

Nixon akamtangaza Ford kuwa Makamu wa Rais na kupitishwa na Congress, Ford akamwambia Betty, "Nilitamani Uspika, lakini nimepata cheo kikubwa zaidi ya usipika Nadhani Umakamu wa Rais ni cheo kikubwa kunitosha kustaafu siasa 1976".

Ila kwakuwa Nyota ni karma na ndoto ambayo Mungu amekupangia, Mwaka 1974, Congress walimkuta Nixon na hatia ya kufanya faulo kwenye uchaguzi wa mwaka 1972 uliomrejesha madarakani kwa muhula wa pili, Faulo za Nixon hujulikana kama Kashfa ya Watergate, hivyo Nixon akang'oka madarakani, na makamu wake wa Rais, Ford akawa Rais, hii ndio maana halisi ya msamiati Nyota.

Nyota ni "Hidden Power" yani nguvu iliyofichwa ndani yako, Ni nguvu ambayo unakuwa nayo wewe lakini inatokana na kudra na mipango ya Mungu, ndio maana Ford aliutaka Uspika, akapambana miaka mingi na hakuupata, Ghafla akawa Makamu wa Rais kisha Rais bila kugombea, hii ndio Nyota, Huku Maalim Seif aliutaka uraisi akapambana miaka mingi na hakuupata, Ghafla akawa Makamu wa kwanza wa Rais, hii ndio bahati.

Bahati ni jitihada zilizo beba kudura ya Mungu, ndio maana unaweza kupambania ndoto yako na usifanikiwe kwa sababu kudura za Mungu kwako ni bahati tu na sio Nyota, Sasa nadhani nimeeleweka

Nyota ndio iliyomfanya Joe Biden kurejea Ikulu ya White House, alikotumikia miaka minane akiwa makamu wa rais, baada ya kuitafuta nafasi hii kwa karibu miaka 36 wakati akilitumikia Baraza la Seneti la Marekani, huku bahati aliyokuwa nayo Hillary Clinton ndio imemfanya ikulu ya White House ibaki historia kwake kuihudumu kama Rais wa nchi.

Unaweza kuwa na ndoto, lakini isitimie kwakuwa Nyota yako haiwezi kukufanya ufanikiwe, halikadharika unaweza kufanikiwa kwakuwa una bahati ila usifikie ndoto kwakuwa Nyota yako haiwezi kukufanya ufanikiwe kwenye ndoto yako.

Kwa kupata makala Zaidi wasiliana na Mimi WhatsApp 0679555526 uungwe group la Maktaba Kuu.

Ukinakili kazi zangu kumbuka kufanya acknowledgment.
Wako Mjoli wa Historia na diplomasia ya ulimwengu.

Ndimi: Comred Mbwana Allyamtu
Copyrights of this article reserved
written by Comred Mbwana Allyamtu
•Napatika Kwa mawasliano
Comred Mbwana Allyamtu

Kwa Tanzania
+255679555526.
+255765026057.

Kwa Rwanda
+250733153930
+250788214234

Kwa DRC
+243 977 860 824
Email- mbwanaallyamtu990@gmail.com

Copyright 2021, All Rights Reserved.

Maktaba Kuu.


View attachment 1709354
Haya mambo ya nyota na bahati ni upuuzi na story unaopstikana Afrika tu,Tena kwa watu wa chini kwa kipato,hizi story utazisikia Kawe,Tandale,usawhilini,hizi story utazisikia kwenye vijiwe vya kahawa,shoeshine,bodaboda,na kwa watu wasio hata na shahada kichwani.
Huwezi kusikia hizi story maeneo ya Seaclif,white sand hotel,Kwenye casino,le grande casino posta,au watu wanapiga cigars pale Kapital lounge makumbusho ukute wanaongea huu upuuzi.
Hakuna Cha nyota Wala bahati,It's just life and plans.
 
Siri iliyopo katika Miguu yako na Ulimwengu wako wa Roho
 

Attachments

  • images (26).jpeg
    images (26).jpeg
    32.1 KB · Views: 2
Siri iliyopo katika Miguu yako na Ulimwengu wako wa Roho


Umewahi kujiuliza kwanini wachawi huwa wanachota mchanga mahali zilipokanyaga nyayo za mtu?


+255758669940


Ndugu mpendwa , miguu yako ina maana kubwa Sana na umuhimu wa kipekee katika ulimwengu wa roho . Na hii ni kwa pande zote mbili , ulimwengu wa Roho wa Nuru Siri iliyopo katika Miguu yako na Ulimwengu wako wa Roho ulimwengu wa roho wa giza.
Kibaya ni kwamba shetani anazitumia Sana Siri nyingi za ulimwengu wa roho ambazo wanadamu wengi wamefichwa na wanaofunuliwa ni wachache Sana. Ndiyo maana Mungu anasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.


Upo muunganiko (connection) mkubwa Sana Kati ya nyayo za miguu yako na nafsi yako ktk ulimwengu wa roho. Nyayo zako zimebeba taarifa zako zote . Mchawi anapopata nyayo zako anaweza kuelewa kila kitu kinachohusiana na maisha yako . Na kama hauna ulinzi wa kiroho , anaweza kufunga kila kitu ktk maisha yako .
Nyayo zako zinapokanyaga juu ya ardhi zinaacha taarifa zako hapo. Na ndiyo maana ardhi ya kwako/ nyumbani kwenu inakutambua na inakusikiliza chochote utakachoiambia. Au hili nalo haulifahamu nije kukufafanulia siku nyingine? Na hapa ndiyo uelewe laana aliyopewa kaini inavyofanya kazi ( kulaaniwa juu ya ardhi).


+255758669940


Yaani ukilaaniwa juu ya ardhi ,nyayo zako zinabeba taarifa . Kwahiyo kila utakapokwenda ukishakanyaga tu mguu wako ktk ardhi nyayo zako zinatoa taarifa ktk ardhi hiyo "huyu mtu ameelaaniwa juu ya ardhi" . Kwahiyo hata ufanye nini uende wapi hutafanikiwa mpk laana ivunjwe..


Kwahiyo nyayo zako zina connection Kati ya ardhi na mbingu .


Labda nikupe changamoto Kidogo ambayo unaweza usiipende wewe mkristo lkn ndiyo maarifa yenyewe nakuongezea Sasa.


Umewahi kujiuliza kwanini wafuasi wa Mwamposa hawayakanyagi mafuta ya upako wakiwa wamevaa viatu??


Ni ukweli kuwa Mungu anapenda usafi , lkn Umewahi kujiuliza kwa kina kwanini manabii wote pamoja na Yesu ,wayahudi walikuwa wanavua viatu walipokuwa wanakaribia mbele za Mungu hata Kama ni porini kwny mifugo? Mungu anamwambia Musa "vua viatu maana mahali hapa ni patakatifu". Ilikuwa ni lazima connection ya nyayo isome kwny ardhi ipeleke taarifa kwenye ulimwengu wa Roho.


Tuliache hilo ni somo la siku nyingine . Turudi kwny mada kuU

NYAYO ZAKO ZIMEBEBA VITU GANI? MAFANIKIO YAKO


Mchawi anapotaka kuiba muda wamafanikio yako na wakati wa mwanadamu huwa anapiga na kumfunga MIGUU:


Anakufunga miguu kwasavabu katika miguu yako ndio kika kitu kipo huko taalifa zako bahati yako mafanikio yako huanzia kwenye miguu


Katika nyayo za miguu kuna vitu 5 ambavyo wachawi wanalenga kujuondolea katima maisha


💚1. Kibali;💚
- inachafuliwa nyota yako usikubalike na watu bila sababu kila unapoenda. Nyayo zako zimebeba kibali chako cha maisha yako🙏


💚2. Heshima;💚
- Unaondolewa heshima uwe mtu wa kudharauliwa ktk jamii na kuonekana hufai . Ndiyo maana hata kimila vijana huinama na kuwashika miguu wazee nao huwashika kichwa.🙏


💚3. Hatua;💚
- Unafungwa miguu usipige hatua yyt ya maendeleo au mafanikio. Miguu ndiyo inakufanya utembee huko na huko kutafuta riziki . Ukiishafungwa maana yake hutapiga hatua yyt .🙏


💚4. Maamuzi;💚
- wanapokufunga miguu wanakufunga ufahamu wako wa kufikiri usiweze kufanya maamuz ya maana ya kusonga mbele.unapanga mipango mingi mizuri lkn hautekelezi. Hata ukipata wazo zuri kiasi gani utaishia kulisema tu na kuliweka kwny mipango miaka inaenda.🙏


💚5.Umiliki na utawala;💚
-Ukifungwa miguu unapoteza umiliki wa mali na ardhi unayoikanyaga. Hutamiliki Mali na Kama ulikuwa nazo utaanza kufilisika.🙏


Haya ni mambo ambayo roho ya umaskini inapomuingia mtu huwa inamuondolea . Na hivi vyote vinaanzia kwenye nyayo zako.


hakuna mchawi anayependa wewe uendelew wala kufanikiwa kila hatua unayopiga wao huweka vikwazo ili kukulidisha nyuma kimaendelea......


namba yasimu
+255758669940
 
Back
Top Bottom