chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 12,002
- 20,661
Siku hizi kumeibuka kundi la watu likisihi watanzania tuwe wazalendo
Uzalendo ni zao la jinsi unavyoishi na watu unaotaka wawe wazalendo!
Kama ndani ya taifa moja wana ccm wana haki kuliko wa vyama vingine,unatarajia wale wa vyama vingine watakuwa na upendo na nchi yao? Kama wabunge wa ccm wanaenda watakako wanafanya mikutano sehemu yoyote ya nchi bila kukamatwa na polisi,lakini wapinzani wanakamatwa,je katika mazingira haya unataka au unatarajia uzalendo?
Hapo tayari taifa limegawanyika mapande mawili,wale UZALENDO TUMBO/MASLAHI,hawa ni wale watoto wapendwa(sio wa kambo) hawabaguliwi,hawalishwi makombo,na WANATUSIHI TUWE WAZALENDO ili chakula chao kisiingie mchanga waendelee kula
Wengi wanaosihi uzalendo,ukiwachunguza ni watu wanaofaidika na mfumo uliopo(status quo)nadhani hata enzi ya biashara ya utumwa,waliokuwa wanafaidika nayo waliwaita waliokuwa wanaipinga "si wazalendo" uzalendo ni neno linalotumika na wanasiasa kama kichaka
Hivi Wazanzibari wanaoona figisu za uonevu dhidi ya CUF unatarajia na unawaomba wawe wazalendo? Uzalendo ni tunda la haki,tenda haki kwa wananchi uone kama hawatakuwa wazalendo wa kutupwa,nani asiyejua kwamba wanayofanyiwa CUF ni uonevu? Hawa unatarajia wawe wazalendo au waanze movement ya kuirudisha Zanzibar yao(hapa tayari uzalendo wa kuipenda jamhuri ya muungano unatoweka kwa kuwa Taasisi za Tanganyika ndizo zimekalia haki ya CUF)
Hivi unatarajia uzalendo kwa jinsi bunge linavyoendeshwa?
Mwisho,kuna uzalendo kuliko kufata katiba na sheria? Kufata katiba na sheria ndio uzalendo ambao kama taifa TULIJIWEKEA KAMA KIPIMO CHETU CHA JUU,mengine ni kuongeza tu,je tunafata katiba na sheria,
Maana kuna msemo kwamba SAMAKI HUOZA KUANZIA KICHWANI,yanayotokea tarime ,au kumkamata Mwalimu ambaye yeye/mwanafunzi wake hajui jina la mkuu wa wilaya,je ni ishara sasa uozo wa samaki wetu umetapakaa?
Uzalendo ni nini?
Uzalendo ni zao la jinsi unavyoishi na watu unaotaka wawe wazalendo!
Kama ndani ya taifa moja wana ccm wana haki kuliko wa vyama vingine,unatarajia wale wa vyama vingine watakuwa na upendo na nchi yao? Kama wabunge wa ccm wanaenda watakako wanafanya mikutano sehemu yoyote ya nchi bila kukamatwa na polisi,lakini wapinzani wanakamatwa,je katika mazingira haya unataka au unatarajia uzalendo?
Hapo tayari taifa limegawanyika mapande mawili,wale UZALENDO TUMBO/MASLAHI,hawa ni wale watoto wapendwa(sio wa kambo) hawabaguliwi,hawalishwi makombo,na WANATUSIHI TUWE WAZALENDO ili chakula chao kisiingie mchanga waendelee kula
Wengi wanaosihi uzalendo,ukiwachunguza ni watu wanaofaidika na mfumo uliopo(status quo)nadhani hata enzi ya biashara ya utumwa,waliokuwa wanafaidika nayo waliwaita waliokuwa wanaipinga "si wazalendo" uzalendo ni neno linalotumika na wanasiasa kama kichaka
Hivi Wazanzibari wanaoona figisu za uonevu dhidi ya CUF unatarajia na unawaomba wawe wazalendo? Uzalendo ni tunda la haki,tenda haki kwa wananchi uone kama hawatakuwa wazalendo wa kutupwa,nani asiyejua kwamba wanayofanyiwa CUF ni uonevu? Hawa unatarajia wawe wazalendo au waanze movement ya kuirudisha Zanzibar yao(hapa tayari uzalendo wa kuipenda jamhuri ya muungano unatoweka kwa kuwa Taasisi za Tanganyika ndizo zimekalia haki ya CUF)
Hivi unatarajia uzalendo kwa jinsi bunge linavyoendeshwa?
Mwisho,kuna uzalendo kuliko kufata katiba na sheria? Kufata katiba na sheria ndio uzalendo ambao kama taifa TULIJIWEKEA KAMA KIPIMO CHETU CHA JUU,mengine ni kuongeza tu,je tunafata katiba na sheria,
Maana kuna msemo kwamba SAMAKI HUOZA KUANZIA KICHWANI,yanayotokea tarime ,au kumkamata Mwalimu ambaye yeye/mwanafunzi wake hajui jina la mkuu wa wilaya,je ni ishara sasa uozo wa samaki wetu umetapakaa?
Uzalendo ni nini?