Ligogoma
JF-Expert Member
- Aug 27, 2010
- 3,502
- 6,458
Heloo!!!
Ndoa nyingi siku hizi zinavunjika! Zinavunjika kwa sababu upande mmoja una feel hauwezi kubeba jukumu la ndoa!
Kwa nini?
Kwa sababu vijana wanaoa kama fashion, kuiga, kutafuta hadhi na wengine kutafuta hata kipato tena unakuta ni kipato cha nauli za likizo tu ofisini! Zikitokea changamoto za ndoa hawapo tayari kuzikabili!
Kabla ya kuoa, jisikie kwanza unahitaji kuoa, jisikie unahitaji kuwa na mzigo wa familia yako, jisikie unatamani majukumu, jisikie unatamani changamoto mpya katika maisha!
Ukioa kwa kupata hisia katika nafsi, changamoto za ndoa kwako zitakuwa si mzigo kama zilivyo changamoto za familia yako ya awali (baba, mama na nduguzo) ambao tatizo lolote upo tayari kulikabili na si kuwatenga na kukimbia!
Why umkimbie/umkimbize mkeo ilhali tabia hizo hizo umeweza kuzivumilia miaka nenda rudi na hujazikimbia kutoka kwa dada yako?
Nilipofikisha miaka 27 nilijisikia kabisa nahitaji changamoto za ndoa, nilioa nina miaka 29. Rafiki yangu kipenzi nae akaona aoe baada ya mimi kuoa hivyo mwaka uliofuata akiwa na miaka 31 akavuta jiko.
Mwaka mmoja baadae akaachana na mkewe wakiwa na mtoto mmoja, kwa madai mwanamke anamzingua sana tabia mbovu na hafai kuwa mke!
Miaka sita baadae akiwa na miaka takribani 38 akajisikia kuoa sasa, bahati nzuri akamkumbuka mwanae na mkewe walioachana hivyo wakatafutana na bahati mwanamke nae hakuwa kwenye mahusiano thabiti tangu walipoachana hivyo ikarahisisha kurudiana kwao.
Miaka kadhaa sasa wanaishi pamoja raha mustarehe na wameongeza familia, nimemuuliza jamaa yangu vipi mkeo hakuzingui tena!
Akanijibu "Nahisi ule ulikuwa ni utoto, mke wangu kumbe ananipenda sana na kadiri alivyokuwa anaonyesha upendo nikaona kero kama nabanwa banwa, anataka kunitawala, nachungwa, nipo kifungoni na kadhalika. Ajabu maisha ni yale yale lakini sasa hivi nayafurahia sana"
Muoe vijana, muoe mkiwa tayari kwa kuoa kiakili, kimwili na kihisia.
Nimemaliza
Ndoa nyingi siku hizi zinavunjika! Zinavunjika kwa sababu upande mmoja una feel hauwezi kubeba jukumu la ndoa!
Kwa nini?
Kwa sababu vijana wanaoa kama fashion, kuiga, kutafuta hadhi na wengine kutafuta hata kipato tena unakuta ni kipato cha nauli za likizo tu ofisini! Zikitokea changamoto za ndoa hawapo tayari kuzikabili!
Kabla ya kuoa, jisikie kwanza unahitaji kuoa, jisikie unahitaji kuwa na mzigo wa familia yako, jisikie unatamani majukumu, jisikie unatamani changamoto mpya katika maisha!
Ukioa kwa kupata hisia katika nafsi, changamoto za ndoa kwako zitakuwa si mzigo kama zilivyo changamoto za familia yako ya awali (baba, mama na nduguzo) ambao tatizo lolote upo tayari kulikabili na si kuwatenga na kukimbia!
Why umkimbie/umkimbize mkeo ilhali tabia hizo hizo umeweza kuzivumilia miaka nenda rudi na hujazikimbia kutoka kwa dada yako?
Nilipofikisha miaka 27 nilijisikia kabisa nahitaji changamoto za ndoa, nilioa nina miaka 29. Rafiki yangu kipenzi nae akaona aoe baada ya mimi kuoa hivyo mwaka uliofuata akiwa na miaka 31 akavuta jiko.
Mwaka mmoja baadae akaachana na mkewe wakiwa na mtoto mmoja, kwa madai mwanamke anamzingua sana tabia mbovu na hafai kuwa mke!
Miaka sita baadae akiwa na miaka takribani 38 akajisikia kuoa sasa, bahati nzuri akamkumbuka mwanae na mkewe walioachana hivyo wakatafutana na bahati mwanamke nae hakuwa kwenye mahusiano thabiti tangu walipoachana hivyo ikarahisisha kurudiana kwao.
Miaka kadhaa sasa wanaishi pamoja raha mustarehe na wameongeza familia, nimemuuliza jamaa yangu vipi mkeo hakuzingui tena!
Akanijibu "Nahisi ule ulikuwa ni utoto, mke wangu kumbe ananipenda sana na kadiri alivyokuwa anaonyesha upendo nikaona kero kama nabanwa banwa, anataka kunitawala, nachungwa, nipo kifungoni na kadhalika. Ajabu maisha ni yale yale lakini sasa hivi nayafurahia sana"
Muoe vijana, muoe mkiwa tayari kwa kuoa kiakili, kimwili na kihisia.
Nimemaliza