Unakumbuka nini ukiwa Primary?

Unakumbuka nini ukiwa Primary?

mbolea, kidumu ya maji, fagio ya chelewa na kuni aaaa kudadeq ukikosa unarud hom. bado kushika namba sa moja na kufagia duuuuuuuuh nashukuru Mungu yamenitoka
 
Wakuu wakati tuna subir post za TCU eb tujikumbushe machache tukiwa shule ya msingi. Karibu.
Nakumbuka kasuku langu lile la mafuta ya "kimbo"ile ya nusu lita nilikuwa nanyweaga uji!!dadeki nakuwa wa kwanza kupokea naenda fasta kuupooza na kunywa na narudi tena kwenye foleni!!!
 
Tulikua na kundi la vichwa vibovu kama nane hivi tunakaa mtaa mmoja Mabatini mtaa wa Miembe giza tunasoma shule moja..wote tumepinda mbaaya.

Sasa kuna mgahawa wa kisomali walikuwa wanapika msosi unanukia town nzima na Mara kwa Mara tulikuwa tunapita kwenye ule mgahawa na tunaishia kunywa maji tu na kuondoka kwa shingo upande tukiacha harufu murua ya misosi nyuma yetu.

Zamani mtihani wa darasa la saba ilikuwa siku moja ..hivyo siku hiyo baada ya kumaliza mtihani tukakubaliana tunaenda kwenye ule mgahawa..tunaagiza msosi..then baada ya hapo tunatoka nduki kama za kwenye magazeti ya Sani..sawa....sawa! Tukakubaliana.

Mapema kesho yake tukafika mkahawani...tukapiga msosi kila mtu best food yake kama wafungwa wanaosubiri kunyongwa wanavyojipendelea...baada ya kushiba tulitawanyika kwa mbio na kasi ya ajabu na siku hiyo ndio nilijua wasomali wana roho ngumu maana yule msomali wa kaunta alimuunganishia jamaa yetu aliepinda kuliko wote kwenye crew letu..baada ya kurudi na kukutana nae aliekimbizwa na msomali jamaa alisema " aliingia kwenye maji machafu na msomali akavua suruali akabakia na kichupi cha VIP akamfuata kwenye maji machafu ila jamaa akamzidi kete akamwachia manyoya msomali" tukamaliza shule kwa soo! Huko kwenye sherehe ya graduation sasa ndo headmaster au big alisema hatafanya tena sherehe baada ya mitihani ya elo wai! Tulikichafua na Mzee mwanidani bwena mbaaaya!

Asee!! Hiki kituko sitakisahahu ila tulikuwa na vituko saana primary kundi letu.
 
Nakumbuka kuwaburuza wote darasani, kuanzia darasa la kwanza hadi la Saba nambari moja tu kwenye paper.
 
Mi nakumbuka kuandikiana barua za urafiki Dada na kaka na kuchukuliana zawadi
 
Back
Top Bottom