Yona F. Maro R I P Nov 2, 2006 4,202 218 Nov 13, 2008 #1 nimeanzisha thread ya mashairi ya nyimbo ya zamani tujitahidi kuweka mpaka audio kama inawezekana
Yona F. Maro R I P Nov 2, 2006 4,202 218 Nov 13, 2008 Thread starter #2 [Mwanameka -Dar International(Marijani)] [Wote] Kweli penzi eee, penzi lavunja udugu Watu wakakorofishana, wakakosa kusikilizana Penzi lavunja unyumba eee, nimeyaona kwa Musa Mwanameka umeleta maneno, umeuvunja unyumba kwa Musa Mwanameka eeee, Mwanameka jirani yangu Mimi naona vibaya....... Umemponza mamaye , umemponza mwenzio Mwanameka umeleta maneno, umeuvunja unyumba kwa Musa Uliposikia eee, kwamba Musa ameoa Kaoa mke wa ndoa....... Musa sasa katulia eee, uhuni kaweka kando Ukatumia kila uwezo, kuyabadili mawazo ya Musa Watambua eee,ukifusa(?) urembo Ukazidisha na mapambo, vipini wanja kwa poda eee Na mwendo wako maringo... Musa macho yake yameona, na moyo ukaanza sononeka Ukabadili na njia eee. lazima upite kwa Musa Ukenda sokoni kwa Musa.... Musa amevumilia eee, mwisho kapotea njia Kakusimamisha bila kutambua, akazungumza neno la mapenzi Ulipopata kauli yake, ukakubali bila kusita Uliyotaka yamekuwa...... Kazi ikawa ni moja, ni mapenzi motomoto Umempa pendo lenye huba, maneno matamu kama asali Ukichanganya na urembo wako, Musa kanasa kwenye ulimbo Akili zake zimemruka... Kwako wala habanduki, kwa mkewe hakumbuki Amekwisha ionja asali, anataka kuchonga mzinga Penzi nalo eee, penzi nalo halina siri Na siri si ya watu wawili... Mkewe Musa katambua, naye kadai talaka Hakuliki wala hakulaliki, mpaka Musa katoa talaka Baada ya kisa eeee, Mwanameka umefanya mkasa Kweli wanisikitisha.... Mara Musa humtaki, hata kumuona hupendi Jama Musa ameumbuka, kakosa mwana na maji ya moto Kweli penzi eee, penzi lavunja udugu Watu wakakorofishana, wakakosa kusikilizana Penzi lavunja unyumba eee, nimeyaona kwa Musa Mimi sasa nimeshaamini, Ibilisi ya mtu ni mtu (Chorus) [Wote] Kweli Mwanameka umefanya madhambi makubwa Mambo ulomfanyia Musa yanasikitisha Eee Mwanameka mkasa uliofanya ni wa mwaka Ooo bwana Musa hatokushau mpaka kufa Tena amekwisha apa mambo ya upuuzi hataki tena Keshaumwa na nyoka akiona unyasi anashituka Eee Mwanameka hebu punguza matata [Marijani] Mwanameka umetuachia hadithi mitaani Kila mmoja anashangazwa na vitendo vyako Kila mtu anasimulia mambo yako Ati watu mama wanasema....... [Wote] Mgombanishi.... [Marijani] Kweli watu mama wanasema.... [Wote] Muhuni [Marijani] Ati watu mama wanasema....... [Wote] Mdanganyifu [Marijani] Kweli kweli kweli Mwanameka.... [Wote] Umezidi [Marijani] Oooooooo Mwanameka [Wote] Umezidi [Marijani] Mwanameka umetuachia hadithi mitaani mama aaa [Wote] Kweli mwnameka umefanya madhambi makubwa......... YouTube - Marijani Raajab - Mwanameka
[Mwanameka -Dar International(Marijani)] [Wote] Kweli penzi eee, penzi lavunja udugu Watu wakakorofishana, wakakosa kusikilizana Penzi lavunja unyumba eee, nimeyaona kwa Musa Mwanameka umeleta maneno, umeuvunja unyumba kwa Musa Mwanameka eeee, Mwanameka jirani yangu Mimi naona vibaya....... Umemponza mamaye , umemponza mwenzio Mwanameka umeleta maneno, umeuvunja unyumba kwa Musa Uliposikia eee, kwamba Musa ameoa Kaoa mke wa ndoa....... Musa sasa katulia eee, uhuni kaweka kando Ukatumia kila uwezo, kuyabadili mawazo ya Musa Watambua eee,ukifusa(?) urembo Ukazidisha na mapambo, vipini wanja kwa poda eee Na mwendo wako maringo... Musa macho yake yameona, na moyo ukaanza sononeka Ukabadili na njia eee. lazima upite kwa Musa Ukenda sokoni kwa Musa.... Musa amevumilia eee, mwisho kapotea njia Kakusimamisha bila kutambua, akazungumza neno la mapenzi Ulipopata kauli yake, ukakubali bila kusita Uliyotaka yamekuwa...... Kazi ikawa ni moja, ni mapenzi motomoto Umempa pendo lenye huba, maneno matamu kama asali Ukichanganya na urembo wako, Musa kanasa kwenye ulimbo Akili zake zimemruka... Kwako wala habanduki, kwa mkewe hakumbuki Amekwisha ionja asali, anataka kuchonga mzinga Penzi nalo eee, penzi nalo halina siri Na siri si ya watu wawili... Mkewe Musa katambua, naye kadai talaka Hakuliki wala hakulaliki, mpaka Musa katoa talaka Baada ya kisa eeee, Mwanameka umefanya mkasa Kweli wanisikitisha.... Mara Musa humtaki, hata kumuona hupendi Jama Musa ameumbuka, kakosa mwana na maji ya moto Kweli penzi eee, penzi lavunja udugu Watu wakakorofishana, wakakosa kusikilizana Penzi lavunja unyumba eee, nimeyaona kwa Musa Mimi sasa nimeshaamini, Ibilisi ya mtu ni mtu (Chorus) [Wote] Kweli Mwanameka umefanya madhambi makubwa Mambo ulomfanyia Musa yanasikitisha Eee Mwanameka mkasa uliofanya ni wa mwaka Ooo bwana Musa hatokushau mpaka kufa Tena amekwisha apa mambo ya upuuzi hataki tena Keshaumwa na nyoka akiona unyasi anashituka Eee Mwanameka hebu punguza matata [Marijani] Mwanameka umetuachia hadithi mitaani Kila mmoja anashangazwa na vitendo vyako Kila mtu anasimulia mambo yako Ati watu mama wanasema....... [Wote] Mgombanishi.... [Marijani] Kweli watu mama wanasema.... [Wote] Muhuni [Marijani] Ati watu mama wanasema....... [Wote] Mdanganyifu [Marijani] Kweli kweli kweli Mwanameka.... [Wote] Umezidi [Marijani] Oooooooo Mwanameka [Wote] Umezidi [Marijani] Mwanameka umetuachia hadithi mitaani mama aaa [Wote] Kweli mwnameka umefanya madhambi makubwa......... YouTube - Marijani Raajab - Mwanameka