Unakumbuka hizi

[Mwanameka -Dar International(Marijani)]



[Wote]

Kweli penzi eee, penzi lavunja udugu

Watu wakakorofishana, wakakosa kusikilizana

Penzi lavunja unyumba eee, nimeyaona kwa Musa

Mwanameka umeleta maneno, umeuvunja unyumba kwa Musa



Mwanameka eeee, Mwanameka jirani yangu

Mimi naona vibaya.......

Umemponza mamaye , umemponza mwenzio

Mwanameka umeleta maneno, umeuvunja unyumba kwa Musa



Uliposikia eee, kwamba Musa ameoa

Kaoa mke wa ndoa.......

Musa sasa katulia eee, uhuni kaweka kando

Ukatumia kila uwezo, kuyabadili mawazo ya Musa



Watambua eee,ukifusa(?) urembo

Ukazidisha na mapambo, vipini wanja kwa poda eee

Na mwendo wako maringo...

Musa macho yake yameona, na moyo ukaanza sononeka



Ukabadili na njia eee. lazima upite kwa Musa

Ukenda sokoni kwa Musa....

Musa amevumilia eee, mwisho kapotea njia

Kakusimamisha bila kutambua, akazungumza neno la mapenzi



Ulipopata kauli yake, ukakubali bila kusita

Uliyotaka yamekuwa......

Kazi ikawa ni moja, ni mapenzi motomoto

Umempa pendo lenye huba, maneno matamu kama asali



Ukichanganya na urembo wako, Musa kanasa kwenye ulimbo

Akili zake zimemruka...

Kwako wala habanduki, kwa mkewe hakumbuki

Amekwisha ionja asali, anataka kuchonga mzinga



Penzi nalo eee, penzi nalo halina siri

Na siri si ya watu wawili...

Mkewe Musa katambua, naye kadai talaka

Hakuliki wala hakulaliki, mpaka Musa katoa talaka



Baada ya kisa eeee, Mwanameka umefanya mkasa

Kweli wanisikitisha....

Mara Musa humtaki, hata kumuona hupendi

Jama Musa ameumbuka, kakosa mwana na maji ya moto



Kweli penzi eee, penzi lavunja udugu

Watu wakakorofishana, wakakosa kusikilizana

Penzi lavunja unyumba eee, nimeyaona kwa Musa

Mimi sasa nimeshaamini, Ibilisi ya mtu ni mtu



(Chorus)



[Wote]

Kweli Mwanameka umefanya madhambi makubwa

Mambo ulomfanyia Musa yanasikitisha

Eee Mwanameka mkasa uliofanya ni wa mwaka

Ooo bwana Musa hatokushau mpaka kufa

Tena amekwisha apa mambo ya upuuzi hataki tena

Keshaumwa na nyoka akiona unyasi anashituka

Eee Mwanameka hebu punguza matata



[Marijani]

Mwanameka umetuachia hadithi mitaani

Kila mmoja anashangazwa na vitendo vyako

Kila mtu anasimulia mambo yako

Ati watu mama wanasema.......



[Wote]

Mgombanishi....

[Marijani]

Kweli watu mama wanasema....

[Wote]

Muhuni

[Marijani]

Ati watu mama wanasema.......

[Wote]

Mdanganyifu

[Marijani]

Kweli kweli kweli Mwanameka....

[Wote]

Umezidi

[Marijani]

Oooooooo Mwanameka

[Wote]

Umezidi

[Marijani]

Mwanameka umetuachia hadithi mitaani mama aaa

[Wote]

Kweli mwnameka umefanya madhambi makubwa.........

YouTube - Marijani Raajab - Mwanameka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom