Unakaribishwa kuunda kabila jipya

Unakaribishwa kuunda kabila jipya

kwamtoro

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2010
Posts
4,922
Reaction score
3,244
Nimetafakari kwa kina na kutambua kwamba kuna uwezekano wa kuunda kabila jipya.

Nakaribisha Pm kwa yeyote atakaye amua kuasi kabila lake ili ajiunge na mimi kuunda kabila letu jipya ambayo tutaitengenezea lugha mpya.

Ikiwezekana tutakula viapo vya kuasi majina ya koo za makabila yetu na kupeana majina ya ukoo wetu mpya kutokana na kabila letu.Kama wewe unajuta kuzaliwa kabila ulilo nalo, njoo ujachelewa. Mila na desturi tutaziunda Watu tukitimia 100 ndio mchakato rasmi utaanza.

Kila mtu atakuwa na wajibu wa kutuletea maneno 50 ya atakayo penda kitu gani kiitwe vipi katika kutengeneza lugha.

NB- Hii kabila mkoa wake utakuwa hapa hapa Dar es Salaam
 
Hii itakuwa kitu ya Arusha au Malawi.
 
Hii itakuwa kitu ya Arusha au Malawi.

Yuko sawa. Hii inawafaa zaidi wale waluozaliwa kwenye muunganiko wa kabila nyingi. kwa mfano baba awe ni muungano wa kabila A na mama ni kabila B. Basi mtoto atakayezaliwa atakuwa ni wa kabila AB. Huyu mtoto ambaye sasa ni wa kabila AB akioana na mwenzake wa kabila tuseme C kwa baba na tuseme D kwa mama basi mtoto hapa atakuwa ni kabila CD.

Sasa watoto hawa wa miungano wa kabila AB na CD wakioana watazaa mtoto wa kabila jipya la ABCD. Sasa huyu naye akikitana na wa namna hii wakazaa mtoto, aiasee hyu atakuwa ndiye anayefaa kuwa mteja wako wa kwanza.
 
Hii itakuwa kitu ya Arusha au Malawi.
mkuu unamaanisha si yeye anayesema haya ila nguvu fulani..........!mkuu Katavi leo barcelona wanataka wabadili mto utiririke kuelekea mlimani!!!usikose.
 
Last edited by a moderator:
Mi nipo tayari kuungana na wewe ktk kuanzisha hilo kabila jipya, ngoja nikupm mkuu!
 
Hii itakuwa kitu ya Arusha au Malawi.

Yuko sawa. Hii inawafaa zaidi wale waluozaliwa kwenye muunganiko wa kabila nyingi. kwa mfano baba awe ni muungano wa kabila A na mama ni kabila B. Basi mtoto atakayezaliwa atakuwa ni wa kabila AB. Huyu mtoto ambaye sasa ni wa kabila AB akioana na mwenzake wa kabila tuseme C kwa baba na tuseme D kwa mama basi mtoto hapa atakuwa ni kabila CD.

Sasa watoto hawa wa miungano wa kabila AB na CD wakioana watazaa mtoto wa kabila jipya la ABCD. Sasa huyu naye akikitana na wa namna hii wakazaa mtoto, aiasee hyu atakuwa ndiye anayefaa kuwa mteja wako wa kwanza.
 
Mi pia nipo.
Nijumuishe katika hilo kabila!!
 
yani nikuambie kitu hata mjipange vp hamtaweza, may be muwe watu kumi mkae eneo la peke yenu alafu mletewe watoto ambao bado hawajaanza kuongea, ndiyo muanze wamezesha hizo sumu zenu za lugha mpya mtaweza ila napo mtachemka maana hawa watoto watakuwa wakianza muingiliano na jamii nyingine watasahau hiyo lugha hivyo basi, hapo ndiyo itakuwa mwisho wa lugha.
 
Ndo mambo ya kuingia msituni yanaanzaga hivi hivi .....
baadaye mtataka kuunda taifa jipya.......
baada ya hapo mtataka rais na serikali yenu na katiba yenu.....baadaye kinanuka .............
 
nimecheka sana, naomba kuuliza hivi humu jf kuna wanachama wa freemason?, napia kunawatu wanaamini ushirkina.

kwa kweli sijui, ila najua kwenye wengi kuna mengi
 
Nimetafakari kwa kina na kutambua kwamba kuna uwezekano wa kuunda kabila jipya.

Nakaribisha Pm kwa yeyote atakaye amua kuasi kabila lake ili ajiunge na mimi kuunda kabila letu jipya ambayo tutaitengenezea lugha mpya.

Ikiwezekana tutakula viapo vya kuasi majina ya koo za makabila yetu na kupeana majina ya ukoo wetu mpya kutokana na kabila letu.Kama wewe unajuta kuzaliwa kabila ulilo nalo, njoo ujachelewa. Mila na desturi tutaziunda Watu tukitimia 100 ndio mchakato rasmi utaanza.

Kila mtu atakuwa na wajibu wa kutuletea majina 50 ya atakayo penda kitu gani kiitwe vipi katika kutengeneza lugha.

NB- Hii kabila mkoa wake utakuwa hapa hapa Dar es Salaam

Mkuu kwamtoro nimeipenda id yako vipi ni kweli unatokea pande za kwamtoro
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom