Unahitaji Greenhouse ya Chuma (Steel)

Unahitaji Greenhouse ya Chuma (Steel)

Kilimo Kwanza asante kwa taarifa muhimu. Ni kweli kilimo cha greenhouse kinalipa sana, kwa sababu tija ni kubwa mno! Lakini ni vizuri pia watu waelewe kwamba greenhouse haziwezi kufanya kazi Dar na maeneo mengine ya Pwani kutokana na joto kali na humidity. Greenhouse inakubali kwenye maeneo ya Altitude kuanzia 900m, lakini pia joto lisiwe juu ya 27. Kuna namna ambayo unaweza kufanya greenhouse ifanye kazi Dar, lakini ni high tech, kwa sasa hatuwezi. Watu wengi wa Dar walihamasishwa kununua greenhouse, na wakafanya hivyo. Matokeo yake walipata hasara kubwa, kwa sababu hawakuvuna hata robo ya robo waliyotarajia. Nawafahamu zaidi ya watu 140 waliofunga greenhouse, na sasa wamepata hasara kubwa, wanalia!!. Kitaalam, haishauriwi hata kidogo kufunga greenhouse Dar na Pwani. Ni costfful na painful experience.
 
Kilimo Kwanza asante kwa taarifa muhimu. Ni kweli kilimo cha greenhouse kinalipa sana, kwa sababu tija ni kubwa mno! Lakini ni vizuri pia watu waelewe kwamba greenhouse haziwezi kufanya kazi Dar na maeneo mengine ya Pwani kutokana na joto kali na humidity. Greenhouse inakubali kwenye maeneo ya Altitude kuanzia 900m, lakini pia joto lisiwe juu ya 27. Kuna namna ambayo unaweza kufanya greenhouse ifanye kazi Dar, lakini ni high tech, kwa sasa hatuwezi. Watu wengi wa Dar walihamasishwa kununua greenhouse, na wakafanya hivyo. Matokeo yake walipata hasara kubwa, kwa sababu hawakuvuna hata robo ya robo waliyotarajia. Nawafahamu zaidi ya watu 140 waliofunga greenhouse, na sasa wamepata hasara kubwa, wanalia!!. Kitaalam, haishauriwi hata kidogo kufunga greenhouse Dar na Pwani. Ni costfful na painful experience.


Mkuu.. Turbulence, unachokisema kilishasemwa na company moja hivi ya kilimo hapo Dar, walifanya hiyo research na wakatoa hayo majibu. Kikubwa ninacho faham kuhusu hiyo company wao ndio wanao uza greenhouse zisizofaa kwa mazingira ya Dar, na mikoa ya pwani kiujumla. Mteja niliyesema nilimtembelea kigamboni alifungiwa greenhouse fupi sana, isiyo ruhusu hewa kuzunguka na kutoka nje, alipoenda kulalamika ofisini kwao walikiri kwamba alikosea kumfungia hiyo greenhouse na wamemuhaidi kumpa ambayo ni ndefu na inayo ruhusu hewa kutoa nje.

Unavyosema kuna watu wengi unao wafaham walio fungiwa greenhouse na wamepata hasara, pia wapo wengi tunao wafahamu walio jenga greenhouse hapo Dar na Pwani na wamepata faida. Kiujumla biashara unayosema wewe haikufai kwa mwingine yeye ndio inayo mfaa tena na kumtajirisha, sasa kama kila biashara ingekuwa ni rahisi kufanya basi kila mtu huku Dar angekuwa mfanyabiashara, unahitaji kuwa jasiri na kumaanisha katika unachokifanya tu.

Tumeangalia hilo tatizo la joto na humudity(unyevu) mikoa ya pwani, na kulitatua kwa kujenga greenhouse inayo ruhusu hewa kuzunguka, joto na unyevu kutokaa ndani. Kimsingi greenhouse kwa mikoa ya pwani inatakiwa kuzuia wadudu na kupunguza jua kali, na siyo kutunza joto na unyevu ndani, hivyo nyumba inatengenezwa kuzingatia hayo. Mimea inayopandwa kwenye greenhouse hizi inaweza kuhimili mpaka nyuzi joto 33.
 
Kilimo Kwanza: Kuna utafiti umefanywa na Wizara ya Kilimo na mashirika mengine kuhusiana na matumizi ya greenhouse Dar. Majibu ni kwamba hazifai, labda ziwe special sana. Unaweza kuvuna kidogo ukilima wakati wa baridi kama huu, lakini nyakati nyingine zote za mwaka hazifai kabisa. Kama wewe ni mtaalam, sina shaka kuwa moyoni mwako unaujua huu ukweli. Kuna watu wanatumia ignorance ya watu kuhusiana na hiyo teknolojia, na desperation ya watu kupata pesa ya haraka na kuwadanganya kuwa ati greeenhouse inaweza kufanya kazi vizuri Dar. Kisha wanawauzia, when things fall apart wanakimbia. Huu ni UTAPELI, UDANGANYIFU na TAMAA. Natumai haumo kwenye hili kundi. Ningekuelewa kama unge-promote teknolojia ya "Net", hiyo sawa inafanya kazi vizuri sana Dar na Zanzibar. Greenhouse zitumike maeneo stahili: Moshi, Arusha, Mwanza, etc etc. Greenhouse ni kilimo kinachoweza kubadili maisha ya mkulima, lakini bahati mbaya, mazingira ya dar hayafai kwa hii teknolojia. Huo ndio ukweli
 
Je huku nzega tabora green house inaweza kufanya kazi vizuri
Nina mpango wa kuitafuta
 
Kilimo Kwanza: Kuna utafiti umefanywa na Wizara ya Kilimo na mashirika mengine kuhusiana na matumizi ya greenhouse Dar. Majibu ni kwamba hazifai, labda ziwe special sana. Unaweza kuvuna kidogo ukilima wakati wa baridi kama huu, lakini nyakati nyingine zote za mwaka hazifai kabisa. Kama wewe ni mtaalam, sina shaka kuwa moyoni mwako unaujua huu ukweli. Kuna watu wanatumia ignorance ya watu kuhusiana na hiyo teknolojia, na desperation ya watu kupata pesa ya haraka na kuwadanganya kuwa ati greeenhouse inaweza kufanya kazi vizuri Dar. Kisha wanawauzia, when things fall apart wanakimbia. Huu ni UTAPELI, UDANGANYIFU na TAMAA. Natumai haumo kwenye hili kundi. Ningekuelewa kama unge-promote teknolojia ya "Net", hiyo sawa inafanya kazi vizuri sana Dar na Zanzibar. Greenhouse zitumike maeneo stahili: Moshi, Arusha, Mwanza, etc etc. Greenhouse ni kilimo kinachoweza kubadili maisha ya mkulima, lakini bahati mbaya, mazingira ya dar hayafai kwa hii teknolojia. Huo ndio ukweli

Turbulence.. nashukuru kwa maoni yako, karibu utembele kazi zetu.
 
2015-03-16 10.21.04.jpg hoho.jpg nyanya.jpg
 
kilimo kwanza nisaidie wapi na kwabei gani nawezapata drip Irigation system utayotosha eka moja
 
kilimo kwanza nisaidie wapi na kwabei gani nawezapata drip Irigation system utayotosha eka moja

Mkuu Araway... tunaweza kukupatia drip irrigation system pamoja na kukufungia pia, ila ni muhimu kutembelea shamba kwanza ili kufaham layout kabla hatujakupa gharama, pia tutahitaji kujua aina ya zao utakalo panda, na source ya maji imekaa vp, mengine kama hayo, tuwasiliane tukusaidie maelezo vizuri zaidi.
 
Unahitaji Greenhouse Ya Chuma(Steel)

  1. Total galvanized jstructure
  2. Width - 8mtr
  3. Length - 15mtr
  4. Gutter/Shoulder height - 3.0mtr
  5. Center height - 4.5mtr
  6. Entrance Door - 1mtr Width by 2mtr Height
  7. Poly film - 200 microns, anti-drip and anti-mist effect
  8. HDPE Insect net – 80gsm
  9. Mesh size – 32mesh
  10. Drip line - 16mm diameter with Filter
  11. Foundation depth - 2.5feet
  12. Wind speed capacity - 120kmh

[TABLE="class: grid, width: 500, align: center"]
[TR]
[TD]Area
[/TD]
[TD]120sqm[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Tomato Spacing[/TD]
[TD]20cm by 40cm[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Plants[/TD]
[TD]800[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Minimum Output[/TD]
[TD]15kg[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Average Price Per Box (40kg)[/TD]
[TD]Shs 30,000/=[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Total Cost of Production - 7 Month[/TD]
[TD]Shs 600,000/=[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Greenhouse Construction[/TD]
[TD]Shs 6,000,000/=[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Gross Revenue[/TD]
[TD]Shs 9,000,000/=[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Net Profit First Season[/TD]
[TD]Shs 2,400,000/=[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Net Profit Second Season[/TD]
[TD]Shs 8,000,000/=[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Net Profit Third Season[/TD]
[TD]Shs 8,000,000/=[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Inclusive: Pesticides, Fertilizers, Training, Support for First Season, Spray and Fertilizer Programme

NB:
The client should be responsibility to deliver water into the greenhouse
The water pump and water source should be supplied by client

Call us on 0683-644-480

Mkuu tunakushukuru kwa kuleta hoja Ya maendeleo....na maswali kidogo
1. Ipo green house ya mfano ambayo mazao yameshakomaa?
2. Kuna jamaa yumo humu anaitwa greenhouse au abdullatif na yule jamaa wa amka na badilika. . Je unauhusiano nao?
3. naomba mchanganuo wa kulima hoho kwenye green house hii.
4. Unaweza nipatia makadirio ya kufunga drip kwenye shamba tambarare la ekari moja kwa mkoa wa moshi
5. Na mwisho gharama hizo zinaapply hadi nje ya dsm ... mfano moshi inakuwa bei gani...
 
Naam:
1. Kwa sasa greenhouse zote tulizo jenga hapa dodoma, miche yake ina miezi miwili hadi mitatu, ikifika july nitaweka picha za hizo greenhouse zote maaana ndipo itakuwa mavuno.
2. Ndio namfaham huyo mtu ila hatuna mausiano naye wala hatufanyi kazi naye pamoja.
3. Kuhusu mchanganuo wa kulima hoho kwenye greenhouse upo ulioandaliwa vizuri, unaweza ni PM email yako nikakutumia ila kwa faida ya wengi nita summarize kidogo.
Ndani ya GH ya 8x15=120sqm utapanda miche 540, kila mche unaweza kukupatia wastani wa kilo 5, hivyo kufanya jumla ya kilo 2700, kama kila kilo utauza kwa bei ya wastani wa shs 3000, hivyo jumla kuu ya mauzo ni shs 8,100,000/=
4. Hii inategemea sana na shamba lako lilipo, ni vyema kufika shambani kwanza na kuona kisha tutakakupatia bei halisi, makadirio unayo niuliza sii halisi, yanaweza kupungua au kuzidi pia, ila wastani shs 4mil kwa hekari moja inaweza kutosha kabisa.
5. Hizo gharama ni kwa hapa dodoma, nje ya mko wa dodoma tunaweza kuongea na kuangalia ni jinsi gani gharama zitakuwa, maana upatikanani wa materials na kusafirisha unatofautiana gharama.

Karibu sana mkuu.
 
Kilimo Kwanza: Kuna utafiti umefanywa na Wizara ya Kilimo na mashirika mengine kuhusiana na matumizi ya greenhouse Dar. Majibu ni kwamba hazifai, labda ziwe special sana. Unaweza kuvuna kidogo ukilima wakati wa baridi kama huu, lakini nyakati nyingine zote za mwaka hazifai kabisa. Kama wewe ni mtaalam, sina shaka kuwa moyoni mwako unaujua huu ukweli. Kuna watu wanatumia ignorance ya watu kuhusiana na hiyo teknolojia, na desperation ya watu kupata pesa ya haraka na kuwadanganya kuwa ati greeenhouse inaweza kufanya kazi vizuri Dar. Kisha wanawauzia, when things fall apart wanakimbia. Huu ni UTAPELI, UDANGANYIFU na TAMAA. Natumai haumo kwenye hili kundi. Ningekuelewa kama unge-promote teknolojia ya "Net", hiyo sawa inafanya kazi vizuri sana Dar na Zanzibar. Greenhouse zitumike maeneo stahili: Moshi, Arusha, Mwanza, etc etc. Greenhouse ni kilimo kinachoweza kubadili maisha ya mkulima, lakini bahati mbaya, mazingira ya dar hayafai kwa hii teknolojia. Huo ndio ukweli
Kwa Dar IPI inafaa?.na hyo yaNET inafanyikaje?
 
Ohhk.... kwahio kama zanzibar greenhouse gani inafaa?? Na hio inayofaa inaweza cost shillingi ngapi tafadhali msaada kwa hapo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom