mgeni wenu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 3,664
- 1,731
Wana JF kama mnakumbuka baada ya uchaguzi wa Igunga kuna kada wa CHADEMA aliuwawa na mwili wake kuokotwa baadaye ukiwa umeoza na hata kutotambulika kwa Urahisi,Baadaye Uchaguzi wa Arumeru Aliuwawa Msafiri Mbwambo(Mwenyekiti wa Chadema USA RIVER)kwa kukatwa Shingo kwa msumeno wa engine ya Mnyororo(chain Saw)tena wauaji wakisaidiwa na viongozi wa CCM ambao walikamatwa na kutoroka mikononi mwa Polisi(kwa Msaada wa Viongozi wa CCM na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani)
Sikuona Bunge kusimama na kuunda tume,pia walikufa Waandamanaji(Chadema)kwa kuuwawa na Polisi Arusha Bunge lilikuwa kimya na hakuna aliyeinuka kusema,pia waliuwawa watu Kwa Bomu Olasiti(Arusha)kwa mipango michafu ya wana CCM hakuna aliyesema,Wabunge wa Chadema wakiwa wakipigwa na Kunyanyaswa na Polisi,hakuna aliyetakiwa kuwajibika,.
Kwenye Mkutano wa Chadema Soweto(arusha)walikufa Wana Chadema na watoto wadogo kwa kupigwa Risasi na polisi hiyo hawakuona Ila Majangiri ambao wana Mahusiano na wabunge wa CCM walipoguswa na mifugo ya Wakubwa kuguswa imebidi Baraza livunjwe na Wapo wanaotaka Pinda pia atimuliwe,
HUU NI UNAFIKI WA BUNGE...
Sikuona Bunge kusimama na kuunda tume,pia walikufa Waandamanaji(Chadema)kwa kuuwawa na Polisi Arusha Bunge lilikuwa kimya na hakuna aliyeinuka kusema,pia waliuwawa watu Kwa Bomu Olasiti(Arusha)kwa mipango michafu ya wana CCM hakuna aliyesema,Wabunge wa Chadema wakiwa wakipigwa na Kunyanyaswa na Polisi,hakuna aliyetakiwa kuwajibika,.
Kwenye Mkutano wa Chadema Soweto(arusha)walikufa Wana Chadema na watoto wadogo kwa kupigwa Risasi na polisi hiyo hawakuona Ila Majangiri ambao wana Mahusiano na wabunge wa CCM walipoguswa na mifugo ya Wakubwa kuguswa imebidi Baraza livunjwe na Wapo wanaotaka Pinda pia atimuliwe,
HUU NI UNAFIKI WA BUNGE...