Unafiki wa viongozi mkoa wa Arusha

Unafiki wa viongozi mkoa wa Arusha

Chiluba

Member
Joined
Nov 8, 2007
Posts
51
Reaction score
7
Huku wananchi wa kawaida wanaoishi maeneo ya Moshono hadi kilipo chuo kikuu cha Nelson Mandela mkoani Arusha, wakitaabika kwa vumbi jingi na barabara mbovu, imekuwa ni kawaida kwa Uongozi wa Mkoa na TANROAD mkoani hapa kufanya marekebisho ya barabara hiyo pale tuu wanaposikia kuna ugeni wa mmoja wa viongozi wakubwa anaetegemewa kutumia barabara hiyo. Kwa Mara ya mwisho barabara hii ilipitishwa grader na kumwagwa vifusi mwaka Jana 2012, Rais alipokwenda kufungua rasmi Chuo cha Nelson Mandela.
Baada ya muda mfupi barabara hiyo imekuwa na mashimo mengi na vumbi jingi sanaaa na kuwa kero kubwa kwa wananchi wanaoishi pembezoni na hata wafanyakazi wa Chuo hiki kipya, hilo halikuonekana kama tatizo kwa viongozi wa Mkoa wa Arusha.
Baada ya Kusikikia Waziri Mkuu Pinda, atafanya ziara katika chuo hicho kesho tar 31/01/13, kuanzia jana na leo barabara hyo imeanza kusawazishwa na hata kunyunyuziwa maji kuondo vumbi.
Watu wanajiuliza, JEE UONGOZI WA MKOA UPO KWA AJILI YA KUWAFURAHISHA JK NA PINDA AU KUWATUMIKIA WANANCHI WA MKOA HUU??? KAMA TATIZO NI PESA, HIZI ZA KUREKEBISHA KIPINDI CHA UGENI WAO KINATOKA WAPI? NI FUNGU LA RAIS NA WAZIRI MKUU AU? KWA NINI HALI ISIACHWE KAMA ILIVYO ILI NAO WAJIONEE MATATIZO YA WANANCHI???
 
Wabunge husika wakalijadili hilo kwenye vikao vyao vya wilaya na mkoa-arusha ni kati ya mikoa ambayo barabara za ndani zinajengwa kwa kasi sana.naamini hata hiyo barabara ikisimamiwa itajengwa,kikubwa mbunge husika aiingize katika mpango wa halmashauri yake.
 
Wabunge husika wakalijadili hilo kwenye vikao vyao vya wilaya na mkoa-arusha ni kati ya mikoa ambayo barabara za ndani zinajengwa kwa kasi sana.naamini hata hiyo barabara ikisimamiwa itajengwa,kikubwa mbunge husika aiingize katika mpango wa halmashauri yake.

Mkuu,barabara zinazojengwa kwa sasa zote ni mpango na hela ya Benki ya Dunia..hoja hapa si kuwepo au kujadiliwa kwenye vikao vya wilaya, suala la msingi ni barabara kutengenezwa kipindi cha ziara za Viongozi tuuu..hii maaana yake ni kwamba bila kutembelewa na kiongozi barabara hazitengenezwi??..yeye anapita kwa siku moja tuu,inatengenezwa! wananchi wa kawaida wanaitumia kila siku haitengenezwi ndio hoja ya msingi hapo!
 
Tabia hii siyo Arachugga tu, ndo mtindo wa siku zote , sehemu yeyote hapa Bongoland.
Mbona mgeni wako (manzi ako) akija home unafanya usafi!
 
Inanikumbusha enzi za shule kabla ya mgeni kufika tulikuwa tunafagia njia zote na kupaka mawe chokaa,
 
Back
Top Bottom