Unafahamu nini kuhusu wachina?

Unafahamu nini kuhusu wachina?

Paul dybala

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2023
Posts
553
Reaction score
2,266
Wachina ni wachapakazi sana, wabahili sana, wambea sana, wanapenda sana sigara lakini pia ni wezi sana.

Ukipata kazi kwa wachina ujue utafanya kazi kweli kweli, iwe ni kiwandani, barabarani au popote pale. Kuna siku nilikuwa na boss wangu tukawa tunatafuta sehemu ya kuweka machine za dubwi, bilikuwa kazi ngumu kushawishi mtu akubali dubwi kwa sababu wengi wa wateja wanakataa wanasema dubwi linaleta wezi na mimi muda huo nimetafuta sehemu 20 tokea asubuhi hadi muda huo usiku na hatujala bhasi akawa hajaridhika akanioneshe nikaulizie tuweke dubwi salon ya kike eti nikimshawishi mteja ananipa 5000.

Aisee nilimuangalia sana halafu sikufanya kitu nikazama kwenye waleti nikatoa 20000 nikamwambia aendee yeye wakikubali nitampa hio 20000 kisha nikalaza siti ya gari nikalala, alitoa macho alishangaa nimepata wapi ujasiri. Tokea siku hio hakuwahi nituma kazi ya kijinga.

Ubahili wao ni mkubwa jamaa hawabadi nguo kila siku ni hiohio, kingine mchina usimpe siri yako.
 
Wachina ni watu wenye akili sana wanajitambua na kutambua historia yao inaitwa century of humiliation.

Wachina ni wafanya kazi sana.

Serikali yao inafanya kazi sana na inawapenda wachina sana hii nimeshuhudia mwenyewe ni kwamba wanafahamu kwa nini wapo madarakani na wanajua consequences za wao kutokuwa madarakani kwa China.

Wana miundombinu mingi mizuri.
 
Wachina ni watu wenye akili sana wanajitambua na kutambua historia yao inaitwa century of humiliation.

Wachina ni wafanya kazi sana.

Serikali yao inafanya kazi sana na inawapenda wachina sana hii nimeshuhudia mwenyewe ni kwamba wanafahamu kwa nini wapo madarakani na wanajua consequences za wao kutokuwa madarakani kwa China.

Wana miundombinu mingi mizuri.
Nafanya kaz na wachina Kwa kweli sifa hizo zote wanazo sigara ndio kama chakula kwao uwambii kitu kasoro wanawake Tu sjawai ona wakivuta
 
Kitu kimoja nachopenda toka kwao serikali yao inafanya kazi kubwa na kwao siasa sio uwanja wa maonesho ya vichaa kama ilivyo katika nchi nyingi kwetu huku Africa.

China siasa na uongozi ni jambo serious sana ma mayors wa maeneo yao mbalimbali wana vision kubwa kweli na wanashindana na muda kutelekeza hizo vision
 
Ukifika China ukaaishi na Tanzania utaona kuwa wengine tunaishi bora liende na kuna wengine wana angalia kesho ya kizazi chao.

Utendaji wa serikali iliyopo China tuchukulie tu mfano manispaa ya mjii wa Chongqing na ukafananisha serikali iliyopo Tanzania utaona kabisa huku tunacheza.
 
Huku mtaani kwetu wnaniita the black chinese
 
Back
Top Bottom