kwa mie mtanzania wa kawaida hata asipoenda nje au kufanya hayo makitu poa tu
Ilimradi nipate maji, madawa, umeme, elimu bora na huduma nyingine za kijamii
....Magufuli si diplomat....hivyo sitegemei kumwona akisafiri sana nje ya nchi....haswa huko ulaya na marekani wanakotupatia misaada...ila ikibidi awepo huko namwona akiwatumia zaidi ma diplomats atakaowachagua...haswa waziri wa mambo ya nje....Katika kujenga mahusiano na nchi za nje...naona hili Magufuli halitamsumbua sana .....maana tayari JK hii ndio ilikua agenda yake iliyomfanya mtembezi wa dunia...
....katika kukuza viwanda...namwona JPM atashughulika sana na asia...haswa china...katika kuvuta uwekezaji wa wachina TZ...
...labda akiwa makini JPM anaweza kuchukua model ya ethiopia...pale ambapo wao wamevutia wachina kuwajengea special economic zones kule ethiopia....jambo ambalo ni bora sana na halihitaji utembezi wa rais nje....maana wao wawekezaji ndio wanavutika kuja africa kuwekeza..na si viongozi wetu kushinda kwao wakitembeza bakuli....
Cha msingi ni kutimiza ahadi zake alizowaahidi watanzania ili awe kiongozi bora kuliko wengine waliomtangulia. Safari sio issue sana as long as aliyepita alitembea sana kuimarisha uhusiano wa nchi yetu na mataifa ya nje.