Unabii wa TB Joshua watimia

Unabii wa TB Joshua watimia

Ambae haamin na anataka kuamin aende akaombewe au kama ua jambo limeshindikana kabisa nenda ukaombewe kama hautafunguliwa unabii na miujiza imezungumzwa sana kwa biblia hivo basi imani ndio msingi mkuu
 
Hana lolote nabii gani huyo,kama kweli yeye ni nabii aoneshe walipo watoto waliotekwa na boko haramu
 
Na bado jpili atatoa unabii mwingine ,lazima utatiki.si unigeria wala nini,kama huamini huamini tu ata hao Wa bongo
 
Hana lolote nabii gani huyo,kama kweli yeye ni nabii aoneshe walipo watoto waliotekwa na boko haramu
Sio kila kitu anatabiri ni mpaka mungu amwoneshe ndipo anatoa utabiri inaonesha wewe hufuatilii mafundisho yake ndo maana huelewi.
 
1. Mgalatia
2. Muongo
3. Tapeli wa kiNigeria


Sent from my iPad Air using JamiiForums



Mkuu huyu nabii anahitajika akawaponye wagonjwa wa ebola kwa kuwashika kichwani!
Aache huu utabir wa kutumia current issues aenda Sierra leone na Guinea
 
Mbona hakutabiri ujio wa Ebola West Africa?. Ilimpita wapi ??
 
Watu wanamfuata mungu kwa ajili ya woga na si kwamba wanampenda mungu bali wanalazimika.
 
Naomba kuuliza.
Tuchukulie mfano kuwa ni kweli jamaa anatabiri vitu na hutokea. Hii ina mantiki gani kwangu kama binadamu mkristo (au hata muislam)?
Maana kama ni kubashiri mwisho wa dunia na hivyo tujiandae wengi wenu mtakua wanafiki tu maana maandalizi yenu ni ya woga na wala si ya dhati ya kupenda kufwata njia ya Mungu.
Swala mwisho wa dunia na utabiri halitakiwi kumshtua hata punje muumini wa kweli wa hayo madhehebu yenu.

TB Joshua ni mfwatiliaji mzuri na wa kina sana katika mambo ya dunia. Kuanzia politics mpaka tabia nchi. Anachofanya ni intelligent guesswork tu navyoona mimi, bado sijaamini kama ana extra powers and more specifically from God.

Je ww unaweza fatilia na ukaguess?
 
Hata Elia alibishana na manabii wa Baali. Kukomesha ubishi akawaalika kuthibitisha MUNGU wa kweli hadharani. Akawataka watangulie kumtolea sadaka Mungu wao na ajithibitishe Kwa kuzipokea. Tunajua yaliyotokea. Elia alimwomba MUNGU wake ajithibitishe Kwa kuipokea sadaka yake. MUNGU wa kweli hujithibitisha na huwatuma manabii wake. Tusibishane Wakristo. Matendo huzungumza zaidi. Mtumishi wa MUNGU Joshua anatabiri yanatokea. Kama ni nabii wa MUNGU,wanaobisha tusishinsane nao
.MUNGU wetu hujitetea
 
Haya tenaa, wale wabishi wanabishana na Redio. Hapa tena TB Joshua anathibitika,mwanzo Wa mwaka alisema ombeni kwa ajili ya russia,akasema vita itaibuka kinyume yake ,ata pressure itakuwa kubwa hata italilemea taïfa hilo. Lile nililokua nangojea kuliona ni pale aliposema,mataifa yataungana kupigana na urusi. À ha sasa leo nimeona, Majeshi ya ushirika Wa ulaya (NATO),yamepeleka silaha na kiasi cha askari 4,000 kupigana na urusi.Mungu awasaidie lakini nimeona.

Yeye hajui atakufa lini
 
Hivi yule mrithi wa hayati Sheikh Yahya yupo? Maana hatusikii mbwembwe zake, tofauti ni kwamba Christian wanatabiri kupitia maono ya Mungu, the other side wanatabiri kupitia majini
 
Hivi yule mrithi wa hayati Sheikh Yahya yupo? Maana hatusikii mbwembwe zake, tofauti ni kwamba Christian wanatabiri kupitia maono ya Mungu, the other side wanatabiri kupitia majini

Kwani huu ugonjwa wa kifua kikuu umepata mtoto?
T.B Joshua
 
Kwanini asiombee yasitokee maafa!! Huwa nashindwa kuwaelewa watu mnaowaamini wa-Nigeria, hawa jamaa ni waongo, matapeli, waliotumwa kutafuta pesa Kwa kila njia

Umenena..hivi kama anaweza kutabiri kwa kuona siri za Mungu anashindwaje kuombea Boko Haramu waangamie?
 
Kiasi kwamba unataka kutuaminisha kwamba haufahamu kuwa kuna cold war toka muda mrefu?
Anafanya timing anasema lile amabalo hata watoto wanaweza kuliona litatokea.[/acha wivu
 
Msiba wetu ni kuwa huwa hatusomi historia..
Watu kama huyu walikuwepo tena wenye visa vingi kuliko huyu na pia huyu si wa mwisho watakuja wengine huenda "wazuri" ktk kazi zao kuliko huyu.Hii ndo dunia na haya ndo mambo yake.Kila kitu ni mzunguko wa nyakati na matukio.kila mwenye akili aitumie vyema akili yake.ujinga ni uamuzi na uhuru wa mtu.
Yuko wapi "Babu" wa Loliondo?....(historia ya jana)
 
sasa kama alisema tuwaombee na tukafanya hivyo, mbona yanaendelea kutokea. au hata yeye hakumuomba uyo Mungu wake??
 
Akiiombea wagonjwa wa ebola kwa kuwashika kichwani atajipatia umaarufu wakutosha

Among my favourite posts this year!! avec vous ungeweka namba ya mpesa ningetuma hata wekundu! Hahahahha!! Umenichekesha sana!
 
Back
Top Bottom