"Binafsi sifikirii kukata rufaa, wewe acha tu niende nikaitumikie adhabu ambayo ilishapangwa na watu wasionipenda eti kwa sababu ya kudai jasho la kazi ya mikono yangu, hawajui ni kiasi gani nilivyoweza kupata ile fedha ya mtaji wa biashara."
"Vipi kuhusu biashara yako ya kuokota chupa za maji?
Nadhani ndiyo hivyo imeshakosa mtu wa kuweza kusimamia kwa sababu mke wangu ni mjamzito, hivyo hataweza pilikapilika za kwenda barabarani kuokota chupa, ni jambo gumu sana kwa kweli, naumia lakini sina jinsi." Source -
Global Publishers
Ukweli maneno haya yamenigusa sana, kwa wapenzi wa cheka hamna namna ya kumsaidia huyu mama mja mzito? Mengi/bhakresa huyu mtu alikuwa anafanyakazi ya kuokota machupa yenu ya maji sasa hamna namna ya kumsaidia kweli? binafsi naona kafungwa kwa sababu ya umasikini wake tu. IGP saidi mwema alishawahi kusema Jela sio jehanamu, naamini atarudi tu.