Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Juzi jumamosi nilibahatika kumsindikiza rafiki yangu mmoja kwenda kujitambulisha kwa wazazi wa fiancee wake. Pamoja nami na bwana harusi mtarajiwa, tulikuwa pia na mjomba wa huyo rafiki yangu na kaka yake.
Tulipofika ukweni baada ya kukaribishwa na utambulisho mrefu, kwa kweli ilikuwa ni mjomba wa rafiki yangu kueleza kile kilichotupeleka pale. Na hilo lilipofganyika mbele ya wenyeji wetu ambao walikuwa wakitusubiri wake kwa waume...ndipo aliposimama mzee mmoja ninayemkadiria kuwa na miaka 50 -60 ambaye nilikuja kuambiwa baadaye kuwa ni baba mkubwa wa binti ambaye jamaa anamchumbia kwani baba yake mzazi alishatangulia mbele ya haki.....Kama utani mzee akaanza kumuuliza jamaa maswali ambayo baadhi yetu yalituacha hoi....Mambo yalikuwa kama ifuatavyo;
Mzee: Kijana una kazi?
Jamaa: Ndio mzee mimi ni mhandisi wa kampuni fulani
Mzee: Una nyumba?
Jamaa: Hapana mzee, bado sijabahatika kujenga lakini nina kiwanja tayari
Mzee: Una gari?
Jamaa: Hapana
Mzee: Uliwahi kuoa kabla ya kuja kumchumbia binti yangu?
Jamaa: Hapana
Mzee: Una mtoto uliyezaa huko nyuma?
Jamaa: Kimya kidogo,....baadaye ndio ninaye..
Mzee: Mchumba wako anafahamu hilo?
Jamaa: Hapana..
Mzee: Sasa wewe unataka kumchumbia binti yangu jambo kama hilo humuelezi mwenzio huoni kuwa unatengeneza bomu?...Inaelekea hauko serious wewe na kumuoa huyo msichana nadhani unahitaji kwenda kujipanga upya na ikibidi uzungumze na mwenzio....au unasemaje?
Huwezi kuamini wote tulikuwa kimya....baadae shangazi wa binti akaitwa na binti kusikia tu jamaa ana mtoto nje......mjadala ukawa mrefu lakini hatimaye jamaa alitakiwa kumueleza mchumba wake mbele ya kadamnasi ile ukweli na baadae mambo mengine yakaendelea lakini hali ilikuwa tete sana.....
Tulipofika ukweni baada ya kukaribishwa na utambulisho mrefu, kwa kweli ilikuwa ni mjomba wa rafiki yangu kueleza kile kilichotupeleka pale. Na hilo lilipofganyika mbele ya wenyeji wetu ambao walikuwa wakitusubiri wake kwa waume...ndipo aliposimama mzee mmoja ninayemkadiria kuwa na miaka 50 -60 ambaye nilikuja kuambiwa baadaye kuwa ni baba mkubwa wa binti ambaye jamaa anamchumbia kwani baba yake mzazi alishatangulia mbele ya haki.....Kama utani mzee akaanza kumuuliza jamaa maswali ambayo baadhi yetu yalituacha hoi....Mambo yalikuwa kama ifuatavyo;
Mzee: Kijana una kazi?
Jamaa: Ndio mzee mimi ni mhandisi wa kampuni fulani
Mzee: Una nyumba?
Jamaa: Hapana mzee, bado sijabahatika kujenga lakini nina kiwanja tayari
Mzee: Una gari?
Jamaa: Hapana
Mzee: Uliwahi kuoa kabla ya kuja kumchumbia binti yangu?
Jamaa: Hapana
Mzee: Una mtoto uliyezaa huko nyuma?
Jamaa: Kimya kidogo,....baadaye ndio ninaye..
Mzee: Mchumba wako anafahamu hilo?
Jamaa: Hapana..
Mzee: Sasa wewe unataka kumchumbia binti yangu jambo kama hilo humuelezi mwenzio huoni kuwa unatengeneza bomu?...Inaelekea hauko serious wewe na kumuoa huyo msichana nadhani unahitaji kwenda kujipanga upya na ikibidi uzungumze na mwenzio....au unasemaje?
Huwezi kuamini wote tulikuwa kimya....baadae shangazi wa binti akaitwa na binti kusikia tu jamaa ana mtoto nje......mjadala ukawa mrefu lakini hatimaye jamaa alitakiwa kumueleza mchumba wake mbele ya kadamnasi ile ukweli na baadae mambo mengine yakaendelea lakini hali ilikuwa tete sana.....