UN: Watoto 2,000 waliotumikishwa kijeshi Yemen waliuawa vitani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,505
9,286
1643609747686.png

Ripoti mpya ya wataalam wa Umoja wa Mataifa imeeleza kwamba takriban watoto 2,000 waliosajiliwa na waasi wa Kihouthi wa Yemen kuwa wapiganaji, walifariki vitani, kati ya Januari mwaka 2020 na Mei mwaka 2021.

Ripoti imeeleza zaidi kwamba waasi hao wanaoungwa mkono na Iran, wanaendeleza kambi za kuwasajili na kuwahimiza watoto kushiriki vita.Kwenye ripoti hiyo iliyowasilishwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa jana, wataalam wamesema walichunguza baadhi ya kambi shuleni na vilevile msikiti, ambao Wahouthi hutumia kueneza nadharia zao na kuwasajili watoto.

Wataalam wameeleza kwamba walinakili visa 10, ambapo watoto walipelekwa kupigana, baada ya kuambiwa watasajiliwa katika kozi za tamaduni.Jopo hilo la wataalam limesema lilipokea orodha ya watoto 1, 406 waliokufa vitani mwaka 2020 baada ya kusajiliwa na Wahouthi na vilevile orodha ya watoto 562 waliokufa kati ya Januari mwaka jana hadi Mei mwaka jana.

Vita vya Yemen vimedumu kwa miaka saba sasa.
 
Sisi huku tuna panya road
Kule wana watoto wa ibilisi huko wana watoto wanaobeba ak 47
Kila sehemu na utamaduni wao
 
Back
Top Bottom