Ngamanya Kitangalala
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 501
- 1,214
Kumekuwa na upotoshwaji mkubwa kuhusu ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Chato
Kwa nini uwanja wa ndege Chato????
Ukisoma ilani ya uchaguzi ya CCM mwaka 2015- 2020, imeelekeza ni lazima serikali ichukue hatua za makusudi kukuza sekta ya utalii nchini, ili ifikapo 2020, Tanzania iwe na uwezo wa kupokea watalii wasiopungua 2m kwa mwaka toka watalii 1.2m mwaka 2014, hasa ukizingatia Tanzania ni nchi ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi cha utalii baada ya Brazil
Na ni kwa nini utalii?
Sekta ya utalii Tanzania, ndio sekta inayoongoza katika kuingiza fedha nyingi za kigeni kuliko sekta yeyote ile hapa Tanzania( 25%) ya fedha zote za kigeni( foreign currency) zinatokana na utalii, mfano mwaka 2018/ 2019 sekta hiyo iliingizia taifa takribani $ 2.4 bilioni, pia sekta ya utalii nchini inachangia takribani 17.6% ya pato ghafi la taifa(GDP), pia sekta ya utalii imetoa ajira za moja kwa moja takribani watu elfu sita na ajira zisizo za moja kwa moja takribani watu milioni mbili
Sasa kwa Tanzania ukanda pekee unaofanya vizuri katika utalii ni ukanda wa kaskazini, ambapo unaopokea watalii wengi kuliko kanda zingine za Kusini na Kanda ya Kaskazini magharibi, takribani 90% ya watalii wote wanaoingia hapa nchini wanaelekea ukanda wa Kaskazin
Sasa ili kufikia malengo ya kuongeza idadi ya watalii, serikali waliamua kufungua baadhi ya kanda zingine za za utalii, kanda hizo ni Kanda ya Kusini( mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe,Songwe) ambapo Kitulo ilipandishwa hadhi na kuwa hifadhi ya Kitulo, na kanda ya Kaskazini magharibi yenye mikoa ya ( Geita, Mwanza, Kagera, Kigoma)
Serikali walifanya nini kwa kanda ya Kaskazini magharibi?
Hatua ya kwanza waliofanya, kwanza ni kuyapandisha hadhi mapori tengefu ya Burigi, Biharamulo, Kimisi , Rumanyika & Kyerwa na kuwa hifadhi za taifa( National parks) Burigi- Chato, Rumanyika-Karagwe & Kyerwa
Sasa ili kuweza kuvutia watalii waweze kufika Kwan urahisi katika hifadhi hizo, serikali waliona ipo haja ya kujenga uwanja mkubwa wa kinataifa wa ndege katibu na maeneo hayo, ambapo watalii wataweza kufika kwa urahisi zaidi kuliko ilivyo sasakatika hifadhi hizo ambapo kuna hifadhi ya tatu kwa ukubwa hapa nchini( Burigi- Chato)baada ya Serengeti na Sellou
Kwa hiyo kwa kuzingatia umuhimu wa kukuza sekta ya utalii nchini, ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Chato una manufaa makubwa katika uchumi wetu
Kwa nini uwanja wa ndege Chato????
Ukisoma ilani ya uchaguzi ya CCM mwaka 2015- 2020, imeelekeza ni lazima serikali ichukue hatua za makusudi kukuza sekta ya utalii nchini, ili ifikapo 2020, Tanzania iwe na uwezo wa kupokea watalii wasiopungua 2m kwa mwaka toka watalii 1.2m mwaka 2014, hasa ukizingatia Tanzania ni nchi ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi cha utalii baada ya Brazil
Na ni kwa nini utalii?
Sekta ya utalii Tanzania, ndio sekta inayoongoza katika kuingiza fedha nyingi za kigeni kuliko sekta yeyote ile hapa Tanzania( 25%) ya fedha zote za kigeni( foreign currency) zinatokana na utalii, mfano mwaka 2018/ 2019 sekta hiyo iliingizia taifa takribani $ 2.4 bilioni, pia sekta ya utalii nchini inachangia takribani 17.6% ya pato ghafi la taifa(GDP), pia sekta ya utalii imetoa ajira za moja kwa moja takribani watu elfu sita na ajira zisizo za moja kwa moja takribani watu milioni mbili
Sasa kwa Tanzania ukanda pekee unaofanya vizuri katika utalii ni ukanda wa kaskazini, ambapo unaopokea watalii wengi kuliko kanda zingine za Kusini na Kanda ya Kaskazini magharibi, takribani 90% ya watalii wote wanaoingia hapa nchini wanaelekea ukanda wa Kaskazin
Sasa ili kufikia malengo ya kuongeza idadi ya watalii, serikali waliamua kufungua baadhi ya kanda zingine za za utalii, kanda hizo ni Kanda ya Kusini( mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe,Songwe) ambapo Kitulo ilipandishwa hadhi na kuwa hifadhi ya Kitulo, na kanda ya Kaskazini magharibi yenye mikoa ya ( Geita, Mwanza, Kagera, Kigoma)
Serikali walifanya nini kwa kanda ya Kaskazini magharibi?
Hatua ya kwanza waliofanya, kwanza ni kuyapandisha hadhi mapori tengefu ya Burigi, Biharamulo, Kimisi , Rumanyika & Kyerwa na kuwa hifadhi za taifa( National parks) Burigi- Chato, Rumanyika-Karagwe & Kyerwa
Sasa ili kuweza kuvutia watalii waweze kufika Kwan urahisi katika hifadhi hizo, serikali waliona ipo haja ya kujenga uwanja mkubwa wa kinataifa wa ndege katibu na maeneo hayo, ambapo watalii wataweza kufika kwa urahisi zaidi kuliko ilivyo sasakatika hifadhi hizo ambapo kuna hifadhi ya tatu kwa ukubwa hapa nchini( Burigi- Chato)baada ya Serengeti na Sellou
Kwa hiyo kwa kuzingatia umuhimu wa kukuza sekta ya utalii nchini, ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Chato una manufaa makubwa katika uchumi wetu