Umimi wa Serikali ya Rais Magufuli unaua umoja wa Kitaifa

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Jan 26, 2020
3,716
11,704
Serikali tuliyonayo kwa sasa ndio serikali ya kibinafsi zaidi na iliyojaa umimi kuliko nyingine zote zilizopata kutokea.

Ukifungilia vyombo vya habari muda wote utasikia "rais katoa pikipiki.......", "rais kajenga hospitali........", "rais anajenga SGR.........", "tunakushukuru rais kwa hiki au kile..…..", yaani kila kitu ni kumtukuza na kumsifu rais tu.

Haya hayatokei kwa bahati mbaya, binadamu wanajua ku 'survive', kwasasa wamemsoma rais na wanajua kuwa anapenda kutukuzwa na kusifiwa hivyo basi wanampta anachokitaka.

Madhara yake kwa taifa ni kuwa wananchi hawana 'sense of ownership' na kinachoendelea nchini mwao, hawaoni kuwa wao ni sehemu ya maendeleo ya nchi, wao hawana mchango wowote kwenye maendeleo ya nchi, ni kama vile rais anatoa hela zake binafsi mfukoni kufanya yale anayodaiwa kuyafanya.

Hali hii haina afya kwa umoja na mshikamano wa Taifa hili, serikali imeajiriwa na wananchi na ni muhimu kwa viongozi kulikumbuka hilo, wakati wa vita ya Kagera nchi nzima tulisimama pamoja, watu walijitolea kutoka vijijini huko wajiunge na jeshi ili wakaipoganie nchi yao, wengine walijitolea vyakula na hata magari yao, wale waliokataliwa kujiunga na jeshi labda kwa sababu za kiafya walilia machozi kwa kuikosa nafasi ya kwenda kuipigania nchi yao, haya yalitokea kwasababu mwalimu alikua na uwezo wa kuwafanya wananchi waione nchi kuwa ni yao, magumu ni yetu sote na mafanikio ni yetu sote.

Mnaolipwa mishahara ili kumshauri JPM fanyeni kazi yenu vizuri, adui wa nje mwenye nia mbaya anapata wasaa mzuri zaidi wa kuishambilia nchi pale ambapo hakuna umoja.

Tujiulize, leo hii JPM akifa (God forbid), au akikamatwa na ICC kimabavu, je kuna wananchi watafurahia mioyoni mwao au hata kufurahia waziwazi? Kama ukiona jibu ni ndio basi ujue tuko pabaya, matukio ya namna hiyo yanaposhindwa kuiunganisha nchi basi ni wazi kuwa nchi hiyo ina tatizo kubwa.
 
Kusifiwa ni miundombinu aliyoitengeneza, na ni propaganda nzuri anayoitumia kuonyesha kukubalika.

Kinachopotoshwa katika usifiaji ni kwamba usifiaji umepewa sura kuwa anayofanya jamaa anayafanya mwenyewe bila ya msaada wa mtu yoyote.
 
Kusifiwa ni miundombinu aliyoitengeneza, na ni propaganda nzuri anayoitumia kuonyesha kukubalika.

Kinachopotoshwa katika usifiaji ni kwamba usifiaji umepewa sura kuwa anayofanya jamaa anayafanya mwenyewe bila ya msaada wa mtu yoyote.
Ni mbaya sana hii, alafu eti anashangaa wapinzani wakimkosoa yeye zaidi, kama kilakitu umekipa sura yake sasa nani mwingine wakukosolewa zaidi yake?
 
Mkapa alijaribu kukemea hilo Suala hadharani lkn naona ilishashindikana,akaona ale buyu tu asije kugeuziwa kibao.
Nakumbuka alikemea mbele ya JPM, lakini tabia hii imeendelea na kukua zaidi, kama wanaomzunguka wana encourage tabia zake basi ni wazi atapuuzia maonyo ya wazee.
 
Mkapa alijaribu kukemea hilo Suala hadharani lkn naona ilishashindikana,akaona ale buyu tu asije kugeuziwa kibao.
Nakumbuka alikemea mbele ya JPM, lakini tabia ni kama waliomzunguka wana encourage tabia zake basi ni wazi atapuuzia maonyo ya wazee
Kiukweli huyu mwamba anasifiwa!
Sijawahi kuona, yaani kila Chombo cha habari utakachofungulia.
But too much is harmful.
Ni shida yaani, sasa hadi magari ya kubeba wagonjwa ya msaada wanawaambia wananchi JPM amewapa!
 
Kwani utakubali? Lkn unajua kwamba wewe ni Mmarangu, kwani wao ndio wenye chuki na wivu ndio maana hata Selasini (Mrombo) kaondoka chadema, shauri ya chuki na wivu wenu, ...
Unawahukumu bure hao wamarangu kwa chuki zako binafsi. Na inaonekana ndio sera yenu awamu ya tano, chuki za ukabila na ukanda.
 
Wewe ulitaka asifiwe dikteta Mbowe ? Huyu anayewakata mamilion wabunge wake na kwenda kula bata
Kiongozi kusifiwa haina shida, lakini kinachoendelea ni zaidi ya sifa, mnasahau kuwa ni kodi za wananchi ndio zinaleta maendeleo, serikali inasimamia tu. Sasa nyie kila kukicha JPM kaleta hiki, JPM kaleta kile... Ni mwendo wa kusifu na kuabudu. Haina afya hiyo tabia.
 
Back
Top Bottom