Umeshawahi kutapeliwa?

Umeshawahi kutapeliwa?

Charliemic

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2019
Posts
604
Reaction score
976
Hii ilinikumba 2016, nikiwa chuga! Huyu dogo nilimwopoa through Social Media tukajenga mazoea coz tulikuwa tunachat daily! Nikampanga weekend tukakutana town, tukakaa somewhere akala viepe yai akapiga soda!

Nikampa 20,000/= akalipie logde kisha anishtue through simu! Ilikiwa jirani na location tuliyokuwepo! Nikamsubiri dakika 20 nikaona kimya kumpigia hapatikani! Nikajua nimeliwa!!

Hebu tupe mkasa wako ulikuwaje!?
 
Mwaka 2005 kuna boya aliniuzia kipande cha jamaa pale chuga mtaa wa bondeni

Nakumbuka ndio ilikua mara ya kwanza nazama chuga na nlikua bado nyoka sema ujanja mwingi,ilikua msimu wa kuelekea xmass raia walikua wengi mbaya full msongamano,ghafla katokea jamaa kanisonga huku anaogea sauti ya chini "oya dogo kuna hii phone nimekwapua kwa boya ndani ya costa za moshi kaa vip nipe nusu bei m"

Sasa mm kwakua nilishaonywaga nisipende kua karibu na mtu usiemjua nikawa ata simjibu tena nikaongeza mwendo kuendelea na mitikasi yangu jamaa hakukata tamaa alivyoona simuelewi kachomoa bonge ya simu na kwa kipindi kile zilikua chache si ndio nikafanya kosa la kusimama niishangae kuuliza bei nikaambia toa elf70, uzuri mfukoni nilikua na elf8 tu nikamwambia sina ela.

Jamaa acha apunguze bei kutoka elf70 mpaka buku4 si nikampa akanikabidhi mzigo wangu ila akanionya nisifungue hapo hapo nikafungulie mbali maana mwenye simu yupo maeneo hayo nisije kamatwa nayo..

Nikaenda zangu panda basi la kurudia home nimepata siti si mzuka wa kufungua bahasha ukapanda kufungua mpaka nillishiwa nguvu yaan ni mche wa sabuni umechongwa chongwa ukawa na umbo la simu

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom