jamaikatz
JF-Expert Member
- Jul 11, 2023
- 369
- 1,255
Habari wanaJF,
Siku zote UMASKINI haufurahishi, unatesa, unadhalilisha na unaumiza sana unamfanya mtu adharauliwe, achukiwe na wakati mwingine hata kutengwa maskini hana rafiki.
Na pia kutokana na hali ngumu ya maisha ya umaskini wetu kuna muda huwezi kuzuia machozi yasitoke kutokana na majaribu unayopitia ila jambo moja la muhimu ni kwamba machozi yasibabaishe kwenye hiyo safari yako ukaishia njiani, lia kisha uchungu ukiisha futa machozi, simama endelea na safari yako mpaka kieleweke.
Usije ukatishwa na maisha mazuri ya wengine mtandaoni, mtandaoni mtu ata kuonyesha kile anachotaka ukione ila hataki kuonyesha uhalisia wa maisha yake.
Na hatukupewa maisha mazuri au mabaya, Mungu alitupa maisha tu,ni chaguo letu kuyafanya yawe mazuri au mabaya.
Na pia nisisahau kuna walio andaliwa na wazazi wao maisha bora alafu kuna akina sisi tunao waandalia wazazi wetu maisha bora, hatufanani kikubwa kuheshimiana tu.
Tusichoke kupambana ili tuu tokomeze umaskini.
Siku zote UMASKINI haufurahishi, unatesa, unadhalilisha na unaumiza sana unamfanya mtu adharauliwe, achukiwe na wakati mwingine hata kutengwa maskini hana rafiki.
Na pia kutokana na hali ngumu ya maisha ya umaskini wetu kuna muda huwezi kuzuia machozi yasitoke kutokana na majaribu unayopitia ila jambo moja la muhimu ni kwamba machozi yasibabaishe kwenye hiyo safari yako ukaishia njiani, lia kisha uchungu ukiisha futa machozi, simama endelea na safari yako mpaka kieleweke.
Usije ukatishwa na maisha mazuri ya wengine mtandaoni, mtandaoni mtu ata kuonyesha kile anachotaka ukione ila hataki kuonyesha uhalisia wa maisha yake.
Na hatukupewa maisha mazuri au mabaya, Mungu alitupa maisha tu,ni chaguo letu kuyafanya yawe mazuri au mabaya.
Na pia nisisahau kuna walio andaliwa na wazazi wao maisha bora alafu kuna akina sisi tunao waandalia wazazi wetu maisha bora, hatufanani kikubwa kuheshimiana tu.
Tusichoke kupambana ili tuu tokomeze umaskini.