Ultra Sound inauwezo wa kutambua jinsia ya mtoto aliye tumboni?

2991

JF-Expert Member
Feb 3, 2017
619
626
Habarini za j3 ladies and gentlemen, kwa sasa wife ni mjamzito na alikuwa anasumbuliwa saaana na tumbo hvyo baada ya kwenda hospital tukashauriwa afanye kipimo cha ultra sound ili wajue mtoto amekaaje na baada ya kucheki wakasema mtoto yuko poa bt daktari husika akamwambia wife kuwa image inaonyesha ni mtoto wa kiume.

kwa wataalam na wenye uelewa na uzoefu wa hii kitu je ni kweli ina huo uwezo ili nikae nikijua nina mtoto wa kiume?
 
Du kweli tunishi ulimwengu tofauti. Kuanzia wiki nane lakini kwa uhakika zaidi baada ya wiki ya 20 wanaweza kuona ama kujua jinsia ya mtoto.

Hongera ileeni mimba salama na nawakieni kila la kheri
 
Ni kweli, ukitaka utulie kwa uhakika mkienda tena waombe waangalie na kuwaambia. Pia itategemea mtoto amekaaje, kuna wakati wanageuka wanakuwa hawawezi kuona. Ulipoenda itakuwa mtoto alikaa vizuri kwa wao kuona. Hongera
 
Du kweli tunishi ulimwengu tofauti. Kuanzia wiki nane lakini kwa uhakika zaidi baada ya wiki ya 20 wanaweza kuona ama kujua jinsia ya mtoto.

Hongera ileeni mimba salama na nawakieni kila la kheri
nashukuru kufahamu, tulivyoenda alituambia ni weeks 32
 
Back
Top Bottom