Nyumba nyingi za vijijini pamoja na kuwa duni zimejengwa kwenye maeneo ambayo hayajapimwa ambayo ni maeneo yanayomilikiwa na ukoo au familia kama mashamba, hivyo hayana hati. Sasa hiyo kodi inayotozwa kwenye nyumba ya nyasi ambayo hata valuation yake haijulikani inakuwaje. Kama walivyochangia wadau huko juu ni kama kodi ya kichwa inarudi kwa utaratibu mwingine, maana hii ilikuwa haijali unaishi mjini au kijijini, maskini au siyo maskini, una kazi ya kukuingizia kipato au huna. Ila wakifanikiwa kuirudisha hiyo kodi ya kichwa, wasisahau kuondoa VAT kwenye bidhaa tunazonunua maana sasa tunarudi kwenye uchumi wa kijima tena......tumlazimishe!